< 2 Samweli 4 >

1 Ish-Boshethi mwana wa Sauli aliposikia kwamba Abneri amekufa huko Hebroni, akakosa ujasiri, nayo Israeli yote wakatiwa hofu kuu.
Quand Isboseth, fils de Saül, apprit qu'Abner, fils de Ner, était mort à Hébron, ses bras en furent énervés, et tous les hommes d'Israël défaillirent.
2 Basi mwana wa Sauli alikuwa na watu wawili waliokuwa viongozi wa vikundi vya uvamizi. Mmoja aliitwa Baana na mwingine Rekabu, waliokuwa wana wa Rimoni, Mbeerothi, kutoka kabila la Benyamini. Beerothi alihesabiwa kuwa sehemu ya Benyamini,
Or, il y avait deux chefs des troupes d'Isboseth, fils de Saül: l'un se nommait Baana, et l'autre Rhéchab; ils étaient fils de Rhemmon, de Bèroth de la tribu de Benjamin; car Bèroth était comptée parmi les villes de Benjamin.
3 kwa sababu watu wa Beerothi walikimbilia huko Gitaimu na wameishi huko kama wageni mpaka siku hii ya leo.
Ceux de Bèroth ont depuis émigré à Géthalin, où, de nos jours encore, ils sont colons.
4 (Yonathani mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa mlemavu miguu yote miwili. Alikuwa na miaka mitano wakati habari kuhusu Sauli na Yonathani zilipofika kutoka Yezreeli. Yaya wake akambeba ili kukimbia, lakini yaya alipokuwa anaharakisha kuondoka, mtoto alianguka akawa kiwete. Jina lake aliitwa Mefiboshethi.)
Il restait de Jonathan, fils de Saül, un fils de cinq ans, infirme des pieds; car, lorsqu'on vint de Jezraël annoncer que Saül et Jonathan étaient morts, la nourrice de cet enfant le prit dans ses bras et s'enfuit. En se hâtant de l'éloigner, elle le laissa tomber, et il resta boiteux; il se nommait Miphiboseth.
5 Basi Rekabu na Baana, wana wa Rimoni Mbeerothi wakaenda nyumbani kwa Ish-Boshethi, nao walifika huko wakati alipokuwa kwenye mapumziko yake ya mchana.
Et les fils de Rhemmon le Bérothéen, Rhéchab et Baana partirent; et, par la grande chaleur du jour, ils entrèrent chez Isboseth, comme il dormait sur un lit de repos, à l'heure de midi.
6 Wakaingia kwenye chumba cha ndani kana kwamba wanachukua ngano, wakamchoma Ish-Boshethi mkuki wa tumboni. Ndipo Rekabu na Baana nduguye wakatoroka.
Le gardien de la porte avait vanné du froment, sa tête s'était affaissée, et il s'était endormi; Rhéchab et Baana poussèrent donc plus avant.
7 Walikuwa wameingia ndani ya nyumba wakati alipokuwa amelala kitandani chumbani kwake. Baada ya kumchoma mkuki na kumuua, walikata kichwa chake. Wakiwa wamekichukua, walitembea usiku kucha kwa njia ya Araba.
Ils pénètrent dans la maison où Isboseth dormait sur son lit de repos, en sa chambre à coucher; ils le frappent, le tuent, lui tranchent la tête, qu'ils emportent, et marchent toute la nuit du côté de l'occident.
8 Wakamletea Daudi kichwa cha Ish-Boshethi huko Hebroni, wakamwambia mfalme, “Hiki hapa kichwa cha Ish-Boshethi mwana wa Sauli, adui yako, aliyejaribu kuondoa uhai wako. Siku hii ya leo Bwana amemlipia kisasi mfalme bwana wangu dhidi ya Sauli na mzao wake.”
Et ils portèrent à David, en Hébron, la tète d'Isboseth, et ils dirent au roi: Voici la tête d'Isboseth, fils de Saül, ton ennemi, qui te cherchait pour te faire périr; le Seigneur a achevé aujourd'hui de venger, de Saül et de sa race, le seigneur roi.
9 Daudi akawajibu Rekabu na Baana nduguye, wana wa Rimoni, Mbeerothi, akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, ambaye ameniokoa kutoka taabu zote,
Et David répondit à Rhéchab et à Baana son frère, fils de Rhemmon le Bérothéen, et il leur dit: Vive le Seigneur! le sauveur de mon âme en toutes ses afflictions,
10 yule mtu aliponiambia, ‘Sauli amekufa,’ akadhani ananiletea habari njema, nilimkamata, nikamuua huko Siklagi. Hiyo ndiyo zawadi niliyompa kwa ajili ya taarifa yake!
Celui qui est venu m'annoncer la mort de Saül, et qui croyait m'apporter une bonne nouvelle, je l'ai saisi et l'ai fait mourir en Sécelac, où il s'attendait à recevoir une récompense.
11 Je, ni mara ngapi zaidi wakati watu waovu wamemuua mtu asiye na hatia akiwa ndani ya nyumba yake mwenyewe na kwenye kitanda chake mwenyewe? Je, sasa nisidai damu yake mikononi mwenu na kuwaondoa duniani?”
Et maintenant, de méchants hommes ont tué un homme juste, dans sa maison, sur sa couche. Certes, je vous demanderai compte du sang que votre main a versé, et je vous effacerai de la terre.
12 Kwa hiyo Daudi akawaamuru watu wake, wakawaua. Wakakata mikono yao na miguu, na kutundika viwiliwili vyao kando ya dimbwi huko Hebroni. Lakini wakakichukua kichwa cha Ish-Boshethi na kukizika katika kaburi la Abneri huko Hebroni.
David donna donc ses ordres à ses serviteurs, et ils les tuèrent; puis, ils leurs coupèrent les mains et les pieds, et les pendirent vers la fontaine d'Hébron, et ils inhumèrent la tête d'Isboseth dans le sépulcre d'Abner, fils de Ner.

< 2 Samweli 4 >