< 2 Samweli 7 >

1 Baada ya mfalme kuingia rasmi katika jumba lake la kifalme, naye Bwana akiwa amemstarehesha pande zote mbali na adui zake,
And it came to pass, when the king dwelt in his house, and the LORD had given him rest from all his enemies round about,
2 akamwambia nabii Nathani, “Mimi hapa, ninaishi katika jumba la kifalme la mierezi, wakati Sanduku la Mungu limebaki katika hema.”
that the king said unto Nathan the prophet: 'See now, I dwell in a house of cedar, but the ark of God dwelleth within curtains.'
3 Nathani akamjibu mfalme, “Lolote ulilo nalo moyoni, endelea ukalifanye, kwa maana Bwana yu pamoja nawe.”
And Nathan said to the king: 'Go, do all that is in thy heart; for the LORD is with thee.'
4 Usiku ule neno la Bwana likamjia Nathani, kusema:
And it came to pass the same night, that the word of the LORD came unto Nathan, saying:
5 “Nenda ukamwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana: Je, ewe ndiwe wa kunijengea mimi nyumba ili nikae ndani yake?
'Go and tell My servant David: Thus saith the LORD: Shalt thou build Me a house for Me to dwell in?
6 Sijakaa ndani ya nyumba tangu siku niliyowaleta Waisraeli kutoka Misri hadi leo. Nimekuwa nikitembea kutoka mahali pamoja hadi mahali pengine ndani ya hema kama makao yangu.
for I have not dwelt in a house since the day that I brought up the children of Israel out of Egypt, even to this day, but have walked in a tent and in a tabernacle.
7 Popote nilipotembea pamoja na Waisraeli wote, je, nimewahi kumwambia kiongozi wao yeyote niliyemwamuru kuwachunga watu wangu Israeli, “Kwa nini hujanijengea nyumba ya mierezi?”’
In all places wherein I have walked among all the children of Israel, spoke I a word with any of the tribes of Israel, whom I commanded to feed My people Israel, saying: Why have ye not built Me a house of cedar?
8 “Sasa basi, mwambie mtumishi wangu Daudi, ‘Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: Nilikutoa wewe kutoka machungani na kutoka kuandama kundi la kondoo na mbuzi ili kuwaongoza watu wangu Israeli.
Now therefore thus shalt thou say unto My servant David: Thus saith the LORD of hosts: I took thee from the sheepcote, from following the sheep, that thou shouldest be prince over My people, over Israel.
9 Nimekuwa pamoja nawe popote ulipokwenda, nami nimekuondolea mbali adui zako wote mbele yako. Basi nitalifanya jina lako kuwa kuu kama majina ya watu walio wakuu sana duniani.
And I have been with thee whithersoever thou didst go, and have cut off all thine enemies from before thee; and I will make thee a great name, like unto the name of the great ones that are in the earth.
10 Nami nitawapatia watu wangu Israeli mahali niwapande humo ili kwamba wawe na nyumbani kwao wenyewe wasisumbuliwe tena. Watu waovu hawatawaonea tena, kama walivyofanya mwanzoni,
And I will appoint a place for My people Israel, and will plant them, that they may dwell in their own place, and be disquieted no more; neither shall the children of wickedness afflict them any more, as at the first,
11 na kama walivyofanya tangu mwanzo wakati nilipowaweka viongozi juu ya watu wangu Israeli. Pia nitawapa raha mbele ya adui zenu wote. “‘Bwana akuambia kwamba Bwana mwenyewe atakujengea nyumba.
even from the day that I commanded judges to be over My people Israel; and I will cause thee to rest from all thine enemies. Moreover the LORD telleth thee that the LORD will make thee a house.
12 Siku zako zitakapokwisha nawe ulale pamoja na baba zako, nitainua mzao wako aingie mahali pako, ambaye atatoka viunoni mwako, nami nitauimarisha ufalme wake.
When thy days are fulfilled, and thou shalt sleep with thy fathers, I will set up thy seed after thee, that shall proceed out of thy body, and I will establish his kingdom.
13 Yeye ndiye atakayejenga nyumba kwa ajili ya Jina langu, nami nitaimarisha kiti cha enzi cha ufalme wake milele.
He shall build a house for My name, and I will establish the throne of his kingdom for ever.
14 Nitakuwa baba yake, naye atakuwa mwanangu. Atakapokosea nitamwadhibu kwa fimbo ya wanadamu, kwa adhabu ya kupigwa na wanadamu.
I will be to him for a father, and he shall be to Me for a son; if he commit iniquity, I will chasten him with the rod of men, and with the stripes of the children of men;
15 Lakini upendo wangu kamwe hautaondolewa kwake, kama nilivyouondoa kwa Sauli, niliyemwondoa atoke mbele yako.
but My mercy shall not depart from him, as I took it from Saul, whom I put away before thee.
