< 2 Samweli 7 >

1 Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
Lorsque le roi habitait dans sa maison et que Yahvé lui avait accordé du repos contre tous ses ennemis de tous les côtés,
2 akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
le roi dit à Nathan, le prophète: « Voici, j'habite dans une maison de cèdre, mais l'arche de Dieu habite dans des courtines. »
3 Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
Nathan dit au roi: « Va, fais tout ce que tu as dans le cœur, car Yahvé est avec toi. »
4 Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
Cette même nuit, la parole de Yahvé fut adressée à Nathan, en ces termes:
5 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
Va dire à mon serviteur David: « Yahvé dit: Veux-tu me construire une maison pour que j'y habite?
6 Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
Car je n'ai pas habité dans une maison depuis le jour où j'ai fait monter les enfants d'Israël hors d'Égypte, jusqu'à ce jour, mais je me suis déplacé dans une tente et dans un tabernacle.
7 Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
Dans tous les lieux où j'ai marché avec tous les enfants d'Israël, j'ai dit à quelqu'un des tribus d'Israël à qui j'avais ordonné d'être le berger de mon peuple d'Israël: « Pourquoi ne m'avez-vous pas bâti une maison de cèdre? ».
8 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
Maintenant, dites ceci à mon serviteur David: Yahvé des armées dit: « Je t'ai pris de la bergerie, de la suite des brebis, pour être prince sur mon peuple, sur Israël.
9 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
J'ai été avec toi partout où tu es allé, et j'ai exterminé tous tes ennemis devant toi. Je te ferai un grand nom, comme le nom des grands qui sont sur la terre.
10 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
J'établirai un lieu pour mon peuple d'Israël, et je le planterai, afin qu'il habite dans son lieu et ne soit plus déplacé. Les enfants du mal ne les affligeront plus, comme au début,
11 na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
et comme depuis le jour où j'ai ordonné à des juges d'être à la tête de mon peuple d'Israël. Je vous ferai reposer de tous vos ennemis. De plus, Yahvé te dit que Yahvé te fera une maison.
12 Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
Lorsque tes jours seront accomplis et que tu te coucheras avec tes pères, j'établirai ta descendance après toi, qui sortira de ton corps, et j'établirai son règne.
13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
Il bâtira une maison à mon nom, et j'établirai pour toujours le trône de son royaume.
14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
Je serai son père, et il sera mon fils. S'il commet l'iniquité, je le châtierai avec la verge des hommes et avec les coups des enfants des hommes;
15 Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
mais ma bonté ne se retirera pas de lui, comme je l'ai fait pour Saül, que j'ai rejeté devant toi.
16 Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
Ta maison et ton royaume seront assurés pour toujours devant toi. Ton trône sera affermi pour toujours. »'"
17 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
Nathan adressa à David toutes ces paroles, et selon toute cette vision.
18 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Alors le roi David entra et s'assit devant l'Éternel; et il dit: Qui suis-je, Seigneur Éternel, et quelle est ma maison, pour que tu m'aies conduit jusqu'ici?
19 Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
C'était encore peu de chose à tes yeux, Seigneur Éternel, mais tu as parlé de la maison de ton serviteur pour un temps encore long, et cela parmi les hommes, Seigneur Éternel!
20 “Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
Que peut encore te dire David? Car tu connais ton serviteur, Seigneur Yahvé.
21 Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
C'est à cause de ta parole, et selon ton propre cœur, que tu as fait toute cette grandeur, pour la faire connaître à ton serviteur.
22 “Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
C'est pourquoi tu es grand, Yahvé Dieu. Car il n'y a personne comme toi, et il n'y a pas d'autre Dieu que toi, d'après tout ce que nous avons entendu de nos oreilles.
23 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
Quelle nation sur la terre est semblable à ton peuple, à Israël, que Dieu est allé racheter pour en faire un peuple, et pour se faire un nom, et pour faire de grandes choses pour toi, et des choses redoutables pour ton pays, devant ton peuple, que tu as racheté pour toi hors d'Égypte, d'entre les nations et leurs dieux?
24 Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
Tu as établi pour toi ton peuple Israël, pour qu'il soit ton peuple à jamais; et toi, Yahvé, tu es devenu son Dieu.
25 “Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
« Maintenant, Yahvé Dieu, la parole que tu as prononcée sur ton serviteur et sur sa maison, confirme-la à jamais, et fais ce que tu as dit.
26 ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
Que ton nom soit à jamais glorifié, en disant: L'Éternel des armées est Dieu sur Israël, et la maison de ton serviteur David sera affermie devant toi.
27 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
Car toi, Éternel des armées, Dieu d'Israël, tu as révélé à ton serviteur: Je te bâtirai une maison. C'est pourquoi ton serviteur a trouvé dans son cœur de t'adresser cette prière.
28 Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
« Maintenant, Seigneur Yahvé, tu es Dieu, et tes paroles sont vérité, et tu as promis ce bien à ton serviteur.
29 Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”
Maintenant donc, qu'il te plaise de bénir la maison de ton serviteur, afin qu'elle subsiste à jamais devant toi, car c'est toi, Seigneur Yahvé, qui l'as dit. Que la maison de ton serviteur soit bénie à jamais par ta bénédiction. »

< 2 Samweli 7 >