< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Or, il arriva après cela que [David battit les Philistins et les humilia; et David ôta le frein du tribut de la main des Philistins.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
Il battit aussi Moab et les mesura au cordeau, les faisant coucher par terre; or, il en mesura deux cordeaux, l’un pour les tuer, l’autre pour leur conserver la vie; et Moab fut assujetti à David lui payant tribut.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
De plus, David battit Adarézer, fils de Rohob, roi de Soba, quand il partit pour dominer sur le fleuve d’Euphrate.
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
Et David, après lui avoir pris mille sept cents cavaliers et vingt mille hommes de pied, coupa les nerfs des jambes à tous les chevaux des chariots; mais il en laissa pour cent chariots.
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Vint aussi la Syrie de Damas, pour porter secours à Adarézer, roi de Soba; et David tua vingt-deux mille hommes de la Syrie.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Et David mit une garnison dans la Syrie de Damas; et la Syrie devint tributaire de David; et le Seigneur conserva David dans tous les lieux où il alla.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Et David enleva les armes d’or qu’avaient les serviteurs d’Adarézer, et les porta à Jérusalem.
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
Et de Beté et de Béroth, villes d’Adarézer, le roi David enleva une très grande quantité d’airain.
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
Or, Thoü, roi d’Emath, apprit que David avait battu toutes les forces d’Adarézer;
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
Alors il envoya Joram son fils vers le roi David, pour le saluer, en le félicitant, et lui rendre grâce de ce qu’il avait vivement attaqué Adarézer, et l’avait battu; car Thoü était ennemi d’Adarézer; et dans la main de Joram étaient des vases d’or, des vases d’argent et des vases d’airain,
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
Que le roi David consacra aussi au Seigneur, avec l’argent et l’or qu’il avait consacrés de toutes les nations qu’il avait soumises,
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
De la Syrie, de Moab, des enfants d’Ammon, des Philistins, d’Amalec et des dépouilles d’Adarézer, fils de Rohob, roi de Soba.
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
David se fit encore un nom, lorsque, la Syrie prise, il fut revenu dans la vallée des Salines, où il tailla en pièces dix-huit mille hommes.
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
Et il mit des gardes dans l’Idumée, et il établit une garnison; et toute l’Idumée devint assujettie à David; et le Seigneur conserva David dans tous les lieux où il alla.
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Ainsi David régna sur tout Israël; il rendait aussi des jugements et la justice à tout son peuple.
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Mais Joab, fils de Sarvia, commandait l’armée, et Josaphat, fils d’Ahilud, tenait les registres;
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
Et Sadoc, fils d’Achitob, et Achimélech, fils d’Abiathar, étaient prêtres, et Saraïas, scribe;
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
Mais Banaïas, fils de Joïada, commandait les Céréthiens et les Phéléthiens; mais les fils de David étaient prêtres.

< 2 Samweli 8 >