< 2 Samweli 6 >

1 Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
Davudee İzrailyğançe meer yugna, siyxənə xhebts'al aazır insan g'əyxı', saa'a.
2 Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
Davud, Yahudeene Ba'ala eyhene şahareençe Allahna q'utye qavaalesva, cune insanaaşika sacige maqa ayk'an. Mana q'utye Rəbbine doyul vuxha. Mane q'utyel oo keruvar ıxha. Xəəne G'oşunbışde Rəbbina taxt mane keruvaaşil oo vuxha.
3 Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
Allahna q'utye ts'enne daşk'eeqa alivxhu, Avinadavne tepalyne xaançe qığaahana. Daşk'ad Avinadavne dixbışe Uzzayeeyiy Axioyee he'ekka ıxha.
4 likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
Manbışe Allahna q'utye daşk'eeqa gyuvxhu qığaaha. Q'utyeyne ögiylir Axio ayk'an.
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
Davudur, gırgın İzrailin milletıd gıranne osake hı'iyn t'ampırbı, lirabı, dafbı, medın aalyatbı əlixı', Rəbbine ögil şadba mık'ar hı'ı.
6 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
Naxonne attayle ı'lğəəmee, yatsbı qaçayxaranbı. Uzzeeyib xıl hotku, g'ı'moxhacenva Allahna q'utye avqaaqqa.
7 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
Rəbbina Uzzalqa qəl avqaaqqa, mang'vee hı'rmat deşvaala hav'uva mana maacar ı'xı' gek'ana. Uzza Allahne q'utyeyne k'ane qek'a.
8 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
Davudus, Rəbbee Uzza gik'uva qəl vooxhe. Mane cigayn do g'iyniyne yiğılid Perets-Uzza (Uzzayn qik'uy) vod.
9 Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
Mane yiğıl Davud Rəbbile qərq'ı'n, eyhen: – Zasqa Rəbbina q'utye nəxüb ables vooxheye?
10 Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
Davudus Rəbbina q'utye cusqa, Davudne Şahareeqa quvkees vukkiykan deş. Mang'vee mana Gatğançene Oved-Edomne xaaqa quvkees ulyookka.
11 Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
Rəbbina q'utye xheyible vazna Oved-Edomne xaa aaxva. Rəbbee Oved-Edomusub, mang'une xizanısıb yugna barakat hoole.
12 Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
Paççah Davudulqa «Rəbbee Oved-Edomne xizanıb, mang'une gırgıne karasıb Allahne q'utyel-alla barakat huvuva» hixhar ha'a. Manke Davud Oved-Edomne xaaqa hark'ın, mançe Allahna q'utye cun do huvuyne Davudne şahareeqa şadba qavayle.
13 Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
Rəbbina q'utye haaqqanbışe yixhnəqqees g'el qittumee, Davudee sa yats'iy tavulyna q'ıka gyook'a.
14 Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
Davudee katanıken ileylığ ali'ı, Rəbbine ögil vəəxəxüb g'oyk'al-ulyoyk'al mık' haa'a.
15 wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
Davuduka sacigee gırgıne İzrailyne milletın şadvalin ts'irbı ha'a-ha'a, şeypur ı'lyviyxə Rəbbina q'utye quvkeeka vuxha.
16 Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
Rəbbina q'utye Davudne Şahareeqa quvkekkamee, Şaulna yiş Mikal g'uleençe ileeka yixha. Məng'ı'k'le paççah Davudee Rəbbine ögil g'oyk'al-ulyoyk'al mık' haa'a g'avcumee, məng'ee mana k'ap'ik'ıle avqa qa'a.
17 Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
Rəbbina q'utye qabı, Davudee mançinemee g'üvxüyne çadrene ab, çisva qav'uyne cigeeqa giviyxhe. Davudee Rəbbine ögil gyoxhxhan ha'aniy medın q'urbanbı allya'a.
18 Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
Davudee q'urbanbı alli'iyle qiyğa, milletıs, Xəəne G'oşunbışde Rəbbine doyule xayir-düə hoole.
19 Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
Qiyğa mang'vee İzrailyne milletne adameeşisıb, yadaaşisıb gırgıng'uscab sa gıney, sık'ınin çuru, sa ts'ets'ib qooqqune t'ımılena hoole. Mançeb gırgınbı xaybışeeqa siviyk'al.
20 Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
Davud cune xaabınbışis xayir-düə hevlesva xaaqa sak'ımee, Şaulna yiş Mikal mang'une ögilqa qığeyç'u, eyhen: – İzrailyne paççahee g'iyna vuceecar-vuc nəxür haguna! Mana cune insanaaşineyiy cune g'ulluxçiy içeeşine ögil bəç'ər xhinne ts'ele qıxha.
21 Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
Davudee Mikalık'le eyhen: – Zı man Rəbbine ögil hı'ı. Mang'vee zı yiğne dekkıneyiy mang'une bıkırne nasılene cigee g'əyxı', Cune milletıs, İzrailybışis, xərna hı'ı. Zı inçile qiyğar Rəbbine ögil şadxhesda.
22 Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
Zı yizde ulene ögil sık'ırar uleke g'a'ayxhasda. Ğu eyhene g'ulluxçiy içeeşemee zı axtı qa'as.
23 Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.
Şaulne yişşeqa, Mikalıqa, qiyk'asde yiğılqamee uşax eyxhe deş.

< 2 Samweli 6 >