< 2 Samweli 1 >

1 Baada ya kifo cha Sauli, Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwashinda Waamaleki, Daudi alikaa siku mbili huko Siklagi.
Saul'un ölümünden sonra Amalekliler'e karşı kazandığı zaferden dönen Davut Ziklak'ta iki gün kaldı.
2 Siku ya tatu akaja mtu mwenye nguo zilizoraruka na mavumbi kichwani mwake kutoka kwenye kambi ya Sauli. Alipomjia Daudi, akajitupa chini ili kumpa heshima.
Üçüncü gün, Saul'un ordugahından giysileri yırtılmış, başı toz toprak içinde bir adam geldi. Adam Davut'a yaklaşınca önünde yere kapandı.
3 Daudi akamuuliza, “Wewe umetoka wapi?” Akamjibu, “Nimetoroka kutoka kambi ya Waisraeli.”
Davut, “Nereden geliyorsun?” diye sordu. Adam, “İsrail ordugahından kaçıp kurtuldum” dedi.
4 Daudi akamuuliza, “Ni nini kilichotokea? Niambie.” Akasema, “Watu walikimbia kutoka vitani. Wengi wao walianguka na kufa. Naye Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa.”
Davut, “Ne oldu? Bana anlat” dedi. Adam askerlerin savaş alanından kaçtığını, birçoğunun düşüp öldüğünü, Saul'la oğlu Yonatan'ın da ölüler arasında olduğunu anlattı.
5 Ndipo Daudi akamwambia huyo kijana aliyemletea taarifa, “Je, umefahamuje kwamba Sauli na Yonathani mwanawe wamekufa?”
Davut, kendisine haberi veren genç adama, “Saul'la oğlu Yonatan'ın öldüğünü nereden biliyorsun?” diye sordu.
6 Yule kijana akasema, “Nilijipata huko Mlima Gilboa, naye Sauli alikuwa huko akiegemea mkuki wake, na magari ya vita na wapanda farasi wa upande wa adui wakawa wamemkaribia sana.
Genç adam şöyle yanıtladı: “Bir rastlantı sonucu Gilboa Dağı'ndaydım. Saul mızrağına dayanmıştı. Atlılarla savaş arabaları ona doğru yaklaşıyordu.
7 Alipogeuka na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Je, nifanye nini?’
Saul arkasına dönüp beni görünce seslendi. Ben de, ‘Buyrun, buradayım’ dedim.
8 “Akaniuliza, ‘Wewe ni nani?’ “Nikamjibu, ‘Mimi ni Mwamaleki.’
“Saul, ‘Sen kimsin?’ diye sordu. “‘Ben bir Amalekli'yim’ diye yanıtladım.
9 “Kisha akaniambia, ‘Nikaribie mimi na uniue! Niko katika maumivu makali ya kifo, lakini bado ningali hai.’
“Saul, ‘Ne olur üstüme var ve beni öldür!’ dedi, ‘Çünkü çektiğim acılardan kurtulmak istiyorum.’
10 “Kwa hiyo nikamkaribia nikamuua, kwa sababu nilijua kwamba baada ya kuanguka hangeweza kupona. Nami nikachukua lile taji lililokuwa kichwani mwake na utepe uliokuwa mkononi mwake nami nimevileta hapa kwa bwana wangu.”
Bu yüzden varıp onu öldürdüm. Çünkü yere düştükten sonra yaşayamayacağını biliyordum. Başındaki taçla kolundaki bileziği aldım ve onları buraya, efendime getirdim.”
11 Ndipo Daudi pamoja na watu wote waliokuwa pamoja naye wakazishika nguo zao na kuzirarua.
Bunun üzerine Davut'la yanındakiler giysilerini yırttılar.
12 Wakaomboleza, wakalia pia na kufunga mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwanawe, kwa ajili ya jeshi la Bwana na nyumba ya Israeli, kwa sababu wameanguka kwa upanga.
Kılıçtan geçirilen Saul, oğlu Yonatan ve RAB'bin halkı olan İsrailliler için akşama dek yas tutup ağladılar, oruç tuttular.
13 Daudi akamwambia yule kijana aliyemletea taarifa, “Wewe ni mwenyeji wa wapi?” Akamjibu, “Mimi ni mwana wa mgeni, Mwamaleki.”
Davut, kendisine haber getiren genç adama, “Nerelisin?” diye sordu. Adam, “Ben yabancıyım, bir Amalekli'nin oğluyum” dedi.
