< 2 Samweli 5 >
1 Makabila yote ya Israeli yakamjia Daudi huko Hebroni na kumwambia, “Sisi tu nyama yako na damu yako hasa.
Isarel miphunnaw Hebron kho Devit aonae koe a tho awh. Kaimanaw hah na hru hoi na thitak katang doeh.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani. Naye Bwana alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Ayan vah kaimae lathueng Sawl siangpahrang lah ao navah, Isarelnaw katâcawtkhaikung hoi kâenkhaikung lah ao. BAWIPA ni ka tami Isarelnaw na paca han, na uk han telah nang koe ati telah a ti.
3 Wazee wote wa Israeli wakamwendea Mfalme Daudi huko Hebroni, mfalme akafanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta kuwa mfalme wa Israeli.
Hatdawkvah, Isarel kacuenaw Hebron kho siangpahrang koevah a tho awh. Devit siangpahrang ni Hebron vah BAWIPA e hmalah ahnimouh hoi lawkkamnae ka sak. Devit teh Isarelnaw e siangpahrang lah satui a awi awh.
4 Daudi alikuwa na miaka thelathini alipoanza kutawala, naye akatawala Israeli miaka arobaini.
Devit ni uknae a kamtawng navah kum 30 a pha teh kum 40 touh a uk.
5 Huko Hebroni alitawala Yuda kwa miaka saba na miezi sita, na katika Yerusalemu alitawala Israeli yote na Yuda kwa miaka thelathini na mitatu.
Hebron kho dawk ao teh, Judahnaw kum 7 thapa 6 touh a uk. Jerusalem vah Isarel hoi Judahnaw kum 33 a uk.
6 Mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kuwashambulia Wayebusi walioishi humo. Wayebusi wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu, kwani hata vipofu na viwete wanaweza kukufukuza.” Walidhani, “Daudi hawezi kuingia humu.”
Siangpahrang ni a taminaw a kaw teh, hote ram dawk kho ka sak e Jebusit tami onae koe Jerusalem kho lah a cei awh. Ahnimanaw ni hete kho dawk na kâen awh mahoeh. Mitdawn hoi khokkhemnaw ni hai Devit teh hete kho thung kâen mahoeh, ahnimouh ni na ngang awh han telah ati awh.
7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Hateiteh, Devit ni Devit khopui tie Zion rapanim a tuk teh a tâ.
8 Siku ile, Daudi akasema, “Yeyote ambaye atawashinda Wayebusi, atatumia huo mfereji kuwafikia hao ‘viwete na vipofu’ ambao ni adui za Daudi.” Ndiyo sababu wanasema, “‘Vipofu na viwete’ hawataingia kwenye jumba la ufalme.”
Hote hnin dawk Devit ni, Devit hringnae ni a hmuhma e Jebusit tami mitdawn hoi khokkhem thei hanelah tui pat ka raka e ransa pueng teh ransabawinaw e lû lah ka o sak han, hatdawkvah mitdawn hoi khokkhemnaw teh im thung kâen mahoeh telah a ti.
9 Ndipo Daudi akafanya makao ndani ya ngome na kuiita Mji wa Daudi. Akajenga eneo linalozunguka kuanzia Milo kuelekea ndani.
Devit teh rapanim dawk ao teh, Devit khopui telah min a phung. Millo hmuen a tengpam thoseh, a thung lahai thoseh a sak.
10 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
Hottelah hoi Devit teh hoe a roung teh ransahu BAWIPA Cathut hoi rei ao.
11 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, maseremala na waashi, nao wakajenga jumba la kifalme kwa ajili ya Daudi.
Taire siangpahrang Hiram ni Devit koe patounenaw a patoun teh, Sidar thing, imsakkathoum, talungdêikathoum a patoun awh teh, Devit hane im a sak pouh awh.
12 Naye Daudi akafahamu kuwa Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na ameinua ufalme wake kwa ajili ya Israeli, watu wake.
