< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
For the rest, brethren, pray for us, that the word of God may run, and may be glorified, even as among you;
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
And that we may be delivered from importunate and evil men; for all men have not faith.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
But God is faithful, who will strengthen and keep you from evil.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
And we have confidence concerning you in the Lord, that the things which we command, you both do, and will do.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
And the Lord direct your hearts, in the charity of God, and the patience of Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
And we charge you, brethren, in the name of our Lord Jesus Christ, that you withdraw yourselves from every brother walking disorderly, and not according to the tradition which they have received of us.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
For yourselves know how you ought to imitate us: for we were not disorderly among you;
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
Neither did we eat any man’s bread for nothing, but in labour and in toil we worked night and day, lest we should be chargeable to any of you.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Not as if we had not power: but that we might give ourselves a pattern unto you, to imitate us.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
For also when we were with you, this we declared to you: that, if any man will not work, neither let him eat.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
For we have heard there are some among you who walk disorderly, working not at all, but curiously meddling.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Now we charge them that are such, and beseech them by the Lord Jesus Christ, that, working with silence, they would eat their own bread.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
But you, brethren, be not weary in well doing.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
And if any man obey not our word by this epistle, note that man, and do not keep company with him, that he may be ashamed:
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
Yet do not esteem him as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
Now the Lord of peace himself give you everlasting peace in every place. The Lord be with you all.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
The salutation of Paul with my own hand; which is the sign in every epistle. So I write.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ be with you all. Amen.

< 2 Wathesalonike 3 >