< 2 Samweli 5 >

1 Makabila yote ya Israeli yakamjia Daudi huko Hebroni na kumwambia, “Sisi tu nyama yako na damu yako hasa.
Then came all the tribes of Israel to Dauid vnto Hebron, and said thus, Beholde, we are thy bones and thy flesh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani. Naye Bwana alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
And in time past when Saul was our King, thou leddest Israel in and out: and the Lord hath sayde to thee, Thou shalt feede my people Israel, and thou shalt be a captaine ouer Israel.
3 Wazee wote wa Israeli wakamwendea Mfalme Daudi huko Hebroni, mfalme akafanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta kuwa mfalme wa Israeli.
So all the Elders of Israel came to the King to Hebron: and King Dauid made a couenant with them in Hebron before the Lord: and they anoynted Dauid King ouer Israel.
4 Daudi alikuwa na miaka thelathini alipoanza kutawala, naye akatawala Israeli miaka arobaini.
Dauid was thirtie yeere olde when he began to reigne: and hee reigned fortie yeere.
5 Huko Hebroni alitawala Yuda kwa miaka saba na miezi sita, na katika Yerusalemu alitawala Israeli yote na Yuda kwa miaka thelathini na mitatu.
In Hebron hee reigned ouer Iudah seuen yeere, and sixe moneths: and in Ierusalem hee reigned thirtie and three yeeres ouer all Israel and Iudah.
6 Mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kuwashambulia Wayebusi walioishi humo. Wayebusi wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu, kwani hata vipofu na viwete wanaweza kukufukuza.” Walidhani, “Daudi hawezi kuingia humu.”
The King also and his men went to Ierusalem vnto the Iebusites, the inhabitants of the land: who spake vnto Dauid, saying, Except thou take away the blinde and the lame, thou shalt not come in hither: thinking that Dauid coulde not come thither.
7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
But Dauid tooke the fort of Zion: this is the citie of Dauid.
8 Siku ile, Daudi akasema, “Yeyote ambaye atawashinda Wayebusi, atatumia huo mfereji kuwafikia hao ‘viwete na vipofu’ ambao ni adui za Daudi.” Ndiyo sababu wanasema, “‘Vipofu na viwete’ hawataingia kwenye jumba la ufalme.”
Nowe Dauid had sayd the same day, Whosoeuer smiteth the Iebusites, and getteth vp to the gutters and smiteth the lame and blinde, which Dauids soule hateth, I will preferre him: therefore they saide, The blinde and the lame shall not come into that house.
9 Ndipo Daudi akafanya makao ndani ya ngome na kuiita Mji wa Daudi. Akajenga eneo linalozunguka kuanzia Milo kuelekea ndani.
So Dauid dwelt in that forte, and called it the citie of Dauid, and Dauid built rounde about it, from Millo, and inward.
10 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
And Dauid prospered and grewe: for the Lord God of hostes was with him.
11 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, maseremala na waashi, nao wakajenga jumba la kifalme kwa ajili ya Daudi.
Hiram also king of Tyrus sent messengers to Dauid, and cedar trees, and carpenters, and masons for walles: and they built Dauid an house.
12 Naye Daudi akafahamu kuwa Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na ameinua ufalme wake kwa ajili ya Israeli, watu wake.
Then Dauid knewe that the Lord had stablished him King ouer Israel, and that he had exalted his kingdome for his people Israels sake.
13 Baada ya Daudi kuondoka Hebroni, akajitwalia masuria zaidi na wake huko Yerusalemu, nao wana na binti wengi walizaliwa kwake.
And Dauid tooke him more concubines and wiues out of Ierusalem, after hee was come from Hebron, and more sonnes and daughters were borne to Dauid.
14 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
And these bee the names of the sonnes that were borne vnto him in Ierusale: Shammua, and Shobab, and Nathan, and Salomon,
15 Ibihari, Elishua, Nefegi, Yafia,
And Ibhar, and Elishua, and Nepheg, and Iaphia,
16 Elishama, Eliada na Elifeleti.
And Elishama, and Eliada, and Eliphalet.
17 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akateremka kwenye ngome.
But when the Philistims hearde that they had anoynted Dauid King ouer Israel, all the Philistims came vp to seeke Dauid: and when Dauid heard, he went downe to a fort.
18 Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kusambaa kwenye Bonde la Warefai,
But the Philistims came, and spred themselues in the valley of Rephaim.
19 kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, “Je, niende kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, kwa maana hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”
Then Dauid asked counsel of the Lord, saying, Shall I goe vp to the Philistims? wilt thou deliuer them into mine handes? And the Lord answered Dauid, Goe vp: for I will doubtlesse deliuer the Philistims into thine handes.
20 Ndipo Daudi akaenda mpaka Baal-Perasimu, na huko akawashinda Wafilisti. Akasema, “Kama mafuriko yafurikavyo, Bwana amewafurikia adui zangu mbele yangu.” Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Baal-Perasimu.
Then Dauid came to Baal-perazim, and smote them there, and sayde, The Lord hath deuided mine enemies asunder before mee, as waters be deuided asunder: therefore he called the name of that place, Baal-perazim.
21 Wafilisti wakaiacha miungu yao huko, naye Daudi na watu wake wakaichukua.
And there they left their images, and Dauid and his men burnt them.
22 Wafilisti walikwea kwa mara nyingine na kusambaa katika Bonde la Warefai.
Againe the Philistims came vp, and spred themselues in the valley of Rephaim.
23 Kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, naye akamjibu, “Usipande moja kwa moja, bali wazungukie kwa nyuma na uwashambulie mbele ya miti ya miforosadi.
And when Dauid asked counsell of the Lord, hee answered, Thou shalt not goe vp, but turne about behinde them, and come vpon them ouer against the mulberie trees.
24 Mara utakaposikia sauti ya kutembea kutoka kwenye vilele vya miti ya miforosadi, nenda haraka, kwa sababu hiyo itamaanisha kuwa Bwana ametangulia mbele yako kupiga jeshi la Wafilisti.”
And when thou hearest the noyse of one going in the toppes of the mulberie trees, then remoue: for then shall the Lord goe out before thee, to smite the hoste of the Philistims.
25 Basi Daudi akafanya kama Bwana alivyomwagiza, naye akawaangusha Wafilisti njia yote kuanzia Geba hadi Gezeri.
Then Dauid did so as the Lord had commanded him, and smote the Philistims from Geba, vntil thou come to Gazer.

< 2 Samweli 5 >