< 2 Timotheo 2 >

1 Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
Pour toi donc, mon enfant, affermis-toi dans la grâce qui est dans le Christ Jésus.
2 Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
Et les enseignements que tu as reçus de moi en présence de nombreux témoins, confie-les à des hommes sûrs, qui soient capables d’en instruire d’autres.
3 Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
Prends ta part de la peine comme un brave soldat du Christ Jésus.
4 Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
Dans le métier des armes, nul ne s’embarrasse des affaires de la vie, s’il veut plaire à celui qui l’a enrôlé;
5 Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
et l’athlète n’obtient la couronne, que s’il a lutté selon les règles.
6 Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
Il faut que le laboureur travaille d’abord avant de recueillir les fruits.
7 Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
Réfléchis à ce que je te dis, car le Seigneur te donnera l’intelligence en toutes choses.
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
Souviens-toi que Jésus-Christ, issu de la race de David, est ressuscité d’entre les morts, d’après l’Evangile que je prêche,
9 ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
et pour lequel je souffre jusqu’à être enchaîné comme un malfaiteur; mais la parole de Dieu n’est pas enchaînée.
10 Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
C’est pourquoi je supporte tout à cause des élus, afin qu’eux aussi obtiennent le salut qui est dans le Christ Jésus, avec la gloire éternelle. (aiōnios g166)
11 Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
C’est là une parole certaine: si nous mourons avec lui, nous vivrons aussi avec lui;
12 Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
si nous persévérons dans l’épreuve, nous régnerons avec lui; si nous le renions, lui aussi nous reniera;
13 Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
si nous sommes infidèles, lui reste fidèle, car il ne peut se démentir.
14 Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
Voilà ce que tu dois rappeler, en conjurant devant le Seigneur d’éviter ces disputes de mots qui ne servent à rien, si ce n’est à la ruine de ceux qui les entendent.
15 Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
Éfforce-toi de te montrer dans le service de Dieu comme un homme éprouvé, un ouvrier qui n’a pas à rougir, dispensant avec droiture la parole de la vérité.
16 Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
Fuis les discours profanes et vains; car leurs auteurs iront toujours plus avant dans l’impiété,
17 Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
et leur parole fera des ravages comme la gangrène. De ce nombre sont Hyménée, et Philète,
18 ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
qui se sont éloignés de la vérité, en disant que la résurrection a déjà eu lieu, et qui renversent la foi de plusieurs.
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
Mais le solide fondement de Dieu demeure ferme, avec ce sceau: « Le Seigneur connaît ceux qui sont à lui »; et: « Qu’il s’éloigne de l’iniquité, celui qui prononce le nom du Seigneur. »
20 Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
Dans une grande maison, il n’y a pas seulement des vases d’or et d’argent, mais il y en a aussi de bois et de terre; les uns pour des usages honorables, les autres pour des usages vils.
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
Si donc quelqu’un s’est gardé pur de ces choses-là, il sera un vase d’honneur, sanctifié, utile à son maître, propre à toute bonne œuvre.
22 Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Fuis les passions de la jeunesse et recherche la justice, la foi, la charité et la paix, avec ceux qui invoquent le Seigneur d’un cœur pur.
23 Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
Rejette les questions folles et inutiles; tu sais qu’elles engendrent des disputes.
24 Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
Or il ne faut pas qu’un serviteur du Seigneur conteste; il doit, au contraire, avoir de la condescendance pour tous, savoir instruire et supporter,
25 Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
redressant avec douceur les opposants, dans l’espoir que Dieu leur donnera de se convertir à la connaissance de la vérité,
26 ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.
et que, revenus au bon sens, ils se dégageront des pièges du diable, qui les tient captifs et les asservit à ses volontés.

< 2 Timotheo 2 >