< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
and to be after so and to smite David [obj] Philistine and be humble them and to take: take David [obj] Metheg-ammah [the] Metheg-ammah from hand: power Philistine
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
and to smite [obj] Moab and to measure them in/on/with cord to lie down: lay down [obj] them land: soil [to] and to measure two cord to/for to die and fullness [the] cord to/for to live and to be Moab to/for David to/for servant/slave to lift: bear offering: tribute
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
and to smite David [obj] Hadadezer son: child Rehob king Zobah in/on/with to go: went he to/for to return: rescue hand: power his (in/on/with River Euphrates *Q(K)*)
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
and to capture David from him thousand and seven hundred horseman and twenty thousand man on foot and to hamstring David [obj] all [the] chariot and to remain from him hundred chariot
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
and to come (in): come Syria Damascus to/for to help to/for Hadadezer king Zobah and to smite David in/on/with Syria twenty and two thousand man
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
and to set: put David garrison in/on/with Syria Damascus and to be Syria to/for David to/for servant/slave to lift: bear offering: tribute and to save LORD [obj] David in/on/with all which to go: went
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
and to take: take David [obj] shield [the] gold which to be to(wards) servant/slave Hadadezer and to come (in): bring them Jerusalem
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
and from Betah and from Berothai city Hadadezer to take: take [the] king David bronze to multiply much
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
and to hear: hear Toi king Hamath for to smite David [obj] all strength: soldiers Hadadezer
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
and to send: depart Toi [obj] Joram son: child his to(wards) [the] king David to/for to ask to/for him to/for peace: well-being and to/for to bless him upon which to fight in/on/with Hadadezer and to smite him for man battle Toi to be Hadadezer and in/on/with hand: to his to be article/utensil silver: money and article/utensil gold and article/utensil bronze
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
also [obj] them to consecrate: dedicate [the] king David to/for LORD with [the] silver: money and [the] gold which to consecrate: dedicate from all [the] nation which to subdue
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
from Edom and from Moab and from son: descendant/people Ammon and from Philistine and from Amalek and from spoil Hadadezer son: child Rehob king Zobah
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
and to make David name in/on/with to return: return he from to smite he [obj] Edom in/on/with (Salt) Valley (Valley of) Salt eight ten thousand
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
and to set: put in/on/with Edom garrison in/on/with all Edom to set: put garrison and to be all Edom servant/slave to/for David and to save LORD [obj] David in/on/with all which to go: went
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
and to reign David upon all Israel and to be David to make: do justice and righteousness to/for all people his
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
and Joab son: child Zeruiah upon [the] army and Jehoshaphat son: child Ahilud to remember
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
and Zadok son: child Ahitub and Ahimelech son: child Abiathar priest and Seraiah secretary
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
and Benaiah son: child Jehoiada and [the] Cherethite and [the] Pelethite and son: child David priest to be

< 2 Samweli 8 >