< 2 Samweli 7 >

1 Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
Forsothe it was doon, whanne the kyng Dauid hadde sete in his hows, and the Lord hadde youe reste to hym on ech side fro alle hise enemyes,
2 akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
he seyde to Nathan the prophete, Seest thou not, that Y dwelle in an hows of cedre, and the arke of God is put in the myddis of skynnys?
3 Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
And Nathan seide to the kyng, Go thou, and do al thing which is in thin herte, for the Lord is with thee.
4 Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
Forsothe it was don in that niyt, and lo! the word of the Lord, seiynge to Nathan, Go thou,
5 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
and speke to my servaunt Dauid, The Lord seith these thingis, Whether thou schalt bilde to me an hows to dwelle ynne?
6 Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
For Y `dwellide not in an hows fro the dai in which Y ledde the sones of Israel out of the lond of Egipt til in to this dai; but Y yede in tabernacle and in tent,
7 Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
bi alle places, to whiche Y passyde with alle the sones of Israel? Whether Y spekynge spak to oon of the lynagis of Israel, to whom Y comaundyde, that he schulde feede my puple Israel, and seide, Whi `bildidist thou not an hows of cedre to me?
8 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
And now thou schalt seie these thingis to my seruaunt Dauid, The Lord of oostis seith these thingis, Y took thee fro lesewis suynge flockis, that thou schuldist be duyk on my puple Israel, and Y was with thee in alle thingis,
9 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
where euere thou yedist, and Y killide alle thin enemyes fro thi face, and Y made to thee a greet name bi the name of grete men that ben in erthe;
10 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
and Y schall sette a place to my puple Israel, and Y schal plaunte hym, and Y schal dwelle with hym, and he schal no more be troblid, and the sones of wickidnesse schulen not adde, that thei turmente hym as bifor,
11 na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
fro the dai in which Y ordenede iugis on my puple Israel; and Y schal yyue reste to thee fro alle thin enemyes. And the Lord biforseith to thee, that `the Lord schal mak an hows to thee;
12 Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
and whanne thi daies be fillid, and thou hast slept with thi fadris, Y schal reyse thi seed aftir thee, which schal go out of thi wombe, and Y schal make `stidfast his rewme.
13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
He schal bilde an hows to my name, and Y schal make stable the troone of his rewme til in to with outen ende;
14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
Y schal be to hym in to fadir, and he schal be to me in to a sone; and if he schal do ony thing wickidli, Y schal chastise hym in the yerde of men, and in the woundis of the sones of men.
15 Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
Forsothe Y schal not do awey my mercy fro hym, as Y dide awei fro Saul, whom Y remouede fro my face.
16 Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
And thin hows schal be feithful, and thi rewme schal be til in to with outen ende bifor my face, and thi trone schal be stidfast contynueli.
17 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
By alle these wordys, and bi al this reuelacioun, so Nathan spak to Dauid.
18 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Forsothe Dauid the kyng entride, and satt bifor the Lord, and seide, Who am Y, my Lord God, and what is myn hows, that thou brouytist me hidur to?
19 Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
But also this is seyn litil in thi siyt, my Lord God; no but thou schuldist speke also of the hows of thi seruaunt in to long tyme. Forsothe this is the lawe of Adam, Lord God;
20 “Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
what therfor may Dauid adde yit, that he speke to thee? For thou, Lord God, knowist thi seruaunt; thou hast do alle these grete thingis,
21 Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
for thi word, and bi thin herte, so that thou madist knowun to thi seruaunt.
22 “Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
Herfor, Lord God, thou art magnyfied, for noon is lijk thee, ne there is no God outakun thee, in alle thingis whiche we herden with oure eeris.
23 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
Sotheli what folk in erthe is as the puple of Israel, for which the Lord God yede, that he schulde ayenbie it to him in to a puple, and schulde sette to hym silf a name, and schulde do to it grete thingis, and orible on erthe, in castinge out therof the folk and `goddis therof fro the face of thi puple, which thou `ayen bouytist to thee fro Egipt?
24 Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
And thou confermidist to thee thi puple Israel in to a puple euerlastynge, and thou, Lord, art maad in to God to hem.
25 “Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
Now therfor, Lord God, reise thou withouten ende the word that thou hast spoke on thi seruaunt and on his hows, and do as thou hast spoke;
26 ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
and thy name be magnyfied til in to withouten ende, and be it seid, The Lord of oostis is God on Israel; and the hows of thi seruaunt Dauid schal be stablischid byfor the Lord;
27 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
for thou, Lord of oostis, God of Israel, hast maad reuelacioun to the eere of thi seruaunt, and seidist, Y schal bilde an hows to thee; therfor thi seruaunt foond his herte, that he schulde preie thee bi this preier.
28 Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
Now therfor, Lord God, thou art veri God, and thi wordis schulen be trewe; for thou hast spoke these goodis to thi seruaunt;
29 Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”
therfor bigynne thou, and blesse the hows of thi seruaunt, that it be withouten ende bifor thee; for thou, Lord God, hast spoke these thingis, and bi thi blessyng the hows of thi seruaunt schal be blessid withouten ende.

< 2 Samweli 7 >