< 2 Wathesalonike 3 >

1 Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili Neno la Bwana lipate kuenea kwa haraka na kuheshimiwa kila mahali, kama vile ilivyokuwa kwenu.
Finally, brothers, pray about us, so that the word of the Lord may run and be glorified, just as also with you,
2 Ombeni pia ili tupate kuokolewa kutokana na watu waovu na wabaya, kwa maana si wote wanaoamini.
and that we may be delivered from aberrant and wicked men, for the faith is not of all men.
3 Lakini Bwana ni mwaminifu, naye atawaimarisha ninyi na kuwalinda kutokana na yule mwovu.
But the Lord is faithful, who will establish you and will keep you from evil.
4 Nasi tuna tumaini katika Bwana ya kuwa mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaagiza.
And we are persuaded in the Lord toward you, that what we command you, ye both are doing and will do.
5 Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika saburi ya Kristo.
And may the Lord direct your hearts for the love of God, and for the steadfastness of the Christ.
6 Ndugu, tunawaagiza katika Jina la Bwana Yesu Kristo, jitengeni na kila ndugu ambaye ni mvivu na ambaye haishi kufuatana na maagizo tuliyowapa.
Now we command you, brothers, in the name of our Lord Jesus Christ, for you to withdraw from every brother who walks disorderly and not according to the tradition, which they received from us.
7 Maana ninyi wenyewe mnajua jinsi iwapasavyo kufuata mfano wetu. Sisi hatukuwa wavivu tulipokuwa pamoja nanyi,
For ye yourselves know how it is necessary to imitate us. Because we did not act disorderly among you,
8 wala hatukula chakula cha mtu yeyote pasipo kukilipia. Badala yake tulifanya kazi kwa bidii usiku na mchana, ili tusimlemee mtu yeyote miongoni mwenu.
nor did we eat bread gratis from any man, but in labor and toil, working night and day in order not to burden any of you.
9 Tulifanya hivi, si kwa sababu hatukuwa na haki ya kupata msaada kama huo, bali ndio sisi wenyewe tuwe kielelezo.
Not because we have no right, but that we might give ourselves an example to you, in order to imitate us.
10 Kwa maana hata tulipokuwa pamoja nanyi, tuliwapa amri kwamba: “Mtu yeyote asiyetaka kufanya kazi, hata kula asile.”
For even when we were with you we commanded you this, that if any man will not work, neither let him eat.
11 Kwa kuwa tunasikia kwamba baadhi ya watu miongoni mwenu ni wavivu. Hawafanyi kazi bali hujishughulisha na mambo ya wengine.
For we hear of some who walk among you disorderly, not working at all, but being busybodies.
12 Basi watu kama hao tunawaagiza na kuwahimiza katika Bwana Yesu Kristo, kwamba wafanye kazi kwa utulivu kwa ajili ya chakula chao wenyewe.
Now to such men we command and exhort by our Lord Jesus Christ, that, working with quietness, they should eat their own bread.
13 Kwa upande wenu, ndugu, ninyi kamwe msichoke katika kutenda mema.
But ye, brothers, do not become weary doing good.
14 Ikiwa mtu yeyote hayatii maagizo yetu yaliyoko katika barua hii, mwangalieni sana mtu huyo. Msishirikiane naye, ili apate kuona aibu.
And if any man does not obey our word by this letter, note that man, and do not associate with him, so that he may be ashamed.
15 Lakini msimhesabu kuwa adui, bali mwonyeni kama ndugu.
And yet do not regard him as an enemy, but admonish him as a brother.
16 Basi, Bwana wa amani mwenyewe awapeni amani nyakati zote na kwa kila njia. Bwana awe nanyi nyote.
Now may the Lord of peace himself give you peace through everything in every way. The Lord is with all of you.
17 Mimi, Paulo, ninaandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe. Hii ndio alama ya utambulisho katika barua zangu zote. Hivi ndivyo niandikavyo.
The salutation of Paul by my hand, which is a mark in every letter I write this way.
18 Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ is with all of you. Truly.

< 2 Wathesalonike 3 >