< 2 Timotheo 4 >

1 Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
这就是我在上帝和耶稣基督面前,指导你要做的事情。当耶稣基督到来并建立他的王国,将对活人和死人进行审判。
2 Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
无论是否方便,都要讲述上帝之道;如果人们犯错,要告诉他们,警告他们,鼓励他们。当你这样做时,要用极大的耐心进行教导。
3 Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
因为人们即将不再听得下真正的教导,那个时刻很快就会到来。到时候,他们会好奇地想要听不一样的教导,他们身边的老师,会讲述他们爱听的东西。
4 Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
他们不再聆听真理,反倒流连于谬误。
5 Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
你要时刻保持明智,忍受磨难,进行传福音的工作,完成你的职责。
6 Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
我即将被牺牲;我离世的时候即将到来。
7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
我已进行了一场良善的战斗,已跑完比赛,已坚持对上帝的信。
8 Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
现在有一个奖励留给了我,那是因遵循好事和正直良善而获得的冠冕。主(他是总能正确行事的法官)会在那一天给我这个冠冕。不只是给我,也给渴望他到来的所有人。
9 Jitahidi kuja kwangu upesi
请尽快到我这边来。。
10 kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn g165)
因为底马因贪恋现今的世界,已离开我去了帖撒罗尼迦。革勒士去了加拉太,提多去了达马太。 (aiōn g165)
11 Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
现在只有路加在我这里。请把马可带来,他可以帮助我的工作。
12 Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
我已派推基古到以弗所去。
13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
你来的时候,请带上我在特罗亚时留在加布那里的外衣。还有那些书,特别是那些羊皮书,也要带来。
14 Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
铜匠亚历山大给我带来了很多麻烦,愿主根据他的行为审判他。
15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
你也要提防他,因为他极力反对我所说的话。
16 Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
我第一次辩护的时候,没有一个人支持我,反而离开我。但愿他们不会因此而受到责备。
17 Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
但主站在我身边,给我力量,让我可以宣讲所有的福音信息,让所有外族人都能听见;他将我从狮口中救出来。
18 Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
主必救我脱离一切邪恶之事,也必带我安全进入他在天上的王国。愿荣耀永远归给他。阿门。 (aiōn g165)
19 Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
替我问候百基拉、亚居拉和阿尼色弗一家人。
20 Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
以拉都留在了哥林多。因为特罗非摩病了,我就留他在米利都。
21 Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
请尽可能在冬天前赶过来。友布罗、布田、利奴、革老底亚和所有兄弟姐妹都向你问候。
22 Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.
主与你同在。愿他的恩典与你们同在。

< 2 Timotheo 4 >