< 2 Samweli 4 >

1 Ish-Boshethi mwana wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, akakosa ujasiri, nayo Israeli yote wakatiwa hofu kuu.
Quand le fils de Saül apprit qu'Abner était mort à Hébron, ses mains devinrent lâches, et tout Israël fut consterné.
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa vikundi vya uvamizi. Mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu, waliokuwa wana wa Rimoni, Mbeerothi, kutoka kabila la Benyamini. Beerothi alihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini,
Or le fils de Saül avait deux chefs de bandes, dont l'un s'appelait Baana et l'autre Récab; ils étaient fils de Rimmon le Beérothien, des enfants de Benjamin (car Beéroth était réputé appartenir à Benjamin,
3 kwa sababu watu wa Beerothi walikimbilia huko Gitaimu na wameishi huko kama wageni mpaka siku hii ya leo.
Et les Beérothiens s'étaient enfuis à Guitthaïm, et ils y ont séjourné jusqu'à aujourd'hui).
4 (Yonathani mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa mlemavu miguu yote miwili. Alikuwa na miaka mitano wakati habari kuhusu Sauli na Yonathani zilipofika kutoka Yezreeli. Yaya wake akambeba ili kukimbia, lakini yaya alipokuwa anaharakisha kuondoka, mtoto alianguka akawa kiwete. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.)
Or Jonathan, fils de Saül, avait un fils perclus des pieds; il était âgé de cinq ans lorsque la nouvelle de la mort de Saül et de Jonathan arriva de Jizréel; et sa gouvernante le prit et s'enfuit, et comme elle se hâtait de fuir, il tomba et devint boiteux; son nom était Méphibosheth.
5 Basi Rekabu na Baana, wana wa Rimoni Mbeerothi wakaenda nyumbani kwa Ish-Boshethi, nao walifika huko wakati alipokuwa kwenye mapumziko yake ya mchana.
Les fils de Rimmon, le Beérothien, Récab et Baana, vinrent donc et entrèrent à la chaleur du jour dans la maison d'Ishbosheth, comme il prenait son repos de midi;
6 Wakaingia kwenye chumba cha ndani kana kwamba wanachukua ngano, wakamchoma Ish-Boshethi mkuki wa tumboni. Ndipo Rekabu na Baana nduguye wakatoroka.
Ils entrèrent jusqu'au milieu de la maison, comme pour y prendre du froment, et ils le frappèrent au ventre; puis Récab et Baana, son frère, s'enfuirent.
7 Walikuwa wameingia ndani ya nyumba wakati alipokuwa amelala kitandani chumbani kwake. Baada ya kumchoma mkuki na kumuua, walikata kichwa chake. Wakiwa wamekichukua, walitembea usiku kucha kwa njia ya Araba.
Ils entrèrent donc dans la maison, lorsqu'Ishbosheth était couché sur son lit, dans la chambre où il dormait; et ils le frappèrent et le firent mourir; puis ils lui coupèrent la tête, et la prirent, et marchèrent par le chemin de la plaine toute cette nuit-là.
8 Wakamletea Daudi kichwa cha Ish-Boshethi huko Hebroni, wakamwambia mfalme, “Hiki hapa kichwa cha Ish-Boshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyejaribu kuondoa uhai wako. Siku hii ya leo Bwana amemlipia kisasi mfalme bwana wangu dhidi ya Sauli na mzao wake.”
Et ils apportèrent la tête d'Ishbosheth à David, à Hébron, et ils dirent au roi: Voici la tête d'Ishbosheth, fils de Saül, ton ennemi, qui cherchait ta vie; l'Éternel a vengé aujourd'hui le roi, mon seigneur, de Saül et de sa race.
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni, Mbeerothi, akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka taabu zote,
Mais David répondit à Récab et à Baana, son frère, fils de Rimmon, le Beérothien, et leur dit: L'Éternel est vivant, qui a délivré mon âme de toutes mes détresses!
10 yule mtu aliponiambia, ‘Sauli amekufa,’ akadhani ananiletea habari njema, nilimkamata, nikamuua huko Siklagi. Hiyo ndiyo zawadi niliyompa kwa ajili ya taarifa yake!
J'ai saisi celui qui vint m'annoncer et me dire: Voilà, Saül est mort; et qui pensait m'apprendre de bonnes nouvelles, et je le fis mourir à Tsiklag, pour prix de ses bonnes nouvelles.
11 Je, ni mara ngapi zaidi wakati watu waovu wamemuua mtu asiye na hatia akiwa ndani ya nyumba yake mwenyewe na kwenye kitanda chake mwenyewe? Je, sasa nisidai damu yake mikononi mwenu na kuwaondoa duniani?”
Combien plus, quand des méchants ont tué un homme de bien, dans sa maison, sur son lit, ne redemanderai-je pas maintenant son sang de votre main, et ne vous exterminerai-je pas de la terre?
12 Kwa hiyo Daudi akawaamuru watu wake, wakawaua. Wakakata mikono yao na miguu, na kutundika viwiliwili vyao kando ya dimbwi huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ish-Boshethi na kukizika katika kaburi la Abneri huko Hebroni.
Et David donna ordre à ses gens, qui les tuèrent, et leur coupèrent les mains et les pieds, et les pendirent près de l'étang d'Hébron. Puis ils prirent la tête d'Ishbosheth, et l'ensevelirent dans le tombeau d'Abner, à Hébron.

< 2 Samweli 4 >