< 2 Timotheo 4 >
1 Nakuagiza mbele za Mungu na mbele za Kristo Yesu, atakayewahukumu watu walio hai na waliokufa wakati wa kuja kwake na ufalme wake, kwamba:
Pathen neh Khrih Jesuh hmaiah kang uen. A phoenah, a ram neh aka duek aka hing laitloek ham cai.
2 Hubiri Neno; kuwa tayari wakati ufaao na wakati usiofaa; karipia, kemea na utie moyo kwa uvumilivu wote na kwa mafundisho mazuri.
Ol te hoe pah. Na bihoep tamto akhaw pai thil laeh. Thinsennah thuituennah cungkuem neh toeltham lamtah, sim lamtah, hloep laeh.
3 Maana wakati utakuja watu watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kuyasikia.
Aka cuem thuituennah neh a yaknaem uh pawt vaengah ni a. tue a pai eh. Tedae a hoehhamnah bangla amamih kah hnavue aka thak saya rhoek te a kuk uh ni.
4 Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.
Te phoeiah oltak lamkah a hna te a khong uh vetih cil taengla mael uh ni.
5 Kwa habari yako wewe, vumilia mateso, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiza wajibu wote wa huduma yako.
Tedae nang tah a cungkuem ah cue uh lamtah olthangthen bibi te patang doeah saii. Na bibi te khaw ming lah.
6 Kwa maana mimi sasa ni tayari kumiminwa kama sadaka ya kinywaji, nayo saa yangu ya kuondoka imetimia.
Ka phum uh coeng tih ka voeinah tue khaw ha pai coeng.
7 Nimevipiga vita vizuri, mashindano nimeyamaliza, imani nimeilinda.
Aka then thingthuelnah te ka thingthuel coeng. Hma te ka khah coeng. Tangnah te ka kuem coeng.
8 Sasa nimewekewa taji ya haki ambayo Bwana, mwamuzi wa haki, atanitunukia siku ile: wala si mimi tu, bali pia wote ambao wamengoja kwa shauku kudhihirishwa kwake.
Tahae lamkah kai ham duengnah rhuisam te a khueh coeng. Te te aka dueng laitloekkung boeipa loh tekah khohnin ah kai n'thuung ni. Te phoeiah kai bueng pawt tih a phoenah aka lungnah rhoek boeih te khaw a paek ni.
9 Jitahidi kuja kwangu upesi
Kai taengah koe aka pawk la na haam mako.
10 kwa sababu Dema, kwa kuupenda ulimwengu, ameniacha na amekwenda Thesalonike. Kreske amekwenda Galatia na Tito amekwenda Dalmatia. (aiōn )
Demas loh kai n'phap tih ta kumhal kah he a lungnah. Te dongah Thessalonika la, Kresens te Galati la, Titu te Dalmatia la vik cet. (aiōn )
11 Ni Luka peke yake aliye hapa pamoja nami. Mtafute Marko uje naye kwa sababu ananifaa sana katika huduma yangu.
Ka taengah Luka bueng ni aka om. Marku te lo lamtah namah neh ha puei uh. Kai ham tah bibi dongah congpang koila om.
12 Nimemtuma Tikiko huko Efeso.
Tedae Tukhiko te Ephisa la ka tueih coeng.
13 Utakapokuja, niletee lile joho nililoliacha kwa Karpo huko Troa na vile vitabu vyangu, hasa vile vya ngozi.
Na lo vaengah Troas kah Karpuh taengah himbai neh cayol olpuei la maehpho ka khueh te hang khuen.
14 Aleksanda yule mfua chuma alinitendea ubaya mkubwa. Bwana atamlipa kwa ajili ya yale aliyotenda.
Rhohum aka bi Alexander loh kai soah thae muep a tueng sak. Boeipa loh anih te amah khoboe bangla a thuung bitni.
15 Wewe pia ujihadhari naye kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu.
Mamih kah olka te bahoeng a kamkaih dongah nang khaw anih te ngaithuen.
16 Katika utetezi wangu wa mara ya kwanza, hakuna hata mmoja aliyeniunga mkono, bali kila mmoja aliniacha. Namwomba Mungu wasihesabiwe hatia kwa jambo hilo.
Kai kah olthungnah lamhma vaengah kai taengla ha pawk uh pawh. Hlang boeih loh kai n'phap cakhaw amih te ngaiyaknah boel sih.
17 Lakini Bwana alisimama upande wangu akanitia nguvu, ili kupitia kwangu lile Neno lihubiriwe kwa ukamilifu, watu wote Mataifa wapate kulisikia. Mimi niliokolewa kutoka kinywa cha simba.
Tedae Boeipa loh kai m'pai puei tih kai n'thaphoh. Te daengah ni kai lamkah olhoe te a soep sak vetih namtom loh boeih a yaak eh. Te tlam ni sathueng ka lamloh n'hlawt.
18 Bwana ataniokoa katika kila shambulio baya na kunileta salama katika Ufalme wake wa mbinguni. Atukuzwe yeye milele na milele. Amen. (aiōn )
Boeipa loh khoboe thae boeih lamkah kai n'hlawt vetih vaan kah amah ram khuila n'daem sak ni. Amah te kumhal ah kumhal duela thangpomnah om saeh. Amen. (aiōn )
19 Wasalimu Prisila na Akila, na wote wa nyumbani kwa Onesiforo.
Priska neh Aquila, Onesiphor imkhuikho te toidal ne.
20 Erasto alibaki Korintho. Nami nikamwacha Trofimo huko Mileto akiwa mgonjwa.
Erastu te Kawrin ah om tih Trophimu te a tloh dongah Miletu ah ka khueh.
21 Jitahidi ufike huku kabla ya majira ya baridi. Eubulo anakusalimu, vivyo hivyo Pude, Lino, Klaudia na ndugu wote.
Sikca hlanah pawk hamla na haam mako. Ubuluh, Puden, Linu, Kalaudia neh manuca rhoek boeih loh nang kutn'tuuk uh.
22 Bwana awe pamoja na roho yako. Neema iwe pamoja nanyi. Amen.
Boeipa loh na mueihla te om puei saeh. Lungvatnah tah nangmih taengah om saeh.