< 2 Timotheo 3 >
1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
Sabe porém isto, que nos últimos dias virão tempos difíceis.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
Pois haverá alguns que serão egoístas, gananciosos, presunçosos, soberbos, blasfemos, desobedientes a pais e a mães, ingratos, profanos,
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
sem afeto natural, irreconciliáveis, caluniadores, sem dominio próprio, cruéis, sem amor com os bons,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
traidores, precipitados, orgulhosos, que amam mais os prazeres que a Deus.
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
Eles têm uma aparência de devoção divina, mas negam o poder dela. Afasta-te desses também.
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
Pois dentre esses são os que entram pelas casas, e levam cativas as mulheres insensatas carregadas de pecados, levadas com vários maus desejos;
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
que sempre estão aprendendo, e jamais conseguem chegar ao conhecimento da verdade.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
E assim como Janes e Jambres se opuseram a Moisés, assim também esses se opõem a verdade; esses são corruptos de entendimento, e reprovados quanto à fé.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
Eles, porém, não avançarão; pois a insensatez deles será evidente a todos, como também foi a daqueles.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
Porém tu tens seguido a minha doutrina, conduta, intenção, fé, paciência, amor, perseverança,
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
perseguições, aflições; as quais me aconteceram em Antioquia, em Icônio e em Listra; tais perseguições sofri, e o Senhor me livrou de todas.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
E também todos os que querem viver devotamente em Cristo Jesus sofrerão perseguição.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
Mas os que são maus e enganadores irão de mal a pior, enganando e sendo enganados.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
Tu, porém, continua nas coisas que aprendeste e das quais foste convencido, pois sabes aqueles de quem as aprendeste.
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
e que desde tua infância conheceste as Sagradas Escrituras, que podem te fazer sábio para a salvação pela fé em Cristo Jesus.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
Toda a Escritura [é] divinamente inspirada e proveitosa para ensinar, para mostrar erros, para corrigir, e para instruir na justiça;
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
para que o homem de Deus seja completo, plenamente instruído para toda boa obra.