< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
As to the rest, pray, brothers, concerning us, that the word of the LORD may run and may be glorified, as also with you,
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
and that we may be delivered from the unreasonable and evil men, for not all [are] of the faith;
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
but faithful is the LORD who will establish you, and will guard [you] from the evil [one];
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
and we now have confidence in the LORD, that which we command you both do and will do;
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
and the LORD direct your hearts to the love of God, and to the endurance of the Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
And we command you, brothers, in the Name of our Lord Jesus Christ, to withdraw yourselves from every brother walking disorderly, and not after the tradition that you received from us,
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
for you have known how it is necessary to imitate us, because we did not act disorderly among you;
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
nor did we eat bread of anyone for nothing, but in labor and in travail, working night and day, not to be chargeable to any of you;
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
not because we have no authority, but that we might give ourselves to you [as] a pattern, to imitate us;
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
for even when we were with you, this we commanded you, that if anyone is not willing to work, neither let him eat,
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
for we hear of some walking disorderly among you, working nothing, but being busybodies,
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
and such we command and exhort through our Lord Jesus Christ, that working with quietness, they may eat their own bread;
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
and you, brothers, may you not be weary doing well,
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
and if anyone does not obey our word through the letter, note this one, and have no company with him, that he may be ashamed,
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
and do not count as an enemy, but admonish as a brother;
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
and may the LORD of peace Himself always give to you peace in every way; the LORD [is] with you all!
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
The salutation by the hand of me, Paul, which is a sign in every letter; thus I write.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ [is] with you all! Amen.

< 2 Wathesalonike 3 >