< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
Dalje, braæo, molite se Bogu za nas da rijeè Gospodnja trèi, i da se slavi kao i meðu vama;
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
I da se izbavimo od besputnijeh i zlijeh ljudi; jer vjera nije sviju,
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
A Gospod je vjeran, koji æe vas utvrditi i saèuvati oda zla.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
A uzdamo se u Gospoda za vas da ono što vam zapovijedamo i èinite i èiniæete.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
A Gospod da upravi srca vaša na ljubav Božiju i na trpljenje Hristovo.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
Zapovijedamo vam pak, braæo, u ime Gospoda našega Isusa Hrista, da se odvojite od svakoga brata koji živi neuredno, a ne po uredbi koju primiše od nas.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
Jer sami znate kako treba da se ugledate na nas, jer ne življesmo neuredno meðu vama,
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
Niti zabadava hljeb jedosmo u koga, nego u trudu i u poslu, dan i noæ radeæi, da ne budemo na dosadu nikome od vas.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Ne kao da nemamo vlasti, nego da sebe damo vama za ugled, da budete kao i mi.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
Jer kad bijasmo u vas, ovo vam zapovijedasmo da ako ko neæe da radi da i ne jede.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
Jer èujemo da neki neuredno žive meðu vama, ništa ne radeæi, nego okrajèe i miješaju se u tuðe poslove.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Takovima zapovijedamo i molimo ih u Gospodu našemu Isusu Hristu da mirno radeæi svoj hljeb jedu.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
A vama, braæo, da ne dotuži dobro èiniti.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
A ako ko ne posluša rijeèi naše, onoga poslanicom naznaèite, i ne miješajte se s njim, da se posrami.
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Ali ga ne držite kao neprijatelja, nego ga svjetujte kao brata.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
A sam Gospod mira da vam da mir svagda u svakom dogaðaju. Gospod sa svima vama.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
Pozdrav mojom rukom Pavlovom, koje je znak u svakoj poslanici, ovako pišem:
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
Blagodat Gospoda našega Isusa Hrista sa svima vama. Amin.

< 2 Wathesalonike 3 >