< 2 Timotheo 3 >

1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
To pa védi, da v zadnjih dnevih nastanejo težki časi.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
Kajti ljudje bodejo samoljubni, lakomni, širokoustni, prevzetni, opravljivi, roditeljem nepokorni, nehvaležni, brezbožni,
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
Brezsrčni, nespravljivi, obrekljivi, nezmerni, grozoviti, nedobroljubni,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
Izdajalci, vrtoglavi, napihneni; veselje bolj ljubeči nego Boga,
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
Ki imajo podobo pobožnosti, moč pa njeno tajé; in teh se ogiblji!
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
Izmed teh namreč so oni, ki se plazijo v hiše in v pest dobivajo obložene z grehi ženščine, katere goni mnogotero poželenje,
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
Katere se vedno učé, in nikdar ne morejo priti do spoznanja resnice.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Enako pa, kakor sta Janez in Jambrez ustavljala se Mojzesu, tako se tudi tí ustavljajo resnici, ljudjé popačeni na umu, malopridni za vero.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
Ali napredovali ne bodo; kajti nespamet njihova bode vsem očita, kakor je bila tudi onih.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
Ti pa si hodil za menoj v uku, vedenji, nameri, veri, prizanesljivosti, ljubezni, stanovitnosti;
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
Preganjanjih, trpljenjih, kakošna so me zadela v Antijohiji, v Ikoniji, v Listrih; kakošna preganjanja sem prestal; in iz vsega me je otél Gospod.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
Vsi pa tudi, kateri hoté pobožno živeti v Kristusu Jezusu, bodo preganjani.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
Hudobni pa in sleparski ljudje bodo napredovali v slabem, varali bodo in varani.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
Ti pa ostani v tem, česar si se učil in se preveril, vedóč, od koga si se učil;
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
In da od mladih nóg póznaš sveta pisma, zmožna modriti te v zveličanje po veri, ki je v Kristusu Jezusu.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
Vsako pismo je od Boga navdihneno in koristno za uk, za svarjenje, za opominjanje, za vzrejo v pravici;
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
Da bode popoln človek Božji, pripraven za vsako dobro delo.

< 2 Timotheo 3 >