< 2 Samweli 3 >
1 Vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vilidumu kwa muda mrefu. Daudi akaendelea kuwa imara zaidi na zaidi, wakati nyumba ya Sauli iliendelea kudhoofika zaidi na zaidi.
Saul'un soyuyla Davut'un soyu arasındaki savaş uzun sürdü. Davut giderek güçlenirken, Saul'un soyu gitgide zayıf düşüyordu.
2 Wana walizaliwa kwa Daudi huko Hebroni: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni mwana wa Ahinoamu wa Yezreeli;
Davut'un Hevron'da doğan oğulları şunlardı: İlk oğlu Yizreelli Ahinoam'dan Amnon,
3 mzaliwa wake wa pili alikuwa Danieli mwana wa Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli; wa tatu, Absalomu mwana wa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri;
ikincisi Karmelli Naval'ın dulu Avigayil'den Kilav, üçüncüsü Geşur Kralı Talmay'ın kızı Maaka'dan Avşalom,
4 wa nne, Adoniya mwana wa Hagithi; wa tano, Shefatia mwana wa Abitali;
dördüncüsü Hagit'ten Adoniya, beşincisi Avital'ın oğlu Şefatya,
5 wa sita, Ithreamu mwana wa Egla, mkewe Daudi. Hawa ndio waliozaliwa kwa Daudi huko Hebroni.
altıncısı Davut'un eşi Egla'dan Yitream. Davut'un bu oğullarının hepsi Hevron'da doğdular.
6 Wakati wa vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri alikuwa anajiimarisha katika nafasi yake kwenye nyumba ya Sauli.
Saul'un soyuyla Davut'un soyu arasındaki savaş sürerken, Avner Saul'un soyu arasında güçleniyordu.
7 Basi Sauli alikuwa amekuwa na suria, jina lake Rispa binti wa Aiya. Naye Ish-Boshethi akamwambia Abneri, “Kwa nini umekutana kimwili na suria wa baba yangu?”
Saul'un Aya kızı Rispa adında bir cariyesi vardı. Bir gün İş-Boşet Avner'e, “Neden babamın cariyesiyle yattın?” diye sordu.
8 Abneri akakasirika sana kwa sababu ya kile Ish-Boshethi alichosema, naye akamjibu, “Je, mimi ni kichwa cha mbwa, kwa upande wa Yuda? Siku hii ya leo mimi ni mtiifu kwa nyumba ya baba yako Sauli, kwa jamaa yake na rafiki zake. Sijakukabidhi kwa Daudi, lakini bado unanilaumu kwa kosa la kuhusika na huyu mwanamke!
İş-Boşet'in sorusuna çok öfkelenen Avner şu karşılığı verdi: “Ben Yahuda tarafına geçen bir köpek başı mıyım? Bugün bile baban Saul'un ailesine, kardeşlerine, dostlarına bağlıyım. Seni Davut'un eline teslim etmedim. Ama bugün bu kadın yüzünden beni suçluyorsun.
9 Mungu na amshughulikie Abneri, tena kwa ukali, ikiwa sitafanya kwa ajili ya Daudi kile Bwana alichomwahidi kwa kiapo,
RAB krallığı Saul'un soyundan alıp Dan'dan Beer-Şeva'ya kadar uzanan İsrail ve Yahuda'da Davut'un krallığını kuracağına ant içti. Ben de bunu Davut için yapmazsam Tanrı bana aynısını, hatta daha kötüsünü yapsın!”
10 na kuuhamisha ufalme kutoka kwenye nyumba ya Sauli na kuimarisha kiti cha ufalme cha Daudi juu ya Israeli na Yuda kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba.”
11 Ish-Boshethi hakuthubutu kusema neno jingine kwa Abneri, kwa sababu alimwogopa Abneri.
İş-Boşet Avner'den korktuğu için ona başka bir şey söyleyemedi.
