< 2 Wathesalonike 2 >

1 Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,
Now [I want to write to you] about the time when our Lord Jesus Christ will return and when [God] will gather us together to [where Jesus] is. My fellow believers, I urge you
2 msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.
that you think calmly [about any message] that [claims/says] that the Lord has [already] come again. Do not be shaken or alarmed/worried by any such message. [It does not matter] if [it is a message that someone claims God’s Spirit] revealed to him, or if [it is some other message that someone] has spoken, or whether [it is a message that someone claims] that I wrote in a letter.
3 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
Do not allow anyone to deceive you in any way [with the result that you believe any such message]. 2 Thessalonians 2:3b-5 [The Lord] will not come [MTY] [immediately]. First, [many people] [PRS] will rebel [against God]. The result of their rebelling will be that [they will accept and obey] the man who will sin very greatly [against God].
4 Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
He will be the [supreme] enemy [of God]. He will [proudly] exalt himself above everything that [people] consider to be some god and above everything that people worship. [As a result of wanting people to worship him], he will [even enter] God’s Temple and sit down [there to rule]. He will publicly proclaim that he himself is God! But [God] will [certainly] punish that man forever!
5 Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?
(I am sure that you remember that I kept telling you these things while I was still with you [there in Thessalonica]./Do you not remember that I continued telling you these things while I was still with you [there in Thessalonica]?) [RHQ]
6 Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.
You also know that there is something (OR, someone) that is preventing this man [from being revealed] {[from revealing himself]}. This man is being (held back/restrained) [now] for him to be revealed {that he reveal himself} at the time that [God has planned] [MTY].
7 Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
[Although Satan] is already secretly causing [people] to reject [God’s] laws, (the one/God) who is preventing [this man from revealing himself] now [will continue to prevent him from doing that] until he/[God] removes him.
8 Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.
It is then that [God will allow] this man, who rejects [God’s] laws [completely], to be revealed {to reveal himself}. Then the Lord Jesus will destroy him, by simply commanding it [MTY]. Jesus, by his own glorious arrival, will cause him to become [completely] powerless.
9 Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,
But [before Jesus destroys him], Satan will make him very powerful. As a result, he [will do all kinds of supernatural] miracles and amazing things [DOU] that will seem as though [God has enabled him to do them].
10 na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
And by doing wicked [things], he will completely deceive those who will [certainly] (perish/go to hell). [He will deceive them] because they will have refused to love the true [message]. So they will not be saved {God will not save them}. (questioned)
11 Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,
So, God, by his power, will enable this man to easily deceive people, so that they will believe what [this man] falsely [claims/says that he is].
12 na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.
The result will be that everyone will be [rightly] condemned {that [God] will [justly] condemn everyone} [to be punished] who did not believe the true [message], but who instead gladly chose [to be doing] what is wicked.
13 Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
[Our] fellow believers, whom our Lord [Jesus] loves, we thank God very frequently for you. It is appropriate/right for us to do that, because God chose you (from the beginning [MTY] [of creation/before the world existed]) in order that he might save [you] as a result of [your] believing the true [message] and as a result of [God’s] Spirit setting you apart [for God].
14 Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo.
[We thank God that] he chose you as a result of our [proclaiming] the message about Christ [to you], in order that you might (share in/have) some of the glory that our Lord Jesus Christ has.
15 Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.
So, [our fellow believers, continue to be firm concerning what you believe]; that is, continue believing the [true] teaching that we gave to you by our speaking to you and by our [writing] a letter [to you].
16 Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios g166)
Our Lord Jesus Christ himself and God, our Father, loves us and encourages us and causes us to confidently expect [to receive] the eternal things that [he has promised to give to us] as a result of [Christ] acting kindly toward us in a way we did not deserve. (aiōnios g166)
17 awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.
[We strongly pray that] God and Jesus together will encourage you! And we pray that they will cause you to continue doing and saying things that God considers to be good.

< 2 Wathesalonike 2 >