< 2 Timotheo 3 >

1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
But know this, that in the last days grievous times will come.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
For men will be lovers of themselves, lovers of money, boasters, proud, blasphemers, disobedient to parents, unthankful, unholy, without
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
natural affection, implacable, slanderers, incontinent, fierce, without love for what is good,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
betrayers, headstrong, puffed up, lovers of pleasure rather than lovers of God;
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
having a form of godliness, but denying the power thereof. And from these turn away.
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
For of these are they who creep into houses, and lead captive silly women laden with sins, led away by divers lusts,
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
ever learning, and never able to come to the full knowledge of the truth.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Now as Jannes and Jambres withstood Moses, so also do these withstand the truth; men corrupted in their minds, reprobate concerning the faith.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
But they will proceed no further; for their folly will be clearly manifest to all, as that of those men was.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
But thou art well acquainted with my teaching, manner of life, purpose, faith, long-suffering, love, patience,
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
persecutions, sufferings; what things came upon me at Antioch, at Iconium, at Lystra; what persecutions I endured, and out of them all the Lord delivered me.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
Yea, and all that desire to live godly in Christ Jesus will suffer persecution.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
But evil men and impostors will wax worse and worse, deceiving and being deceived.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
But do thou continue in the things which thou didst learn and wast assured of, knowing from what teachers thou didst learn them,
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
and that from a child thou hast known the Holy Scriptures, which are able to make thee wise unto salvation, through faith which is in Christ Jesus.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
All Scripture is inspired by God, and is profitable for teaching, for reproof, for correction, for discipline in righteousness;
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
that the man of God may be perfect, thoroughly furnished unto every good work.

< 2 Timotheo 3 >