< 2 Wathesalonike 1 >
1 Paulo, Silvano na Timotheo: Kwa kanisa la Wathesalonike mlio katika Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo:
Paul, and Silvanus, and Timothy, unto the Church of the Thessalonians in God our Father and the Lord Jesus Christ.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba na Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God our Father and our Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, imetubidi kumshukuru Mungu kwa ajili yenu siku zote, kama ulivyo wajibu wetu, kwa sababu imani yenu inakua zaidi na zaidi na upendo wa kila mmoja wenu alio nao kwa mwenzake unazidi kuongezeka.
We ought always to give thanks to God for you, brethren, as it is worthy, because your faith increases, and the divine love of each one of you all towards one another abounds more and more;
4 Ndiyo sababu miongoni mwa makanisa ya Mungu, tunajivuna kuhusu saburi yenu na imani mliyo nayo katika mateso yote na dhiki mnazostahimili.
so that we ourselves rejoice over you in the churches of God, on account of your patience and faith in all your persecutions and tribulations which you endure;
5 Haya yote ni uthibitisho kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na kwa sababu hiyo ninyi mtahesabiwa kwamba mnastahili kuwa wa Ufalme wa Mungu, mnaoteswa kwa ajili wake.
the manifestation of the righteous judgment of God, that you may be counted worthy of the kingdom of God, for which you indeed suffer:
6 Mungu ni mwenye haki: yeye atawalipa mateso wale wawatesao ninyi
if indeed it is a righteous thing with God to recompense tribulation to them who are troubling you,
7 na kuwapa ninyi mnaoteseka raha pamoja na sisi, wakati Bwana Yesu atakapodhihirishwa kutoka mbinguni katika mwali wa moto pamoja na malaika wake wenye nguvu.
and to you who are troubled, rest with us, in the revelation of the Lord Jesus from heaven with the angels of his power
8 Atawaadhibu wale wasiomjua Mungu na ambao hawakuitii Injili ya Bwana wetu Yesu.
in the fire of flame, dispensing vengeance to those who know not God, and to those who do not obey the gospel of our Lord Jesus:
9 Wataadhibiwa kwa uangamivu wa milele na kutengwa na uso wa Bwana na utukufu wa uweza wake, (aiōnios )
who shall suffer vengeance, eternal destruction from the face of the Lord and from the glory of his might, (aiōnios )
10 siku hiyo atakapokuja kutukuzwa katika watakatifu wake na kustaajabiwa miongoni mwa wote walioamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwa hawa kwa sababu mliamini ushuhuda wetu kwenu.
when he may come to be glorified among his saints, and among all those who believe, to be wondered at in that day, because our testimony was believed by you.
11 Kwa sababu hii, tunawaombea ninyi bila kukoma, ili Mungu apate kuwahesabu kuwa mnastahili wito wake na kwamba kwa uwezo wake apate kutimiza kila kusudi lenu jema na kila tendo linaloongozwa na imani yenu.
Unto which indeed we are praying incessantly for you, in order that our God may count you worthy of the calling, and may fulfill all the good pleasure of his goodness and work of faith, with power;
12 Tunaomba hivi ili Jina la Bwana wetu Yesu lipate kutukuzwa ndani yenu, nanyi ndani yake, kulingana na neema ya Mungu wetu na Bwana Yesu Kristo.
in order that the name of our Lord Jesus may be glorified in you, and you in him, according to the grace of our God and our Lord Jesus Christ.