< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Après cela David battit les Philistins et les abaissa; et David enleva Méthegamma des mains des Philistins.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
Il battit aussi les Moabites, et les mesura au cordeau, en les faisant coucher par terre; il en mesura deux cordeaux pour les faire mourir, et un plein cordeau pour leur laisser la vie; et les Moabites furent soumis à David et ses tributaires.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
David battit aussi Hadadézer, fils de Réhob, roi de Tsoba, comme il allait rétablir sa domination sur le fleuve de l'Euphrate.
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
Et David lui prit dix-sept cents cavaliers, et vingt mille hommes de pied; et il coupa les jarrets aux chevaux de tous les chars, mais il en réserva cent chars.
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Or les Syriens de Damas vinrent au secours de Hadadézer, roi de Tsoba; et David battit vingt-deux mille Syriens.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Puis David mit des garnisons dans la Syrie de Damas, et les Syriens furent soumis à David et ses tributaires. Et l'Éternel gardait David partout où il allait.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Et David prit les boucliers d'or qu'avaient les serviteurs de Hadadézer, et les apporta à Jérusalem.
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
Le roi David emporta aussi une très grande quantité d'airain de Bétach et de Bérothaï, villes de Hadadézer.
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
Or Thoï, roi de Hamath, apprit que David avait défait toutes les forces de Hadadézer.
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
Et il envoya Joram, son fils, vers le roi David, pour le saluer, et pour le bénir de ce qu'il avait fait la guerre contre Hadadézer et de ce qu'il l'avait défait. Car Hadadézer était continuellement en guerre avec Thoï. Et Joram apporta des vases d'argent, des vases d'or et des vases d'airain,
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
Que David consacra à l'Éternel, avec l'argent et l'or qu'il avait déjà consacrés, du butin de toutes les nations qu'il s'était assujetties,
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
De la Syrie, de Moab, des enfants d'Ammon, des Philistins, d'Amalek, et du butin de Hadadézer, fils de Réhob, roi de Tsoba.
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
David s'acquit encore du renom, à son retour de la défaite des Syriens, en battant, dans la vallée du Sel, dix-huit mille Iduméens,
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
Et il mit des garnisons dans l'Idumée; il mit des garnisons dans toute l'Idumée, et l'Idumée entière fut soumise à David. Et l'Éternel gardait David partout où il allait.
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Ainsi David régna sur tout Israël, faisant droit et justice à tout son peuple.
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Et Joab, fils de Tséruja, commandait l'armée; et Josaphat, fils d'Achilud, était archiviste;
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
Et Tsadok, fils d'Achitub, et Achimélec, fils d'Abiathar, étaient sacrificateurs, et Séraja, secrétaire;
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
Et Bénaja, fils de Jéhojada, était sur les Kéréthiens et les Péléthiens, et les fils de David étaient ses principaux officiers.

< 2 Samweli 8 >