< 2 Wathesalonike 3 >
1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
No demais, irmãos, rogae por nós, para que a palavra do Senhor tenha livre curso e seja glorificada, como tambem entre vós;
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
E para que sejamos livres de homens dissolutos e maus, porque a fé não é de todos.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
Mas fiel é o Senhor, que vos confortará, e guardará do maligno.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
E confiamos de vós no Senhor que tambem fazeis e fareis o que vos mandamos.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
Ora o Senhor encaminhe os vossos corações na caridade de Deus, e na paciencia de Christo.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
Mandamo-vos, porém, irmãos, em nome de nosso Senhor Jesus Christo, que vos aparteis de todo o irmão que andar desordenadamente, e não segundo a tradição que de nós recebeu.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
Porque vós mesmos sabeis como convém imitar-nos, pois que não nos houvemos desordenadamente entre vós:
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
Nem de graça comemos o pão de nenhum, mas com trabalho e fadiga, trabalhando noite e dia, para não sermos pesados a nenhum de vós.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Não porque não tivessemos auctoridade, mas para vos dar em nós mesmo exemplo, para nos imitardes.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
Porque, quando ainda estavamos comvosco, vos mandámos isto, que, se alguem não quizer trabalhar, não coma tambem.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
Porque ouvimos que alguns entre vós andam desordenadamente, não trabalhando, antes fazendo coisas vãs.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Aos taes, porém, mandamos, e admoestamos por nosso Senhor Jesus Christo, que, trabalhando com socego, comam o seu proprio pão.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
E vós, irmãos, não vos canceis de fazer bem.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
Porém, se alguem não obedecer á nossa palavra escripta n'esta carta, notae o tal, e não vos mistureis com elle, para que se envergonhe.
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Todavia não o tenhaes como inimigo, mas admoestae-o como irmão.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
Ora o mesmo Senhor da paz vos dê sempre paz em toda a maneira. O Senhor seja com todos vós.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
Saudação da minha propria mão, de mim, Paulo, que é o signal em todas as epistolas: assim escrevo.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
A graça de nosso Senhor Jesus Christo seja com todos vós. Amen.