< 2 Samweli 5 >
1 Makabila yote ya Israeli yakamjia Daudi huko Hebroni na kumwambia, “Sisi tu nyama yako na damu yako hasa.
Israel koca pum loh David te Hebron la a paan uh tih, “Kaimih he namah rhuh, kaimih he namah saa dae la he.
2 Zamani, wakati Sauli alikuwa mfalme juu yetu, wewe ndiwe uliyeiongoza Israeli vitani. Naye Bwana alikuambia, ‘Wewe utawachunga watu wangu Israeli, na utakuwa mtawala wao.’”
Hlaem hlavai kah Saul a om vaengah ni kaimih soah manghai la na om khaw na om rhoe coeng. Israel te a thak, a thak tih a pawk khaw a pawk puei. Te dongah ni BOEIPA loh namah taengah, 'Ka pilnam Israel te na luem puei vetih Israel soah rhaengsang la na om bitni,’ a ti pai,” a ti uh.
3 Wazee wote wa Israeli wakamwendea Mfalme Daudi huko Hebroni, mfalme akafanya mapatano nao huko Hebroni mbele za Bwana, nao wakamtia Daudi mafuta kuwa mfalme wa Israeli.
Israel patong boeih loh Hebron la manghai te a paan uh. Te vaengah manghai David loh amih te Hebron ah moi a boh pah tih BOEIPA mikhmuh ah David te Israel sokah manghai la a koelh uh.
4 Daudi alikuwa na miaka thelathini alipoanza kutawala, naye akatawala Israeli miaka arobaini.
David a manghai vaengah kum sawmthum lo ca coeng tih kum sawmli khuiah manghai van.
5 Huko Hebroni alitawala Yuda kwa miaka saba na miezi sita, na katika Yerusalemu alitawala Israeli yote na Yuda kwa miaka thelathini na mitatu.
Hebron ah Judah te kum rhih hla rhuk a manghai thil tih Jerusalem ah Israel neh Judah pum te kum sawmthum kum thum a manghai thil.
6 Mfalme na watu wake wakaenda Yerusalemu kuwashambulia Wayebusi walioishi humo. Wayebusi wakamwambia Daudi, “Wewe hutaingia humu, kwani hata vipofu na viwete wanaweza kukufukuza.” Walidhani, “Daudi hawezi kuingia humu.”
Manghai neh a hlang rhoek loh Jerusalem khohmuen khosa kung Jebusi te a caeh uh thil hatah David te a voek tih, “Hela na kun mahpawh, hela David kun boel saeh a ti coeng atah mikdael rhoek neh aka khaem rhoek long mah nang te n'haek thai,” a ti nah.
7 Hata hivyo, Daudi akaiteka ngome ya Sayuni, Mji wa Daudi.
Tedae David loh Zion rhalvong David khopuei te vik a loh.
8 Siku ile, Daudi akasema, “Yeyote ambaye atawashinda Wayebusi, atatumia huo mfereji kuwafikia hao ‘viwete na vipofu’ ambao ni adui za Daudi.” Ndiyo sababu wanasema, “‘Vipofu na viwete’ hawataingia kwenye jumba la ufalme.”
Te khohnin ah David loh, “Aka khaem khaw, mikdael khaw, khat khat long khaw Jebusi aka ngawn tah tuikun khaw pha saeh,” a ti. Te khaw David kah a hinglu a hmuhuet, la a hmuhuet uh tih mikdael khokhaem loh, “Im khuila ha kun boel saeh,” a ti uh dongah ni.
9 Ndipo Daudi akafanya makao ndani ya ngome na kuiita Mji wa Daudi. Akajenga eneo linalozunguka kuanzia Milo kuelekea ndani.
Rhalvong te David loh a om thil dongah David Khopuei la a khue. Te dongah vaikhap lamloh imkhui duela a kaepvai te David loh a sak.
10 Daudi akazidi kuwa na nguvu zaidi na zaidi, kwa sababu Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote alikuwa pamoja naye.
David a caeh a pongpa vaengah a pantai te caempuei Pathen BOEIPA loh anih a om puei dongah ni.
11 Basi Hiramu mfalme wa Tiro akawatuma wajumbe kwa Daudi, wakiwa na magogo ya mierezi, maseremala na waashi, nao wakajenga jumba la kifalme kwa ajili ya Daudi.
Tyre manghai Khiram loh David taengla puencawn a tueih tih lamphai thing, thing kutthai, pangbueng dongkah ham lungto kutthai neh David ham im a sak uh.
