< 2 Timotheo 3 >

1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
But know this: that in the last days, grievous times will come.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
For men will be lovers of self, lovers of money, boastful, arrogant, blasphemers, disobedient to parents, unthankful, unholy,
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
without natural affection, unforgiving, slanderers, without self-control, fierce, not lovers of good,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
traitors, headstrong, conceited, lovers of pleasure rather than lovers of God,
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
holding a form of godliness but having denied its power. Turn away from these, also.
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
For some of these are people who creep into houses and take captive gullible women loaded down with sins, led away by various lusts,
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
always learning and never able to come to the knowledge of the truth.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Even as Jannes and Jambres opposed Moses, so these also oppose the truth, men corrupted in mind, who concerning the faith are rejected.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
But they will proceed no further. For their folly will be evident to all men, as theirs also came to be.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
But you followed my teaching, conduct, purpose, faith, patience, love, steadfastness,
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
persecutions, and sufferings—those things that happened to me at Antioch, Iconium, and Lystra. I endured those persecutions. The Lord delivered me out of them all.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
Yes, and all who desire to live godly in Christ Jesus will suffer persecution.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
But evil men and impostors will grow worse and worse, deceiving and being deceived.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
But you remain in the things which you have learned and have been assured of, knowing from whom you have learned them.
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
From infancy, you have known the holy Scriptures which are able to make you wise for salvation through faith which is in Christ Jesus.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
Every Scripture is God-breathed and profitable for teaching, for reproof, for correction, and for instruction in righteousness,
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
that each person who belongs to God may be complete, thoroughly equipped for every good work.

< 2 Timotheo 3 >