< 2 Timotheo 2 >

1 Basi, wewe mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo ndani ya Kristo Yesu.
So you, my son, be strengthened by the grace that is in Christ Jesus.
2 Nayo mambo yale uliyonisikia nikiyasema mbele ya mashahidi wengi, uwakabidhi watu waaminifu watakaoweza kuwafundisha watu wengine vilevile.
Also, the things that you have heard from me among many witnesses, commit the same to faithful men who will be competent to teach others also.
3 Vumilia taabu pamoja nasi kama askari mwema wa Kristo Yesu.
You therefore are to endure hardship as a good soldier of Jesus Christ.
4 Hakuna askari yeyote ambaye akiwa vitani hujishughulisha na mambo ya kawaida ya maisha haya kwa sababu nia yake ni kumpendeza yule aliyemwandika awe askari.
No one serving as a soldier gets entangled in the affairs of civilian life; he wants to please the one who enlisted him.
5 Vivyo hivyo, yeye ashindanaye katika michezo hawezi kupewa tuzo ya ushindi asiposhindana kulingana na kanuni za mashindano.
Further, if anyone competes in athletics, he is not crowned unless he competes according to the rules
6 Mkulima mwenye bidii ya kazi ndiye anayestahili kuwa wa kwanza kupata fungu la mavuno.
—the hardworking farmer should be the first to receive of the fruits.
7 Fikiri sana kuhusu haya nisemayo, kwa maana Bwana atakupa ufahamu katika mambo hayo yote.
Ponder what I am saying; may the Lord indeed give you understanding in it all.
8 Mkumbuke Yesu Kristo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yeye aliye wa uzao wa Daudi. Hii ndiyo Injili yangu,
Keep thinking of Jesus Christ, raised from the dead, of David's seed; this is my gospel,
9 ambayo kwayo ninateseka hata kufikia hatua ya kufungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu halifungwi.
for which I am suffering to the point of being in chains like a criminal, but the Word of God is not chained.
10 Kwa hiyo ninavumilia mambo yote kwa ajili ya wateule wa Mungu, kusudi wao nao wapate wokovu ulio katika Kristo Yesu, pamoja na utukufu wa milele. (aiōnios g166)
This is why I endure it all: for the sake of the chosen ones, that they also may obtain the salvation that is in Christ Jesus, with eternal glory. (aiōnios g166)
11 Hili ni neno la kuaminiwa: Kwa maana kama tumekufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
This is a trustworthy word: If, indeed, we died together, we will also live together;
12 Kama tukistahimili, pia tutatawala pamoja naye. Kama tukimkana yeye, naye atatukana sisi.
if we endure, we will also reign together; if we deny, He will also deny us;
13 Kama tusipoamini, yeye hudumu kuwa mwaminifu, kwa maana hawezi kujikana mwenyewe.
if we are faithless, He remains faithful —He is incapable of denying Himself.
14 Endelea kuwakumbusha mambo haya ukiwaonya mbele za Bwana waache kushindana kwa maneno ambayo hayana faida yoyote bali huwaangamiza tu wale wanaoyasikia.
Keep reiterating these things, exhorting them before the Lord not to argue about words to no useful purpose—it just ruins the hearers.
15 Jitahidi kujionyesha kwa Mungu kuwa umekubaliwa naye, mtendakazi asiye na sababu ya kuona aibu, ukilitumia kwa usahihi neno la kweli.
Make every effort to render yourself approved by God, a worker who does not need to be ashamed, handling the Word of the Truth correctly.
16 Jiepushe na maneno mabaya, yasiyo na maana, yasiyo ya utauwa, kwa maana hayo huzidi kuwatosa watu katika kukosa heshima kwa Mungu.
But shun godless, empty chatter, because those who do it will become increasingly godless,
17 Mafundisho yao yataenea kama kidonda kisichopona. Miongoni mwao wamo Himenayo na Fileto
and their word will spread like gangrene—among them are Hymenaeus and Philetus,
18 ambao wameiacha kweli, wakisema kwamba ufufuo wa wafu umekwisha kuwako, nao huharibu imani ya baadhi ya watu.
who have wandered away from the Truth, saying that the resurrection has already occurred; and they overturn the faith of some.
19 Lakini msingi wa Mungu ulio imara umesimama, ukiwa na muhuri wenye maandishi haya: “Bwana anawajua walio wake”; tena, “Kila alitajaye jina la Bwana, na auache uovu.”
Nevertheless, the solid foundation of God stands firm, having this seal: “The Lord knows those who are His,” and let everyone who claims the name of the Lord keep away from unrighteousness.
20 Katika nyumba kubwa si kwamba kuna vyombo vya dhahabu na fedha tu, bali pia vimo vyombo vya miti na vya udongo; vingine kwa matumizi maalum, na vingine kwa matumizi ya kawaida.
Now in a large house there are not only vessels of gold and silver, but also of wood and clay; some, to be sure, are for honor, but some are for dishonor.
21 Basi ikiwa mtu amejitakasa na kujitenga na hayo niliyoyataja, atakuwa chombo maalum, kilichotengwa na ambacho kinamfaa mwenye nyumba, kimeandaliwa tayari kwa kila kazi njema.
So if anyone cleanses himself from the latter, he will be a vessel for honor, sanctified and useful to the Master, prepared for every good work.
22 Zikimbie tamaa mbaya za ujana, ufuate haki, imani, upendo na amani pamoja na wale wamwitao Bwana kwa moyo safi.
Flee the lusts of youth; but pursue righteousness, faith, love, peace, along with those who call on the Lord out of a pure heart.
23 Jiepushe na mabishano ya kipumbavu na yasiyo na maana, kwa kuwa wajua ya kwamba hayo huzaa magomvi.
Refuse foolish and ignorant arguments, knowing that they breed quarrels.
24 Tena haimpasi mtumishi wa Bwana kuwa mgomvi, bali inampasa awe mwema kwa kila mtu, awezaye kufundisha, tena mvumilivu.
Now a slave of the Lord should not quarrel but be gentle towards all, skillful at teaching, forbearing,
25 Inampasa kuwaonya kwa upole wale wanaopingana naye, kwa matumaini kwamba Mungu atawajalia kutubu na kuijua kweli,
correcting courteously those who oppose him, in hopes that God may grant them repentance leading to a real knowledge of Truth,
26 ili fahamu zao ziwarudie tena, nao waponyoke katika mtego wa ibilisi ambaye amewateka wapate kufanya mapenzi yake.
and that they may retrieve their senses out of the devil's snare (having been taken captive by him to do his will).

< 2 Timotheo 2 >