< 2 Wathesalonike 3 >
1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
Finally, brothers, pray on for me, that God’s word may run swiftly, and be glorified as in your own case,
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
and that I may be delivered from unreasonable and wicked men; for all do not hold the faith.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
But the Lord is faithful; he will stablish you and guard you from the Evil One.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
Now we have fully fixed our faith on you in the Lord, that you are doing and will continue to do what we enjoin.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
May the Lord incline your hearts to the love of God and to the stedfastness of Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
I summon you, in the name of the Lord Jesus Christ, to shun any brother who leads an idle and disorderly life, which is not according to the rule you received from me.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
For you know well how you must imitate me. For I did not lead an idle or disorderly life among you;
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
I did not eat my food as a gift from any man, but in toil and travail, night and day, I worked, so that I might not be a burden to any of you.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Not that I have no right to such support; it was simply to give you an example for you to imitate.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
For indeed when I was with you, I used to charge you, "If any man will not work, he shall not eat."
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
But I hear that there are those of your number who are leading idle and disorderly lives, who are not busy, but mere busybodies.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Now all such I command and entreat, by the authority of the Lord Jesus Christ, to work in quietness. and to earn their own living.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
But you, brothers, must not grow weary in well-doing.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
If any man does not give heed to what I have said in this letter, mark that man; do not associate with him, so as to make him feel ashamed;
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
and yet do not count him as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
And may the Lord of peace himself give you peace at all times and in every way. The Lord be with you all.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
I, Paul, add this greeting in my own handwriting, which is my token in every letter. Thus I write -
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all.