< 2 Wathesalonike 2 >
1 Ndugu, kuhusu kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo na kukusanyika kwetu pamoja mbele zake, tunawasihi,
But we beseech of you, my brethren, as it regards the coming of our Lord Jeshu Meshiha, and our assemblage with him,
2 msiyumbishwe kwa urahisi wala msitiwe wasiwasi na roho wala neno au barua inayosemekana kuwa imetoka kwetu, isemayo kwamba siku ya Bwana imekwisha kuwako.
that you be not soon moved in your minds, nor perturbed, nor by word, nor by spirit, nor by letter, which (may be) as (if it were) from us, that, Behold, the day of our Lord cometh!
3 Mtu yeyote na asiwadanganye kwa namna yoyote kwa maana siku ile haitakuja mpaka uasi utokee kwanza, na yule mtu wa kuasi adhihirishwe, yule ambaye amehukumiwa kuangamizwa kabisa.
Let no one deceive you by any one of the methods, because unless there shall come first the rebellion, and there be revealed the man of sin, the son of perdition;
4 Yeye atapingana na kujitukuza juu ya kila kitu kiitwacho Mungu au kinachoabudiwa, ili kujiweka juu katika Hekalu la Mungu, akijitangaza mwenyewe kuwa ndiye Mungu.
He who is the adversary, and is exalted over all who is called God and Venerable; so that also in the temple of Aloha as Aloha he will sit, and will make manifest of himself as that he is Aloha.
5 Je, hamkumbuki ya kwamba nilipokuwa pamoja nanyi niliwaambia mambo haya?
Do you not remember, that, when I was with you, these I told you?
6 Nanyi sasa mnajua kinachomzuia, ili apate kudhihirishwa wakati wake utakapowadia.
And now you know what holdeth, that he may be revealed in his time.
7 Maana ile nguvu ya siri ya uasi tayari inatenda kazi, lakini yule anayeizuia ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapoondolewa.
For the mystery of iniquity already beginneth to be effective; only if that which now holdeth be taken from the midst,
8 Hapo ndipo yule mwasi atafunuliwa, ambaye Bwana Yesu atamteketeza kwa pumzi ya kinywa chake na kumwangamiza kabisa kwa utukufu wa kuja kwake.
then will be revealed that evil one, whom our Lord Jeshu will consume by the spirit of his mouth, and will abolish by the revelation of his advent.
9 Kuja kwa yule mwasi kutaonekana kana kwamba ni kutenda kazi kwake Shetani ambaye hutumia nguvu zote, ishara, maajabu ya uongo,
For the coming of that (wicked one) is the working of Satana, with all power, and (with) signs and false miracles,
10 na kila aina ya uovu kwa wale wanaoangamia kwa sababu walikataa kuipenda kweli wapate kuokolewa.
and with all unrighteous deception which is done in them who perish, because they have not received the love of the truth by which they might have been saved.
11 Kwa sababu hii, Mungu ameruhusu watawaliwe na nguvu ya udanganyifu, ili waendelee kuamini uongo,
Wherefore Aloha will send them the working of deception,
12 na wahukumiwe wote ambao hawakuiamini ile kweli, bali wamefurahia uovu.
that they will believe the lie, and all of them will be judged who have not believed in the truth, but have had pleasure in unrighteousness.
13 Lakini imetupasa sisi kumshukuru Mungu daima kwa ajili yenu, ndugu mpendwao na Bwana, kwa sababu Mungu aliwachagua ninyi tangu mwanzo ili mwokolewe kwa kutakaswa na Roho kwa kuiamini kweli.
But we are bound to give thanks unto Aloha at all time for you, our brethren, beloved in our Lord, because Aloha hath chosen you from the beginning unto salvation, by sanctification of the Spirit, and by the belief of the truth.
14 Kwa kusudi hili Mungu aliwaita kwa njia ya kuhubiri kwetu Injili, ili mpate kushiriki katika utukufu wa Bwana Yesu Kristo.
For unto these Aloha called you by our preaching, that you should be the glory of our Lord Jeshu Meshiha.
15 Hivyo basi, ndugu wapendwa, simameni imara na myashike sana yale mafundisho tuliyowapa ikiwa ni kwa maneno ya kinywa au kwa barua.
Wherefore, my brethren, stand fast, and persevere in the precepts which you have been taught, whether by word, or by our epistle.
16 Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe na Mungu Baba yetu, aliyetupenda na kwa neema yake akatupatia faraja ya milele na tumaini jema, (aiōnios )
But our Lord Jeshu Meshiha himself, and Aloha our Father, who hath loved us, and given us everlasting consolation, and a good hope through grace, (aiōnios )
17 awafariji mioyo yenu na kuwaimarisha katika kila neno na tendo jema.
will comfort your hearts, and establish in every word and in every work of good.