< 2 Timotheo 4 >
1 Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
I charge thee, before God and Jesus Christ, who shall judge the living and the dead, by his coming, and his kingdom:
2 Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
Preach the word: be instant in season, out of season: reprove, entreat, rebuke in all patience and doctrine.
3 Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
For there shall be a time, when they will not endure sound doctrine; but, according to their own desires, they will heap to themselves teachers, having itching ears:
4 Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
And will indeed turn away their hearing from the truth, but will be turned unto fables.
5 Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
But be thou vigilant, labour in all things, do the work of an evangelist, fulfill thy ministry. Be sober.
6 Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
For I am even now ready to be sacrificed: and the time of my dissolution is at hand.
7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
I have fought a good fight, I have finished my course, I have kept the faith.
8 Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
As to the rest, there is laid up for me a crown of justice, which the Lord the just judge will render to me in that day: and not only to me, but to them also that love his coming.
9 Jitahidi kuja kwangu upesi
Make haste to come to me quickly.
10 kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn )
For Demas hath left me, loving this world, and is gone to Thessalonica: Crescens into Galatia, Titus into Dalmatia. (aiōn )
11 Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
Only Luke is with me. Take Mark, and bring him with thee: for he is profitable to me for the ministry.
12 Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
But Tychicus I have sent to Ephesus.
13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
The cloak that I left at Troas, with Carpus, when thou comest, bring with thee, and the books, especially the parchments.
14 Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
Alexander the coppersmith hath done me much evil: the Lord will reward him according to his works:
15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
Whom do thou also avoid, for he hath greatly withstood our words.
16 Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
At my first answer no man stood with me, but all forsook me: may it not be laid to their charge.
17 Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
But the Lord stood by me, and strengthened me, that by me the preaching may be accomplished, and that all the Gentiles may hear: and I was delivered out of the mouth of the lion.
18 Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
The Lord hath delivered me from every evil work: and will preserve me unto his heavenly kingdom, to whom be glory for ever and ever. Amen. (aiōn )
19 Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
Salute Prisca and Aquila, and the household of Onesiphorus.
20 Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
Erastus remained at Corinth. And Trophimus I left sick at Miletus.
21 Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
Make haste to come before winter Eubulus and Pudens, and Linus and Claudia, and all the brethren, salute thee.
22 Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.
The Lord Jesus Christ be with thy spirit. Grace be with you. Amen.