< 2 Samweli 8 >

1 Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
Nogen Tid efter slog David Filisterne og undertvang dem, og David fratog Filisterne Meteg-Ha'amma.
2 Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
Fremdeles slog han Moabiterne, og han maalte dem med en Snor, idet han lod dem lægge sig ned paa Jorden og afmaalte to Snorlængder, der skulde dræbes, og een, der skulde blive i Live. Saaledes blev Moabiterne Davids skatskyldige Undersaatter.
3 Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
Ligeledes slog David Rehobs Søn, Kong Hadad'ezer af Zoba, da han var draget ud for at genoprette sit Herredømme ved Floden.
4 Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
David fratog ham 1700 Ryttere og 20 000 Mand Fodfolk og lod alle Stridshestene lamme paa hundrede nær, som han skaanede.
5 Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
Og da Aramæerne fra Damaskus kom Hadad'ezer af Zoba til Hjælp, slog David 22 000 Mand af Aramæerne.
6 Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
Derpaa indsatte David Fogeder i det damaskenske Aram, og Aramæerne blev Davids skatskyldige Undersaatter. Saaledes, gav HERREN David Sejr, overalt hvor han drog frem.
7 Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
Og David tog de Guldskjolde, Hadad'ezers Folk havde baaret, og bragte dem til Jerusalem;
8 Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
og fra Hadad'ezers Byer Teba og Berotaj bortførte Kong David Kobber i store Mængder.
9 Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
Men da Kong To'i af Hamat hørte, at David havde slaaet hele Hadad'ezers Stridsmagt,
10 akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
sendte han sin Søn Hadoram til Kong David for at hilse paa ham og lykønske ham til, at han havde kæmpet med Hadad'ezer og slaaet ham — Hadad'ezer havde nemlig ligget i Krig med To'i — og han medbragte Sølv-, Guld— og Kobber-sager.
11 Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
Ogsaa dem helligede Kong David HERREN tillige med det Sølv og Guld, han havde helliget af Byttet fra alle de undertvungne Folk,
12 yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
Edom, Moab Ammoniterne, Filisterne, Amalek, og af det Bytte, han havde taget fra Rehobs Søn, Kong Hadad'ezer af Zoba.
13 Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
Og David vandt sig et Navn. Da han vendte tilbage fra Sejren over Aram, slog han Edom i Saltdalen, 18 000 Mand;
14 Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
derpaa indsatte han Fogeder i Edom; i hele Edom indsatte han Fogeder, og alle Edomiterne blev Davids Undersaatter, Saaledes gav HERREN David Sejr, overalt hvor han drog frem.
15 Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
Og David var Konge over hele Israel, og han øvede Ret og Retfærdighed mod hele sit Folk.
16 Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
Joab, Zerujas Søn, var sat over Hæren; Josjafat, Ahiluds Søn, var Kansler;
17 Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
Zadok, Abitubs Søn, og Ebjatar, Ahimeleks Søn, var Præster; Seraja var Statsskriver;
18 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.
Benaja, Jojadas Søn, var sat over Kreterne og Pleterne, og Davids Sønner var Præster.

< 2 Samweli 8 >