< 2 Timotheo 3 >

1 Lakini yakupasa ufahamu jambo hili, kwamba siku za mwisho kutakuwa na nyakati za hatari.
Men vid dette, at i de sidste Dage skulle vanskelige Tider indtræde.
2 Kwa maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kumkufuru Mungu, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio watakatifu,
Thi Menneskene skulle være egenkærlige, pengegridske, praleriske, hovmodige, spottelystne, ulydige imod Forældre, utaknemmelige, ryggesløse,
3 wasio na upendo, wasiopenda kupatanishwa, wasingiziaji, wasiozuia tamaa zao, wakatili, wasiopenda mema,
ukærlige, uforligelige, bagtaleriske, uafholdne, rå, uden Kærlighed til det gode,
4 wasaliti, wakaidi, waliojaa majivuno, wapendao anasa zaidi kuliko kumpenda Mungu:
forræderske, fremfusende, opblæste, Mennesker, som mere elske Vellyst, end de elske Gud,
5 wakiwa na mfano wa utauwa kwa nje, lakini wakizikana nguvu za Mungu. Jiepushe na watu wa namna hiyo.
som have Gudfrygtigheds Skin, men have fornægtet dens Kraft. Og fra disse skal du vende dig bort!
6 Miongoni mwao wamo wale wajiingizao katika nyumba za watu na kuwachukua mateka wanawake wajinga, waliolemewa na dhambi zao na kuyumbishwa na aina zote za tamaa mbaya.
Thi til dem høre de, som snige sig ind i Husene og fange Kvindfolk, der ere belæssede med Synder og drives af mange Hånde Begæringer
7 Wakijifunza siku zote lakini kamwe wasiweze kufikia ujuzi wa kweli.
og altid lære og aldrig kunne komme til Sandheds Erkendelse.
8 Kama vile Yane na Yambre walivyopingana na Mose, vivyo hivyo watu hawa hupingana na ile kweli. Hawa ni watu wenye akili zilizopotoka, ambao wamekataliwa kwa mambo ya imani.
Men ligesom Jannes og Jambres stode Moses imod, således modstå også disse Sandheden: Mennesker, fordærvede i Sindet, forkastelige i Troen.
9 Lakini hawataendelea sana, kwa sababu upumbavu wao utakuwa dhahiri kwa watu wote, kama ulivyokuwa dhahiri upumbavu wa hao watu wawili.
Dog, de skulle ikke få Fremgang ydermere; thi deres Afsind skal blive åbenbart for alle, ligesom også hines blev.
10 Lakini wewe umeyajua mafundisho yangu, mwenendo, makusudi, imani, uvumilivu, upendo, ustahimilivu,
Du derimod har efterfulgt mig i Lære, i Vandel, i Forsæt, Tro, Langmodighed, Kærlighed, Udholdenhed,
11 mateso na taabu, yaani mambo yote yaliyonipata huko Antiokia, Ikonio na Listra, mateso yote niliyostahimili, lakini Bwana aliniokoa katika hayo yote.
i Forfølgelser, i Lidelser, sådanne, som ere komne over mig i Antiokia, i Ikonium, i Lystra, sådanne Forfølgelser, som jeg har udstået, og Herren har friet mig ud af dem alle.
12 Naam, yeyote anayetaka kuishi maisha ya utauwa ndani ya Kristo Yesu atateswa.
Ja, også alle de, som ville leve gudfrygtigt i Kristus Jesus, skulle forfølges.
13 Lakini watu waovu na wadanganyaji watazidi kuwa waovu, wakidanganya na kudanganyika.
Men onde Mennesker og Bedragere ville gå frem til det værre; de forføre og forføres.
14 Bali wewe, udumu katika yale uliyojifunza na kuyaamini kwa uthabiti, ukitambua ya kuwa ulijifunza hayo kutoka kwa nani,
Du derimod, bliv i det, som du har lært, og som du er bleven forvisset om, efterdi du ved, af hvem du har lært det,
15 na jinsi ambavyo tangu utoto umeyajua Maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukuhekimisha upate wokovu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu.
og efterdi du fra Barn af kender de hellige Skrifter, som kunne gøre dig viis til Frelse ved Troen på Kristus Jesus.
16 Kila Andiko limevuviwa na Mungu na lafaa kwa mafundisho, kwa kuwaonya watu makosa yao, kwa kuwaongoza na kwa kuwafundisha katika haki,
Hvert Skrift er indåndet af Gud og nyttig til Belæring, til Irettesættelse, til Forbedring, til Optugtelse i Retfærdighed,
17 ili mtu wa Mungu awe amekamilishwa, apate kutenda kila kazi njema.
for at Guds-Mennesket må vorde fuldkomment, dygtiggjort til al god Gerning.

< 2 Timotheo 3 >