< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
As for the rest, my brethren, pray for us, that the word of the Lord may run, and be glorified, as it is among you:
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
and that we may be delivered from unreasonable and wicked men; for all have not faith.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
But the Lord is faithful, who will establish you, and preserve you from the evil one.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
And we trust in the Lord concerning you, that ye both do and will do the things which we give you in charge.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
And may the Lord direct your hearts into the love of God, and into the patience of Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
Now we charge you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, to withdraw yourselves from every brother who walketh disorderly, and not according to the instruction which he received from us.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
For ye know how ye ought to imitate us: for we were not disorderly among you;
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
neither did we eat any one's bread for nothing; but with labor and toil, working night and day, that we might not be burthensome to any of you.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Not that we have not power, but that we might give ourselves as an example to you to imitate us.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
For when we were with you, we gave you this charge, if any will not work, neither let him eat.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
For we hear that there are some among you that walk disorderly, doing no work themselves, but very busy in the affairs of others.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Such we charge and exhort by our Lord Jesus Christ, that they work quietly and earn their own bread.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
But be not you, my brethren, discouraged from well-doing. And if any obey not our order,
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
by this epistle, mark such a one, and do not keep company with him, that he may be ashamed.
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
However do not look upon him as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
Now the Lord of peace himself give you peace at all times and in all places. The Lord be with you all.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
The salutation of me Paul by my own hand, which is the token in every epistle; for so I write,
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
"The grace of our Lord Jesus Christ be with you all." Amen.

< 2 Wathesalonike 3 >