< 2 Samweli 7 >

1 Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
And it came to pass, when the king sat in his house, and the LORD had given him rest around from all his enemies;
2 akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
That the king said to Nathan the prophet, See now, I dwell in a house of cedar, but the ark of God dwelleth within curtains.
3 Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
And Nathan said to the king, Go, do all that [is] in thy heart: for the LORD [is] with thee.
4 Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
And it came to pass that night, that the word of the LORD came to Nathan, saying,
5 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
Go and tell my servant David, Thus saith the LORD, Wilt thou build me a house for me to dwell in?
6 Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
Whereas I have not dwelt in [any] house since the time that I brought the children of Israel out of Egypt, even to this day, but have walked in a tent, and in a tabernacle.
7 Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
In all [the places] in which I have walked with all the children of Israel have I spoken a word with any of the tribes of Israel, whom I commanded to feed my people Israel, saying, Why do ye not build me a house of cedar?
8 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
Now therefore so shalt thou say to my servant David, thus saith the LORD of hosts, I took thee from the sheep-cote, from following the sheep, to be ruler over my people, over Israel:
9 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
And I was with thee whithersoever thou wentest, and have cut off all thy enemies out of thy sight, and have made thee a great name, like to the name of the great [men] that [are] in the earth.
10 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
Moreover, I will appoint a place for my people Israel, and will plant them, that they may dwell in a place of their own, and move no more; neither shall the children of wickedness afflict them any more, as formerly.
11 na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
And as since the time that I commanded judges [to be] over my people Israel, and have caused thee to rest from all thy enemies. Also the LORD telleth thee that he will make thee a house.
12 Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
And when thy days shall be fulfilled, and thou shalt sleep with thy fathers, I will set up thy seed after thee, which shall proceed out of thy bowels, and I will establish his kingdom.
13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
He shall build a house for my name, and I will establish the throne of his kingdom for ever.
14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
I will be his father, and he shall be my son. If he shall commit iniquity, I will chasten him with the rod of men, and with the stripes of the children of men:
15 Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
But my mercy shall not depart from him, as I took [it] from Saul, whom I put away before thee.
16 Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
And thy house and thy kingdom shall be established for ever before thee: thy throne shall be established for ever.
17 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
According to all these words, and according to all this vision, so did Nathan speak to David.
18 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Then king David went in, and sat before the LORD, and he said, Who [am] I, O LORD God? and what [is] my house, that thou hast brought me hitherto;
19 Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
And this was yet a small thing in thy sight, O LORD God; but thou hast spoken also of thy servant's house for a great while to come. And [is] this the manner of man, O LORD God?
20 “Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
And what can David say more to thee? for thou, LORD God, knowest thy servant.
21 Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
For thy word's sake, and according to thy own heart, hast thou done all these great things, to make thy servant know [them].
22 “Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
Wherefore thou art great, O LORD God: for [there is] none like thee, neither [is there any] God besides thee, according to all that we have heard with our ears.
23 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
And what one nation in the earth [is] like thy people, [even] like Israel, whom God went to redeem for a people to himself, and to make him a name, and to do for you great things and terrible, for thy land, before thy people which thou redeemedst to thee from Egypt, [from] the nations and their gods?
24 Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
For thou hast confirmed to thyself thy people Israel [to be] a people to thee for ever: and thou, LORD, art become their God.
25 “Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
And now, O LORD God, the word that thou hast spoken concerning thy servant, and concerning his house, establish [it] for ever, and do as thou hast said.
26 ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
And let thy name be magnified for ever, saying, The LORD of hosts [is] the God over Israel: and let the house of thy servant David be established before thee.
27 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
For thou, O LORD of hosts, God of Israel, hast revealed to thy servant, saying, I will build thee a house: therefore hath thy servant found in his heart to pray this prayer to thee.
28 Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
And now, O LORD God, thou [art] that God, and thy words are true, and thou hast promised this goodness to thy servant:
29 Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”
Therefore now let it please thee to bless the house of thy servant, that it may continue for ever before thee: for thou, O LORD God, hast spoken [it]: and with thy blessing let the house of thy servant be blessed for ever.

< 2 Samweli 7 >