12 Naye Daudi akafahamu kuwa Bwana amemwimarisha kuwa mfalme juu ya Israeli na ameinua ufalme wake kwa ajili ya Israeli, watu wake.
Israel sokah manghai la BOEIPA loh anih a thoh khaw, a pilnam Israel kong ah a ram a phoh te khaw David loh a ming.
13 Baada ya Daudi kuondoka Hebroni, akajitwalia masuria zaidi na wake huko Yerusalemu, nao wana na binti wengi walizaliwa kwake.
David loh yupuei yula muep a loh dongah Hebron lamkah Jerusalem la a pawk vaengah David ham capa neh canu khawk a sak pauh.
14 Haya ndiyo majina ya watoto waliozaliwa kwake huko: Shamua, Shobabu, Nathani, Solomoni,
Jerusalem ah anih ham aka thaang rhoek a ming rhoek tah Shammua, Shobab, Nathan, Solomon,
15 Ibihari, Elishua, Nefegi, Yafia,
Ibhar, Elishua neh, Nepheg neh Japhia,
16 Elishama, Eliada na Elifeleti.
Elishama, Eliada neh Eliphelet.
17 Wafilisti waliposikia kuwa Daudi ametiwa mafuta kuwa mfalme wa Israeli, wakapanda na jeshi lao lote kwenda kumsaka, lakini Daudi akapata habari hizo, naye akateremka kwenye ngome.
Israel sokah manghai la David a koelh uh te Philisti rhoek loh a yaak uh vaengah David mae hamla Philisti rhoek boeih cet uh. Tedae David loh a yaak tih rhalvong la suntla thuk.
18 Basi Wafilisti walikuwa wamekuja na kusambaa kwenye Bonde la Warefai,
Te vaengah Philisti rhoek ha pawk uh tih Rapha kol ah khawk taai uh.
19 kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, “Je, niende kuwashambulia Wafilisti? Je, utawatia mikononi mwangu?” Bwana akamjibu, “Nenda, kwa maana hakika nitawatia Wafilisti mikononi mwako.”
David loh BOEIPA te a dawt tih, “Philisti te ka paan a yaa, amih te ka kut dongah nan tloeng aya?” a ti nah hatah BOEIPA loh David te, “Cet! Philisti te na kut dongah kam paek rhoe kam paek ni,” a ti nah.
20 Ndipo Daudi akaenda mpaka Baal-Perasimu, na huko akawashinda Wafilisti. Akasema, “Kama mafuriko yafurikavyo, Bwana amewafurikia adui zangu mbele yangu.” Kwa hiyo mahali hapo pakaitwa Baal-Perasimu.
David te Baalperazim la cet tih amih te a ngawn. Te vaengah David loh, “Ka thunkha rhoek te BOEIPA loh ka mikhmuh ah tui puut bangla a va coeng,” a ti. Te dongah tekah hmuen te a ming Baalperazim la a khue.
21 Wafilisti wakaiacha miungu yao huko, naye Daudi na watu wake wakaichukua.
Te vaengah a hnoo uh sut amih muei te David neh a hlang rhoek loh a koh uh.
22 Wafilisti walikwea kwa mara nyingine na kusambaa katika Bonde la Warefai.
Te phoeiah a rhaep la Philisti rhoek koep cet uh tih Rapha kol ah taai uh.
23 Kwa hiyo Daudi akamuuliza Bwana, naye akamjibu, “Usipande moja kwa moja, bali wazungukie kwa nyuma na uwashambulie mbele ya miti ya miforosadi.
Te vaengah David loh BOEIPA te a dawt hatah, “Cet boeh, a hnuk longah vael lamtah, amih te tikti rhaldan ah khoep cuuk.
24 Mara utakaposikia sauti ya kutembea kutoka kwenye vilele vya miti ya miforosadi, nenda haraka, kwa sababu hiyo itamaanisha kuwa Bwana ametangulia mbele yako kupiga jeshi la Wafilisti.”
Tikti soi ah haeksak ol na yaak la, na yaak coeng atah cuuk thil laeh. Philisti lambong tloek ham te na hmaiah BOEIPA cet coeng,” a ti nah.
25 Basi Daudi akafanya kama Bwana alivyomwagiza, naye akawaangusha Wafilisti njia yote kuanzia Geba hadi Gezeri.
BOEIPA loh amah a uen bangla David loh a saii tih Philisti te a tloek tih Geba lamloh Gezer la pawk.