12 Ndipo Abneri akatuma wajumbe kwa niaba yake kwa Daudi, kumwambia, “Nchi hii ni ya nani? Fanya mapatano na mimi, nami nitakusaidia kuiweka Israeli yote juu yako.”
Avner kendi adına Davut'a ulaklar gönderip şöyle dedi: “Ülke kimin ülkesi? Benimle bir antlaşma yap; o zaman İsrail'in tümünün sana bağlanması için ben de senden yana olurum.”
13 Daudi akasema, “Vyema, nitafanya mapatano nawe. Lakini nahitaji jambo moja kwako: Usije mbele yangu mpaka umemleta Mikali binti Sauli wakati utakapokuja kuniona.”
Davut, “İyi” diye yanıtladı, “Seninle bir antlaşma yaparım. Yalnız senden şunu istiyorum: Beni görmeye geldiğinde Saul'un kızı Mikal'ı da getir. Yoksa beni görmeyeceksin.”
14 Kisha Daudi akapeleka wajumbe kwa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, kudai, “Nipe Mikali mke wangu, ambaye nilimposa mwenyewe kwa mahari ya magovi 100 ya Wafilisti.”
Öte yandan Davut Saul oğlu İş-Boşet'e de ulaklar aracılığıyla şu haberi gönderdi: “Yüz Filistli'nin sünnet derisi karşılığında nişanlandığım karım Mikal'ı bana ver.”
15 Kwa hiyo Ish-Boshethi akatoa amri kwamba Mikali achukuliwe kutoka kwa Paltieli mumewe, mwana wa Laishi.
Bunun üzerine İş-Boşet, kadının kocası Layiş oğlu Paltiel'den alınıp getirilmesi için adamlar gönderdi.
16 Hata hivyo, mumewe alikwenda pamoja naye, akilia nyuma ya mkewe njia yote hadi Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia Paltieli, “Rudi nyumbani!” Kwa hiyo akarudi.
Kocası kadını ağlaya ağlaya Bahurim'e kadar izledi; sonra Avner ona, “Geri dön” deyince döndü.
17 Abneri akafanya shauri pamoja na wazee wa Israeli, akasema, “Muda mrefu mmetaka kumfanya Daudi mfalme wenu.
Avner İsrail'in ileri gelenleriyle görüşüp onlara şöyle demişti: “Siz bir süredir Davut'un kralınız olmasını istiyorsunuz.
18 Sasa fanyeni hivyo! Kwa maana Bwana alimwahidi Daudi akisema, ‘Kwa kupitia Daudi mtumishi wangu nitawaokoa watu wangu Israeli kutoka mikononi mwa Wafilisti na kutoka mikononi mwa adui zako wote.’”
Şimdi bunu gerçekleştirin! Çünkü RAB, Davut hakkında, ‘Halkım İsrail'i kulum Davut aracılığıyla Filistliler'in ve bütün düşmanlarının elinden kurtaracağım’ demişti.”
19 Pia Abneri mwenyewe akazungumza na kabila la Benyamini. Kisha akaenda mpaka Hebroni kumwambia Daudi kila kitu ambacho Israeli na nyumba yote ya Benyamini walichotaka kufanya.
Avner Benyaminliler'le de görüştü, İsrail'in ve bütün Benyamin halkının uygun gördüğü her şeyi Davut'a bildirmek üzere Hevron'a gitti.
20 Wakati Abneri aliyekuwa na watu ishirini pamoja naye, alipokuja kwa Daudi huko Hebroni, Daudi akamwandalia karamu pamoja na watu wake.
Avner yirmi kişiyle birlikte Hevron'a, Davut'un yanına vardı. Davut Avner'le yanındakilere bir şölen verdi.
21 Ndipo Abneri akamwambia Daudi, “Niache niende mara moja nikakusanye Israeli yote kwa ajili ya mfalme bwana wangu, ili waweze kufanya mapatano na wewe, ili kwamba uweze kutawala juu ya yote yale ambayo moyo wako unaonea shauku.” Basi Daudi akamuaga Abneri, naye akaenda kwa amani.
