< 2 Samweli 6 >
1 Tena Daudi akakusanya watu 30,000 wa Israeli waliochaguliwa.
Then David again gathered together all the elect men of Israel, thirty thousand.
2 Yeye na watu wake wote wakatoka Baala ya Yuda kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka huko, linaloitwa kwa Jina, naam, jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote, ambaye anaketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi walioko juu ya hilo Sanduku.
And David arose and went away, with the entire people who were with him from the men of Judah, so that they might lead back the ark of God, over which is invoked the name of the Lord of hosts, who sits upon the cherubim above it.
3 Wakaweka hilo Sanduku la Mungu juu ya gari jipya la kukokotwa na kulileta kutoka nyumba ya Abinadabu, iliyokuwa juu ya kilima. Uza na Ahio, wana wa Abinadabu, walikuwa wakiongoza hilo gari jipya la kukokotwa
And they placed the ark of God on a new cart. And they took it from the house of Abinadab, who was in Gibeon. And Uzzah and Ahio, the sons of Abinadab, drove the new cart.
4 likiwa na Sanduku la Mungu juu yake, naye Ahio alikuwa anatembea akiwa mbele yake.
And when they had taken it from the house of Abinadab, who was in Gibeon, Ahio preceded the ark as the keeper of the ark of God.
5 Daudi na nyumba yote ya Israeli walikuwa wanacheza mbele za Bwana kwa nguvu zao zote, kwa nyimbo, vinubi, zeze, matari, kayamba na matoazi.
But David and all of Israel played before the Lord on every kind of musical instrument made of wood, and on harps, and lyres, and timbrels, and bells, and cymbals.
6 Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Nakoni, Uza akanyoosha mkono na kulishika Sanduku la Mungu kwa sababu maksai walijikwaa.
And after they had arrived at the threshing floor of Nacon, Uzzah extended his hand to the ark of God, and he touched it, because the oxen were kicking and had caused it to tip.
7 Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza kwa sababu ya kitendo chake cha kukosa heshima, kwa hiyo Mungu akampiga akafia papo hapo kando ya Sanduku la Mungu.
And the indignation of the Lord was enraged against Uzzah. And he struck him for his temerity. And there he died, beside the ark of God.
8 Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, hivyo hadi leo mahali hapo panaitwa Peres-Uza.
Then David was saddened because the Lord had struck Uzzah. And the name of that place was called: the Striking of Uzzah, even to this day.
9 Daudi akamwogopa Bwana siku ile, akasema, “Ni jinsi gani Sanduku la Bwana litakavyoweza kunijia?”
And David was very fearful of the Lord on that day, saying, “How shall the ark of the Lord be brought to me?”
10 Hakuwa radhi kulichukua Sanduku la Bwana kwake katika Mji wa Daudi. Badala yake akalipeleka kwenye nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti.
And he was not willing to send the ark of the Lord to himself in the city of David. Instead, he sent it into the house of Obededom, the Gittite.
11 Sanduku la Bwana likabaki katika nyumba ya Obed-Edomu, Mgiti, kwa miezi mitatu, naye Bwana akambariki pamoja na nyumba yake yote.
And the ark of the Lord dwelt in the house of Obededom the Gittite, for three months. And the Lord blessed Obededom, and all his household.
12 Kisha Mfalme Daudi akaambiwa, “Bwana ameibariki nyumba ya Obed-Edomu pamoja na kila alicho nacho, kwa sababu ya Sanduku la Mungu.” Basi Daudi akateremka na kulipandisha Sanduku la Mungu kutoka nyumba ya Obed-Edomu hadi Mji wa Daudi kwa shangwe.
And it was reported to king David that the Lord had blessed Obededom, and all that was his, because of the ark of God. Therefore, David went and brought the ark of God, from the house of Obededom, into the city of David with joy. And there were with David seven choirs, and calves for victims.
13 Wale waliokuwa wamebeba Sanduku la Bwana walipokuwa wametembea hatua sita, Daudi alitoa dhabihu fahali na ndama aliyenoneshwa.
And when those who were carrying the ark of the Lord had traveled six steps, he immolated an ox and a ram.
14 Daudi, akiwa amevaa kisibau cha kitani, alicheza mbele za Bwana kwa nguvu zake zote,
And David danced with all his ability before the Lord. And David was girded with the linen ephod.
15 wakati yeye na nyumba yote ya Israeli walipopandisha Sanduku la Bwana kwa shangwe na sauti za tarumbeta.
And David, and all the house of Israel, were leading the ark of the testament of the Lord, with jubilation and the sound of the trumpet.
16 Ikawa Sanduku la Bwana lilipokuwa linaingia katika Mji wa Daudi, Mikali binti Sauli akachungulia dirishani. Naye alipomwona Mfalme Daudi akirukaruka na kucheza mbele za Bwana, akamdharau moyoni mwake.
And when the ark of the Lord had entered into the city of David, Michal, the daughter of Saul, looking out through a window, saw king David leaping and dancing before the Lord. And she despised him in her heart.
17 Wakaleta Sanduku la Bwana na kuliweka mahali pake ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, naye Daudi akatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Bwana.
And they led in the ark of the Lord. And they set it in its place in the middle of the tabernacle, which David had pitched for it. And David offered holocausts and peace offerings in the sight of the Lord.
18 Baada ya kumaliza kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani, Daudi akawabariki watu katika jina la Bwana Mwenye Nguvu Zote.
And when he had completed offering holocausts and peace offerings, he blessed the people in the name of the Lord of hosts.
19 Kisha akatoa mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu kwa kila mtu katika mkutano wote wa Waisraeli, wanaume kwa wanawake. Nao watu wote wakaenda nyumbani kwao.
And he distributed to the entire multitude of Israel, as much to men as to women, to each one: one loaf of bread, and one piece of roasted beef, and fine wheat flour fried with oil. And all the people went away, each one to his own house.
20 Daudi aliporudi ili kuwabariki watu wa nyumbani mwake, Mikali binti Sauli akatoka nje kumlaki, akamwambia, “Tazama jinsi mfalme wa Israeli alivyojibainisha mwenyewe leo kwa kuvua mavazi yake machoni pa vijakazi wa watumishi wake, kama vile ambavyo mtu asiye na adabu angelifanya!”
And David returned, so that he might bless his own house. And Michal, the daughter of Saul, going out to meet David, said: “How glorious was the king of Israel today, uncovering himself before the handmaids of his servants, and being unclothed, as if one of the performers were unclothed.”
21 Daudi akamwambia Mikali, “Nilifanya hivyo mbele za Bwana ambaye alinichagua mimi badala ya baba yako au mwingine yeyote kutoka nyumba yake wakati aliponiweka niwe mtawala juu ya Israeli, watu wa Bwana. Kwa hiyo nitacheza mbele za Bwana.
And David said to Michal: “Before the Lord, who chose me rather than your father, and rather than his entire house, and who commanded me, that I should be the leader over the people of the Lord in Israel,
22 Nitakuwa asiye na heshima zaidi kuliko sasa, nami nitajishusha machoni pangu mwenyewe. Lakini kwa hawa vijakazi uliosema habari zao nitaheshimiwa.”
I will both play and demean myself, more so than I have done. And I will be little in my own eyes. And with the handmaids, about whom you are speaking, I will appear more glorious.”
23 Naye Mikali binti Sauli hakuwa na watoto mpaka siku ya kufa kwake.
And so, there was no child born to Michal, the daughter of Saul, even to the day of her death.