16 Nyumba yako na ufalme wako utadumu milele mbele zangu, kiti chako cha enzi kitafanywa imara milele.’”
And thy house and thy kingdom shall be made sure for ever before thee; thy throne shall be established for ever.'
17 Nathani akamwarifu Daudi maneno yote ya maono haya.
According to all these words, and according to all this vision, so did Nathan speak unto David.
18 Ndipo Mfalme Daudi akaingia ndani, akaketi mbele za Bwana, akasema: “Ee Bwana Mwenyezi, mimi ni nani, na jamaa yangu ni nini, hata umenileta mpaka hapa nilipo?
Then David the king went in, and sat before the LORD; and he said: 'Who am I, O Lord GOD, and what is my house, that Thou hast brought me thus far?
19 Naam, kana kwamba hili halitoshi machoni pako, Ee Bwana Mwenyezi, wewe umenena pia kuhusu siku zijazo za nyumba ya mtumishi wako. Je, hii ndiyo njia yako ya kawaida ya kushughulika na mwanadamu, Ee Bwana Mwenyezi?
And this was yet a small thing in Thine eyes, O Lord GOD; but Thou hast spoken also of Thy servant's house for a great while to come; and this too after the manner of great men, O Lord GOD.
20 “Je, Daudi aweza kukuambia nini zaidi? Kwa maana unamjua mtumishi wako, Ee Bwana Mwenyezi.
And what can David say more unto Thee? for Thou knowest Thy servant, O Lord GOD.
21 Kwa ajili ya neno lako na kwa mapenzi yako, umefanya jambo hili kubwa na kulifanya lijulikane na lifahamike kwa mtumishi wako.
For Thy word's sake, and according to Thine own heart, hast Thou wrought all this greatness, to make Thy servant know it.
22 “Tazama jinsi ulivyo mkuu, Ee Bwana Mwenyezi! Hakuna mwingine kama wewe, wala hakuna Mungu ila wewe, kama vile tulivyosikia kwa masikio yetu wenyewe,
Therefore Thou art great, O LORD God; for there is none like Thee, neither is there any God beside Thee, according to all that we have heard with our ears.
23 Naye ni nani aliye kama watu wako Israeli, taifa pekee duniani ambalo Mungu alitoka kwenda kulikomboa kwa ajili yake mwenyewe, na kujifanyia jina mwenyewe, kwa kufanya maajabu makubwa na ya kutisha kwa kuwafukuza mataifa na miungu yao mbele ya watu wako, ambao uliwakomboa kutoka Misri?
And who is like Thy people, like Israel, a nation one in the earth, whom God went to redeem unto Himself for a people, and to make Him a name, and to do for Thy land great things and tremendous, even for you, in driving out from before Thy people, whom Thou didst redeem to Thee out of Egypt, the nations and their gods?
24 Umeimarisha watu wako Israeli hasa kama watu wako mwenyewe milele, nawe, Ee Bwana, umekuwa Mungu wao.
And Thou didst establish to Thyself Thy people Israel to be a people unto Thee for ever; and Thou, LORD, becamest their God.
25 “Basi sasa, Bwana, ukaitimize ahadi uliyosema kuhusu mtumishi wako na nyumba yake milele. Fanya kama ulivyoahidi,
And now, O LORD God, the word that Thou hast spoken concerning Thy servant, and concerning his house, confirm Thou it for ever, and do as Thou hast spoken.
26 ili kwamba jina lako litukuke milele. Ndipo watu watasema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ni Mungu juu ya Israeli!’ Nayo nyumba ya mtumishi wako Daudi itakuwa imara mbele zako.
And let Thy name be magnified for ever, that it may be said: The LORD of hosts is God over Israel; and the house of Thy servant David shall be established before Thee.
27 “Ee Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wa Israeli, umelifunua hili kwa mtumishi wako, ukisema, ‘Nitakujengea nyumba.’ Hivyo mtumishi wako amepata ujasiri kukuletea dua hii.
For Thou, O LORD of hosts, the God of Israel, hast revealed to Thy servant, saying: I will build thee a house; therefore hath Thy servant taken heart to pray this prayer unto Thee.
28 Ee Bwana Mwenyezi, wewe ndiwe Mungu! Maneno yako ndiyo kweli, nawe umemwahidi mtumishi wako mambo haya mazuri.
And now, O Lord GOD, Thou alone art God, and Thy words are truth, and Thou hast promised this good thing unto Thy servant;
29 Sasa naomba uwe radhi kuibariki nyumba ya mtumishi wako, ili idumu mbele zako milele, kwa maana wewe, Ee Bwana Mwenyezi, umesema, na kwa baraka zako nyumba ya mtumishi wako itaendelea kubarikiwa milele.”
now therefore let it please Thee to bless the house of Thy servant, that it may continue for ever before Thee; for Thou, O Lord GOD, hast spoken it; and through Thy blessing let the house of Thy servant be blessed for ever.'

< 2 Samweli 7 >