< 2 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:
Poul, and Siluan, and Tymothe, to the chirche of Tessalonicensis, in God oure fadir,
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
and in the Lord Jhesu Crist, grace to you and pees of God, oure fadir, and of the Lord Jhesu Crist.
3 Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.
We owen to do thankyngis eueremore to God for you, britheren, so as it is worthi, for youre feith ouer wexith, and the charite of ech of you to othere aboundith.
4 Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.
So that we silf glorien in you in the chirchis of God, for youre pacience and feith in alle youre persecuciouns and tribulaciouns.
5 Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.
Whiche ye susteynen in to the ensaumple of the iust dom of God, that ye be had worthi in the kingdom of God, for which ye suffren.
6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi
If netheles it is iust tofor God to quite tribulacioun to hem that troblen you,
7 na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.
and to you that ben troblid, rest with vs in the schewing of the Lord Jhesu fro heuene, with aungelis of his vertu,
8 Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.
in the flawme of fier, that schal yyue veniaunce to hem that knowen not God, and that obeien not to the euangelie of oure Lord Jhesu Crist.
9 Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios g166)
Whiche schulen suffre euere lastinge peynes, in perischinge fro the face of the Lord, and fro the glorie of his vertu, (aiōnios g166)
10 siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.
whanne he schal come to be glorified in hise seyntis, and to be maad wondurful in alle men that bileueden, for oure witnessing is bileuyd on you, in that dai.
11 Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.
In which thing also we preien euere more for you, that oure God make you worthi to his cleping, and fille al the wille of his goodnesse, and the werk of feith in vertu;
12 Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
that the name of oure Lord Jhesu Crist be clarified in you, and ye in hym, bi the grace of oure Lord Jhesu Crist.

< 2 Wathesalonike 1 >