< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Some time later, David’s army attacked the Philistia [army] and defeated them. They took control over the entire Philistia area.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
David’s army also defeated the army of the Moab people-group. David forced their soldiers to lie down on the ground [close to each other]. His men killed two out of every three of them. The [other] Moab people [were forced to] accept David as their ruler, and they were forced to give to him [every year the] payment/tax [that he demanded].
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
David’s army also defeated [the army of] Hadadezer, the son of Rehob, who ruled [the state of] Zobah [in Syria]. That happened when David went to rule again over the area at [the upper part of] the Euphrates River.
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
David’s army captured 1,700 of Hadadezer’s soldiers who rode on horses, and 20,000 of his other soldiers. They also crippled/hamstrung most of the horses that pulled the chariots, but they left/spared enough horses to [pull] 100 chariots.
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
When [the army of] Syria came from Damascus [city] to help King Hadadezer’s [army], David’s soldiers killed 22,000 of them.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Then David stationed (groups of his soldiers/army camps) in their area, and the people of Syria were forced to accept David as their ruler, and to give to David’s government [every year] the payment/tax that he demanded. And Yahweh enabled David’s [army] to win victories wherever they went.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
David’s soldiers took the gold shields that were carried by Hadadezer’s officials, and brought them to Jerusalem.
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
They also brought [to Jerusalem] a lot of bronze [that they found] in Betah and Berothai, two cities that King Hadadezer [had previously] ruled.
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
When Toi, the king of the Hamath [city in Syria], heard that David’s [army] had defeated the entire army of King Hadadezer,
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
he sent his son Joram to greet King David and to (congratulate him/say that he was happy) about his army defeating Hadadezer’s army, which Toi’s [army] had fought many times. Joram brought to David many items/gifts made from gold, silver, and bronze.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
King David dedicated all those items to Yahweh. He also dedicated the silver and gold which his army had taken from the nations that they had conquered.
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
They had taken items from the Edom people-group and the Moab people-group, from the Ammon people-group, from the Philistia people, and from [the descendants of] Amalek, as well as from the people that Hadadezer [previously] ruled.
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
When David returned [after defeating the armies of Syria], he became more famous because his army killed 18,000 soldiers from the Edom people-group in the Salt Valley [near the Dead Sea].
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
David stationed (groups of his soldiers/army camps) throughout the Edom area, and forced the people there to accept him as their king. Yahweh enabled David’s [army] to win battles wherever they went.
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
David ruled over all the Israeli people, and he always did for them what was fair and just.
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Joab was the army commander; Jehoshaphat, the son of Ahilud, was the man who reported to the people everything that David decided that they should do;
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
Zadok the son of Ahitub and Ahimelech the son of Abiathar were the priests; Seraiah was the official secretary;
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
Benaiah the son of Jehoiada was the commander of (David’s bodyguards/the men who protected the king); and David’s sons were priests (OR, his administrators/advisors).

< 2 Samweli 8 >