Avner Davut'a, “Hemen gidip bütün İsrail halkını efendim kralın yanına toplayayım” dedi, “Öyle ki, seninle bir antlaşma yapsınlar. Sen de dilediğin her yeri yönetebilesin.” Bunun üzerine Davut Avner'i yoluna gönderdi. O da esenlikle gitti.
22 Wakati huo huo, watu wa Daudi na Yoabu walirudi kutoka kwenye kushambulia, nao wakarudi na nyara nyingi mno. Lakini Abneri hakuwa tena pamoja na Daudi huko Hebroni, kwa sababu Daudi alikuwa amemruhusu aende zake, naye akaenda kwa amani.
Tam o sırada Davut'un adamlarıyla Yoav, bir baskından dönmüş, yanlarında birçok yağmalanmış mal getirmişlerdi. Ama Avner Hevron'da Davut'un yanında değildi. Çünkü Davut onu göndermiş, o da esenlikle gitmişti.
23 Yoabu na askari wote aliokuwa nao walipowasili, aliambiwa kwamba Abneri mwana wa Neri alikuwa amekuja kwa mfalme na kwamba mfalme alikuwa amemruhusu aende zake, na kwamba alikwisha ondoka kwa amani.
Yoav'la yanındaki bütün askerler Hevron'a vardığında, Ner oğlu Avner'in krala geldiğini, kralın onu gönderdiğini, onun da esenlikle gittiğini Yoav'a bildirdiler.
24 Basi Yoabu alikwenda kwa mfalme na kumwambia, “Ni nini hiki ulichofanya? Tazama, Abneri alikuja kwako. Kwa nini ukamwacha aende? Sasa amekwenda!
Yoav krala gidip, “Ne yaptın?” dedi, “Baksana Avner ayağına kadar gelmiş! Neden onu salıverdin? Çoktan gitmiş!
25 Wajua Abneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya na kuchunguza nyendo zako na kupata kila kitu unachokifanya.”
Ner oğlu Avner'i tanırsın; seni kandırmak, nereye gidip geldiğini, neler yaptığını öğrenmek için gelmiştir.”
26 Ndipo Yoabu akamwacha Daudi na kutuma wajumbe wamfuate Abneri, nao wakamrudisha kutoka kisima cha Sira. Lakini Daudi hakufahamu jambo hili.
Davut'un yanından çıkan Yoav, Avner'in arkasından ulaklar gönderdi. Ulaklar Avner'i Sira Sarnıcı'ndan geri getirdiler. Davut ise bundan habersizdi.
27 Basi Abneri aliporudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando ndani ya lango, kama vile kuzungumza naye faraghani. Ili kulipiza kisasi damu ya nduguye Asaheli, Yoabu akamchoma mkuki tumboni palepale, naye akafa.
Avner Hevron'a dönünce, Yoav onunla özel bir görüşme yapmak bahanesiyle, onu kent kapısına çekti. Kardeşi Asahel'in kanını döktüğü için, Avner'i orada karnından vurup öldürdü.
28 Baadaye, Daudi aliposikia kuhusu jambo hili, akasema, “Mimi na ufalme wangu kamwe hatuna hatia mbele za Bwana kuhusu damu ya Abneri mwana wa Neri.
Davut bu haberi işitince şöyle dedi: “RAB'bin önünde ben de, krallığım da Ner oğlu Avner'in kanından sonsuza dek suçsuzuz.
29 Damu yake na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya nyumba yote ya baba yake! Kamwe asikosekane yeyote katika nyumba ya Yoabu mwenye kidonda chenye usaha, au ukoma au mwenye kuegemea fimbo au aangukaye kwa upanga au kupungukiwa na chakula.”
