< 2 Timotheo 2 >

1 Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
Do you then, my son, strengthen you heart in the grace which is in Christ Jesus.
2 Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
The teachings which you have heard from me, attested by many witnesses, deliver into the keeping of faithful men, who in their turn will be able to teach others also.
3 Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
Take your share in suffering as a good soldier of Jesus Christ.
4 Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
A soldier in active service avoids entangling himself in the every- day affairs of life, so that he may please his commander.
5 Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
And again, an athlete is not crowned unless he obeys the rules of the game.
6 Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
The farmer who has done the work should be the first to get a share of the crop.
7 Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
Reflect on what I am telling you. The Lord will give you understanding in everything.
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
Always remember that Jesus Christ, a descendant of David, has been raised from the dead according to the gospel I proclaim.
9 ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
For preaching it I am suffering, and am even put in chains as a malefacter. But God’s message is no prisoner.
10 Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
That is why I endure everything for the sake of the chosen, that they also may obtain the salvation which is in Christ Jesus with eternal glory. (aiōnios g166)
11 Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
Faithful is the saying. "If we have died with him, we shall also live with him.
12 Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
If we endure suffering, we shall also reign with him. If we disown him, he too will disown us.
13 Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
If we prove faithless. he abides faithful, for he cannot be false to himself."
14 Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
Always call these truths to men’s mind; adjuring them in the presence of God to avoid controversy. It is a useless thing, and subverts those who listen to it.
15 Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
Strive earnestly to present yourself unto God, tested and proved worthy by trial, a workman unashamed, ever cutting a straight path for the message of the truth.
16 Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
but avoid profane babble; for people will go farther and farther in impiety,
17 Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
and their teaching will spread like a gangrene.
18 ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
Among such are Hymenaeus and Philetus, who have gone astray concerning the truth by declaring that the resurrection is already past; and they are undermining the faith of some.
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
Nevertheless God’s firm foundation stands unshaken, bearing this inscription, THE LORD KNOWS THOSE WHO ARE HIS, and this also, LET EVERY ONE WHO NAMES THE NAME OF THE LORD RENOUNCE WICKEDNESS.
20 Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
Now in a great house there are not only vessels of gold and silver, but also of wood and clay, some for noble, some for ignoble uses.
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
If then a man keeps himself clear of these latter, he will be a vessel for honor, consecrated, useful to the Master, prepared for every good work.
22 Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Flee from the passions of youth, but run after righteousness, faith, love, and peace, in company with those who out of a pure heart call upon the Lord.
23 Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
Ever shun foolish and puerile discussions, for you know that they lead to quarrels.
24 Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
The Lord’s slave must not quarrel, but must be kind to all men; a skilful teacher, patient of wrong.
25 Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
He must be gentle when instructing opponents; for possibly God may give them a change of mind for the recognition of the truth,
26 ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.
and they may come to their senses again, and escape the snare of the devil, as they are restored to life by God to do his will.

< 2 Timotheo 2 >