< 2 Samweli 9 >

1 Daudi akauliza, “Je, hakuna mtu hata mmoja wa nyumba ya Sauli aliyebaki ambaye naweza kumtendea wema kwa ajili ya Yonathani?”
Un Dāvids sacīja: vai vēl ir kāds, kas atlicies no Saula nama, ka es tam žēlastību parādu Jonatāna dēļ?
2 Basi palikuwepo mtumishi wa nyumba ya Sauli aliyeitwa Siba. Wakamwita aje mbele ya Daudi, naye mfalme akamwambia, “Wewe ndiwe Siba?” Akamjibu, “Naam, mimi ndiye mtumishi wako.”
Un Saula namam bija kalps, Cībus vārdā, un tas tapa aicināts Dāvida priekšā. Un ķēniņš uz to sacīja: vai tu esi Cībus? Un viņš sacīja: esmu, tavs kalps.
3 Mfalme akauliza, “Je, hakuna yeyote ambaye amebaki wa nyumba ya Sauli ninayeweza kumwonyesha wema wa Mungu?” Siba akamjibu mfalme, “Bado yupo mwana wa Yonathani, yeye ni kiwete miguu yote.”
Un ķēniņš sacīja: vai vēl kāds nav no Saula nama, ka es Dieva žēlastību tam parādu? Un Cībus sacīja uz ķēniņu: Vēl ir viens Jonatāna dēls, tizls uz abām kājām.
4 Mfalme akauliza, “Yuko wapi?” Siba akajibu, “Yuko nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli huko Lo-Debari.”
Un ķēniņš uz to sacīja: kur tas ir? Un Cībus sacīja uz ķēniņu: redzi, viņš ir Mahira, Amiēļa dēla, namā, Lodabarā.
5 Basi Mfalme Daudi akamtaka aletwe kutoka Lo-Debari, kutoka nyumbani kwa Makiri mwana wa Amieli.
Tad ķēniņš Dāvids nosūtīja un to ņēma no Mahira, Amiēļa dēla, nama, no Lodabaras.
6 Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, alipofika kwa Daudi, akainama kumpa mfalme heshima. Daudi akamwita, “Mefiboshethi!” Mefiboshethi akajibu, “Ndimi mtumishi wako.”
Kad nu Mefibošets, Jonatāna dēls, Saula dēla dēls, pie Dāvida nāca tad viņš metās uz savu vaigu un klanījās. Un Dāvids sacīja: Mefibošet! Un viņš sacīja: redzi, še tavs kalps.
7 Daudi akamwambia, “Usiogope, kwa maana hakika nitakutendea wema kwa ajili ya baba yako Yonathani. Nitakurudishia ardhi yote iliyokuwa mali ya Sauli baba yako, nawe daima utakula chakula mezani pangu.”
Un Dāvids uz to sacīja: nebīsties, es tiešām tev parādīšu žēlastību tava tēva Jonatāna dēļ, un tev atdošu visus tava tēva Saula tīrumus, un tev būs vienmēr maizi ēst pie mana galda.
8 Mefiboshethi akasujudu akasema, “Mimi mtumishi wako ni nini hata uangalie mbwa mfu kama mimi?”
Un tas paklanījās un sacīja: kas tavs kalps tāds ir, ka tu uzlūko nomirušu suni, kāds es esmu?
9 Ndipo mfalme akamwita Siba mtumishi wa Sauli na kumwambia, “Nimempa mwana wa bwana wako kila kitu kilichokuwa mali ya Sauli na jamaa yake.
Tad ķēniņš aicināja Cību, Saula kalpu, un uz to sacīja: visu, kas Saulam un viņa namam piederēja, to es esmu devis tava kunga dēlam.
10 Wewe, wanao na watumishi wako mtamlimia mashamba Mefiboshethi na kumletea mavuno, ili kwamba mwana wa bwana wako apate mahitaji yake. Naye Mefiboshethi mwana wa bwana wako atakula chakula mezani pangu daima.” (Siba alikuwa na wana kumi na watano, na watumishi ishirini.)
Tāpēc strādā tu viņam to zemi, tu ar saviem dēliem un ar saviem kalpiem, un savāc, ka tava kunga dēlam ir maizes ko ēst, un Mefibošets, tava kunga dēls, lai vienmēr ēd maizi pie mana galda. Bet Cībum bija piecpadsmit dēli un divdesmit kalpi.
11 Ndipo Siba akamwambia mfalme, “Mtumishi wako atafanya chochote bwana wangu mfalme atakachoagiza mtumishi wake kufanya.” Basi Mefiboshethi akala chakula mezani pa Daudi kama mmoja wa wana wa mfalme.
Un Cībus sacīja uz ķēniņu: visu, ko mans kungs, tas ķēniņš, savam kalpam pavēl, to tavs kalps darīs. Un Mefibošets lai ēd pie mana galda tāpat, kā viens no ķēniņa bērniem.
12 Mefiboshethi alikuwa na mwanawe mdogo aliyeitwa Mika, nao watu wote wa nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi.
Un Mefibošetam bija mazs dēls, vārdā Miha, un visi, kas Cībus namā dzīvoja, tie Mefibošetam bija par kalpiem.
13 Naye Mefiboshethi akaishi huko Yerusalemu, kwa sababu daima alikula mezani pa mfalme, naye alikuwa kiwete miguu yote.
Un Mefibošets dzīvoja Jeruzālemē, tāpēc ka viņš vienmēr ēda pie ķēniņa galda. Un viņš bija tizls uz abām kājām.

< 2 Samweli 9 >