Bu suçun sorumlusu Yoav'la babasının bütün soyu olsun. Yoav'ın soyundan irinli, deri hastalığına yakalanmış, koltuk değneğine dayanan, kılıçla öldürülen, açlık çeken kişiler hiç eksik olmasın!”
30 (Yoabu na Abishai ndugu yake walimuua Abneri kwa sababu alikuwa amemuua Asaheli ndugu yao katika vita huko Gibeoni.)
Böylece Yoav'la kardeşi Avişay, Givon'daki savaşta kardeşleri Asahel'i öldüren Avner'i öldürdüler.
31 Kisha Daudi akamwambia Yoabu na watu wote aliokuwa pamoja nao, “Rarueni nguo zenu na mvae nguo za gunia na mtembee mkiomboleza mbele ya Abneri.” Mfalme Daudi mwenyewe akatembea nyuma ya jeneza.
Sonra Davut Yoav'la yanındakilere şu buyruğu verdi: “Giysilerinizi yırtıp çula sarının ve Avner'in ölüsü önünde yas tutun!” Kral Davut da cenazenin ardısıra yürüdü.
32 Wakamzika Abneri huko Hebroni, naye mfalme akalia kwa sauti kwenye kaburi la Abneri. Pia watu wote wakalia.
Avner'i Hevron'da gömdüler. Kral, Avner'in mezarı başında hıçkıra hıçkıra ağladı. Oradaki herkes de ağladı.
33 Mfalme akaimba ombolezo hili kwa ajili ya Abneri: “Je, ilipasa Abneri afe kama afavyo mpumbavu?
Sonra kral, Avner için şu ağıtı yaktı: “Avner, bir budala gibi mi ölmeliydi?
34 Mikono yako haikufungwa, miguu yako haikufungwa pingu. Ulianguka kama yeye aangukaye mbele ya watu waovu.” Nao watu wote wakamlilia tena.
Ellerin bağlı değildi, ayaklarına zincir vurulmamıştı. Ama sen kötülerin önünde düşen biri gibi düştün!” Herkes Avner için yine ağladı.
35 Kisha watu wote wakaja kumsihi Daudi ale chochote kulipokuwa kungali bado mchana; lakini Daudi akaapa, akisema, “Mungu na anishughulikie, tena kwa ukali, kama nikionja mkate au kitu kingine chochote kabla ya jua kutua!”
Halk Davut'un yanına varıp akşam olmadan bir şeyler yemesi için üstelediyse de, Davut ant içerek şöyle dedi: “Güneş batmadan ekmek ya da başka herhangi bir şey tatmayacağım. Yoksa Tanrı bana aynısını, hatta daha kötüsünü yapsın!”
36 Watu wote wakaona hilo nao ikawapendeza; naam, kila kitu mfalme alichofanya kiliwapendeza.
Herkes bunu benimsedi ve kralın yaptığı her şeyden hoşnut oldukları gibi, bundan da hoşnut oldular.
37 Kwa hiyo siku ile watu wote na Israeli yote wakajua kwamba mfalme hakushiriki katika mauaji ya Abneri mwana wa Neri.
Ner oğlu Avner'in öldürülmesinde kralın parmağı olmadığını o gün bütün İsrail halkı anladı.
38 Kisha mfalme akawaambia watu wake, “Je, hamfahamu kwamba mkuu na mtu mashuhuri ameanguka katika Israeli leo?
Kral adamlarına, “Bugün İsrail'de bir önderin, büyük bir adamın öldüğünü bilmiyor musunuz?” dedi,
39 Nami leo ingawa ni mfalme mpakwa mafuta, mimi ni dhaifu, nao hawa wana wa Seruya wananizidi nguvu. Bwana na amlipize mtenda maovu sawasawa na matendo yake maovu!”
“Meshedilmiş bir kral olduğum halde bugün güçsüzüm. Seruya'nın oğulları benden daha zorlu. RAB kötülük edene yaptığı kötülüğe göre karşılık versin!”