14 Daudi akamuuliza, “Kwa nini hukuogopa kuinua mkono wako ili kumwangamiza mpakwa mafuta wa Bwana?”
Davut, “RAB'bin meshettiği kişiye el kaldırıp onu yok etmekten korkmadın mı?” diye sordu.
15 Kisha Daudi akamwita mmoja wa watu wake na kumwambia, “Nenda ukamuue!” Kwa hiyo akampiga, naye akafa.
Sonra adamlarından birini çağırıp, “Git, öldür onu!” diye buyurdu. Böylece adam Amalekli'yi vurup öldürdü.
16 Kwa maana Daudi alikuwa amemwambia, “Damu yako iwe juu ya kichwa chako mwenyewe. Kinywa chako mwenyewe kimeshuhudia dhidi yako uliposema, ‘Nilimuua mpakwa mafuta wa Bwana.’”
Davut Amalekli'ye, “Kanından sen kendin sorumlusun” demişti, “Çünkü ‘RAB'bin meshettiği kişiyi ben öldürdüm’ demekle kendine karşı ağzınla tanıklıkta bulundun.”
17 Daudi akafanya maombolezo haya kuhusu Sauli na Yonathani mwanawe,
Davut Saul'la oğlu Yonatan için ağıt yaktı.
18 naye akaagiza kwamba watu wa Yuda wafundishwe ombolezo hili la upinde (ambalo limeandikwa katika Kitabu cha Yashari):
Sonra Yaşar Kitabı'nda yazılan Yay adındaki ağıtın Yahuda halkına öğretilmesini buyurdu:
19 “Walio fahari yako, ee Israeli, wameuawa juu ya mahali pako palipoinuka. Jinsi wenye nguvu walivyoanguka!
“Ey İsrail, senin yüceliğin yüksek tepelerinde yok oldu! Güçlüler nasıl da yere serildi!
20 “Msilisimulie hili katika Gathi, msilitangaze hili katika barabara za Ashkeloni, binti za Wafilisti wasije wakafurahia, binti za hao wasiotahiriwa wasije wakashangilia.
Haberi ne Gat'a duyurun, Ne de Aşkelon sokaklarında yayın. Öyle ki, ne Filistliler'in kızları sevinsin, Ne de sünnetsizlerin kızları coşsun.
21 “Enyi milima ya Gilboa, msipate umande wala mvua, wala mashamba yazaayo sadaka ya nafaka. Kwa maana huko ndiko ngao ya mwenye nguvu iliponajisiwa, ngao ya Sauli haitapakwa tena mafuta.
Ey Gilboa dağları, Üzerinize ne çiy ne de yağmur düşsün. Ürün veren tarlalarınız olmasın. Çünkü güçlünün kalkanı, Bir daha yağ sürülmeyecek olan Saul'un kalkanı Orada bir yana atıldı!
22 Kutokana na damu ya waliouawa, kutokana na miili ya wenye nguvu, ule upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma. Upanga wa Sauli haukurudi bure.
Yonatan'ın yayı yere serilmişlerin kanından, Yiğitlerin bedenlerinden hiç geri çekilmedi. Saul'un kılıcı hiç boşa savrulmadı.
23 “Sauli na Yonathani, maishani walipendwa na kuneemeka, na katika kifo hawakutengana. Walikuwa wepesi kuliko tai, walikuwa na nguvu kuliko simba.
Saul'la Yonatan tatlı ve sevimliydiler, Yaşamda da ölümde de ayrılmadılar. Kartallardan daha çevik, Aslanlardan daha güçlüydüler.
24 “Enyi binti za Israeli, lieni kwa ajili ya Sauli, ambaye aliwavika nguo nyekundu na maridadi, ambaye aliremba mavazi yenu kwa mapambo ya dhahabu.
Ey İsrail kızları! Sizi al renkli, süslü giysilerle donatan, Giysinizi altın süslerle bezeyen Saul için ağlayın!
25 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka vitani! Yonathani ameuawa mahali pako palipoinuka.
Güçlüler nasıl da yere serildi savaşta! Yonatan senin yüksek tepelerinde ölü yatıyor.
26 Nahuzunika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu, kwangu ulikuwa mpendwa sana. Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu, wa ajabu zaidi kuliko ule wa wanawake.
Senin için üzgünüm, kardeşim Yonatan. Benim için çok değerliydin. Sevgin kadın sevgisinden daha üstündü.
27 “Tazama jinsi mashujaa walivyoanguka! Silaha za vita zimeangamia!”
Güçlüler nasıl da yere serildi! Savaş silahları yok oldu!”

< 2 Samweli 1 >