< 2 Wathesalonike 1 >
1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:
Paul and Siluanus, and Timotheus, vnto the Church of the Thessalonians, which is in God our Father, and in the Lord Iesus Christ:
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace be with you, and peace from God our Father, and from the Lord Iesus Christ.
3 Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.
We ought to thanke God alwayes for you, brethren, as it is meete, because that your faith groweth exceedingly, and the loue of euery one of you toward another, aboundeth,
4 Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.
So that we our selues reioyce of you in the Churches of God, because of your patience and faith in al your persecutions and tribulatios that ye suffer,
5 Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.
Which is a manifest token of the righteous iudgement of God, that ye may be counted worthy of the kingdome of God, for the which ye also suffer.
6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi
For it is a righteous thing with God, to recompense tribulation to them that trouble you,
7 na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.
And to you which are troubled, rest with vs, when the Lord Iesus shall shewe himselfe from heauen with his mightie Angels,
8 Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.
In flaming fire, rendring vengeance vnto them, that doe not know God, and which obey not vnto the Gospel of our Lord Iesus Christ,
9 Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios )
Which shall be punished with euerlasting perdition, from the presence of the Lord, and from the glory of his power, (aiōnios )
10 siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.
When he shall come to be glorified in his Saints, and to be made marueilous in all them that beleeue (because our testimonie toward you was beleeued) in that day.
11 Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.
Wherefore, we also pray alwayes for you, that our God may make you worthy of this calling, and fulfill all the good pleasure of his goodnes, and the worke of faith with power,
12 Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
That the Name of our Lord Iesus Christ may be glorified in you, and ye in him, according to the grace of our God, and of the Lord Iesus Christ.