< 2 Samweli 6 >
1 Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
and to gather still David [obj] all to choose in/on/with Israel thirty thousand
2 Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
and to arise: rise and to go: went David and all [the] people which with him from Baalah (Baalah of)Judah to/for to ascend: establish from there [obj] ark [the] God which to call: call by name name LORD Hosts to dwell [the] cherub upon him
3 Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
and to ride [obj] ark [the] God to(wards) cart new and to lift: bear him from house: household Abinadab which in/on/with hill and Uzzah and Ahio son: child Abinadab to lead [obj] [the] cart new
4 likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
and to lift: bear him from house: household Abinadab which in/on/with hill with ark [the] God and Ahio to go: went to/for face: before [the] ark
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
and David and all house: household Israel to laugh to/for face: before LORD in/on/with all tree: wood cypress and in/on/with lyre and in/on/with harp and in/on/with tambourine and in/on/with castanets and in/on/with banging
6 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
and to come (in): come till threshing floor Nacon and to send: depart Uzzah to(wards) ark [the] God and to grasp in/on/with him for to release [the] cattle
7 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
and to be incensed face: anger LORD in/on/with Uzzah and to smite him there [the] God upon [the] irreverence and to die there with ark [the] God
8 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
and to be incensed to/for David upon which to break through LORD breach in/on/with Uzzah and to call: call by to/for place [the] he/she/it Perez-uzzah Perez-uzzah till [the] day: today [the] this
9 Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
and to fear David [obj] LORD in/on/with day [the] he/she/it and to say how? to come (in): come to(wards) me ark LORD
10 Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
and not be willing David to/for to turn aside: remove to(wards) him [obj] ark LORD upon city David and to stretch him David house: home Obed-edom Obed-edom [the] Gittite
11 Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
and to dwell ark LORD house: home Obed-edom Obed-edom [the] Gittite three month and to bless LORD [obj] Obed-edom Obed-edom and [obj] all house: household his
12 Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
and to tell to/for king David to/for to say to bless LORD [obj] house: home Obed-edom Obed-edom and [obj] all which to/for him in/on/with for the sake of ark [the] God and to go: went David and to ascend: establish [obj] ark [the] God from house: home Obed-edom Obed-edom city David in/on/with joy
13 Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
and to be for to march to lift: bear ark LORD six step and to sacrifice cattle and fatling
14 Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
and David to dance in/on/with all strength to/for face: before LORD and David to gird ephod linen
15 wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
and David and all house: household Israel to ascend: establish [obj] ark LORD in/on/with shout and in/on/with voice: sound trumpet
16 Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
and to be ark LORD to come (in): come city David and Michal daughter Saul to look about/through/for [the] window and to see: see [obj] [the] king David be agile and to dance to/for face: before LORD and to despise to/for him in/on/with heart her
17 Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
and to come (in): bring [obj] ark LORD and to set [obj] him in/on/with place his in/on/with midst [the] tent which to stretch to/for him David and to ascend: offer up David burnt offering to/for face: before LORD and peace offering
18 Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
and to end: finish David from to ascend: offer up [the] burnt offering and [the] peace offering and to bless [obj] [the] people in/on/with name LORD Hosts
19 Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
and to divide to/for all [the] people to/for all crowd Israel to/for from man and till woman to/for man: anyone bun food: bread one and raisin bun one and raisin bun one and to go: went all [the] people man: anyone to/for house: home his
20 Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
and to return: return David to/for to bless [obj] house: household his and to come out: come Michal daughter Saul to/for to encounter: meet David and to say what? to honor: honour [the] day king Israel which to reveal: uncover [the] day to/for eye maidservant servant/slave his like/as to reveal: uncover to reveal: uncover one [the] worthless
21 Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
and to say David to(wards) Michal to/for face: before LORD which to choose in/on/with me from father your and from all house: household his to/for to command [obj] me leader upon people LORD upon Israel and to laugh to/for face: before LORD
22 Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
and to lighten still from this and to be low in/on/with eye my and with [the] maidservant which to say with them to honor: honour
23 Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.
and to/for Michal daughter Saul not to be to/for her youth till day death her