BAWIPA ni Isarelnaw koe siangpahrang lah ahni teh a caksak e hoi, a tami Isarelnaw hanelah uknaeram a tawmrasang tie Devit ni a panue.
13 Baada ya Daudi kuondoka Hebroni, akajitwalia masuria zaidi na wake huko Yerusalemu, nao wana na binti wengi walizaliwa kwake.
Devit ni Hebron kho hoi a kampuen hnukkhu, Jerusalem khothung e yu a puidonaw bout a la teh, a ca moikapap bout a tawn.
14 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Jerusalem kho sak Devit ni a khe e a canaw e min teh: Shammua, Shobab, Nathan, Solomon,
15 Ibihari, Elishua, Nefegi, Yafia,
Ibhar, Elishua, Nepheg, Japhia,
16 Elishama, Eliada na Elifeleti.
Elishama, Eliada hoi Eliphelet naw hah doeh.
17 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akateremka kwenye ngome.
Filistinnaw ni Devit hah Isarelnaw koe siangpahrang lah ao nahan satui a awi tie a panue awh navah, Filistinnaw pueng ni Devit tawng hanelah a cei awh. Devit ni hote hah a thai toteh rapanim dawk hoi a kum.
18 Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kusambaa kwenye Bonde la Warefai,
Filistinnaw hai a cei awh teh, Rephaim yawn dawk phang a kâkayei awh.
19 kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, “Je, niende kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, kwa maana hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”
Devit ni Filistinnaw tuk hanelah ka cei han maw, ka kut dawk na poe han maw telah BAWIPA a pacei. BAWIPA ni Devit koe, cet loe. Kai ni Filistinnaw na kut dawk na poe han telah atipouh.
20 Ndipo Daudi akaenda mpaka Baal-Perasimu, na huko akawashinda Wafilisti. Akasema, “Kama mafuriko yafurikavyo, Bwana amewafurikia adui zangu mbele yangu.” Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Baal-Perasimu.
Devit teh Baalperazim lah a cei teh, hawvah Devit ni ahnimouh a thei. BAWIPA ni, tui ni a raphoe e patetlah katarannaw hah ka hmaitung vah koung na raphoe pouh telah ati. Hatdawkvah, hote hmuen hah Baalperazim telah min a phung.
21 Wafilisti wakaiacha miungu yao huko, naye Daudi na watu wake wakaichukua.
Hote hmuen koe Filistinnaw ni a ceitakhai e meikaphawknaw hah Devit hoi a taminaw ni koung a raphoe pouh.
22 Wafilisti walikwea kwa mara nyingine na kusambaa katika Bonde la Warefai.
Filistinnaw bout a tho awh teh, Rephaim yawn dawk phang a kâkayei awh.
23 Kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, naye akamjibu, “Usipande moja kwa moja, bali wazungukie kwa nyuma na uwashambulie mbele ya miti ya miforosadi.
Devit ni BAWIPA koe a pacei navah, ahni ni takhang awh hanh, a hnuk lahoi kalup awh nateh batue kahrawng koehoi rongyawn awh.
24 Mara utakaposikia sauti ya kutembea kutoka kwenye vilele vya miti ya miforosadi, nenda haraka, kwa sababu hiyo itamaanisha kuwa Bwana ametangulia mbele yako kupiga jeshi la Wafilisti.”
Batuekung koe a pawlawk na thai toteh tuk awh loe, bangkongtetpawiteh, Filistinnaw tuk hanelah na hmalah BAWIPA a la cei toe tinae doeh.
25 Basi Daudi akafanya kama Bwana alivyomwagiza, naye akawaangusha Wafilisti njia yote kuanzia Geba hadi Gezeri.
BAWIPA ni kâlawk a poe e patetlah Devit ni a sak. Filistinnaw hah Geba hoi Gezer totouh a thei.