< 2 Wathesalonike 1 >

1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:
Paul, Silvanus, and Timothy, to the church of the Thessalonians in God our Father and the Lord Jesus Christ:
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.
We ought always to give thanks to God for you, brothers, as is only fitting, because your faith is greatly increasing and the love that each of you has for one another is abounding.
4 Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.
As a result we ourselves boast about you in the churches of God for your perseverance and faithfulness in all the persecutions and tribulations that you are enduring.
5 Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.
This is evidence of the righteous judgment of God, and it is happening so that you may be considered worthy of the kingdom of God, for which you are suffering.
6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi
It is indeed right for God to repay with affliction those who afflict you,
7 na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.
and to give to you who are being afflicted relief along with us at the revelation of the Lord Jesus from heaven with his mighty angels.
8 Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.
With flaming fire he will inflict vengeance on those who do not know God and who do not obey the gospel of our Lord Jesus.
9 Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios g166)
They will suffer the punishment of eternal destruction, separated from the presence of the Lord and from the glory of his might, (aiōnios g166)
10 siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.
on that day when he comes to be glorified by his saints and to be marveled at by all who have believed, including you, because you have believed our testimony.
11 Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.
With this in mind, we always pray for you that our God will make you worthy of his calling and by his power bring to fulfillment every good intention and work of faith,
12 Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
so that the name of our Lord Jesus will be glorified in you, and you in him, according to the grace of our God and Lord, Jesus Christ.

< 2 Wathesalonike 1 >