< 2 Samweli 3 >

1 Vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vilidumu kwa muda mrefu. Daudi akaendelea kuwa imara zaidi na zaidi, wakati nyumba ya Sauli iliendelea kudhoofika zaidi na zaidi.
I dugo bijaše rat izmeðu doma Saulova i doma Davidova; ali David sve veæma jaèaše a dom Saulov postajaše sve slabiji.
2 Wana walizaliwa kwa Daudi huko Hebroni: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni mwana wa Ahinoamu wa Yezreeli;
I Davidu se rodiše sinovi u Hevronu: prvenac mu bješe Amnon od Ahinoame Jezraeljanke;
3 mzaliwa wake wa pili alikuwa Danieli mwana wa Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli; wa tatu, Absalomu mwana wa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri;
Drugi bješe Hileav od Avigeje žene Navala Karmilca; treæi Avesalom sin Mahe kæeri Talmaja cara Gesurskoga;
4 wa nne, Adoniya mwana wa Hagithi; wa tano, Shefatia mwana wa Abitali;
Èetvrti Adonija sin Agitin; i peti Sefatija sin Avitalin;
5 wa sita, Ithreamu mwana wa Egla, mkewe Daudi. Hawa ndio waliozaliwa kwa Daudi huko Hebroni.
I šesti Itram od Egle žene Davidove. Ti se rodiše Davidu u Hevronu.
6 Wakati wa vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri alikuwa anajiimarisha katika nafasi yake kwenye nyumba ya Sauli.
I dok bijaše rat izmeðu doma Saulova i doma Davidova, Avenir branjaše dom Saulov.
7 Basi Sauli alikuwa amekuwa na suria, jina lake Rispa binti wa Aiya. Naye Ish-Boshethi akamwambia Abneri, “Kwa nini umekutana kimwili na suria wa baba yangu?”
A Saul imaše inoèu po imenu Resfu kæer Ajinu; i Isvostej reèe Aveniru: zašto si spavao kod inoèe oca mojega?
8 Abneri akakasirika sana kwa sababu ya kile Ish-Boshethi alichosema, naye akamjibu, “Je, mimi ni kichwa cha mbwa, kwa upande wa Yuda? Siku hii ya leo mimi ni mtiifu kwa nyumba ya baba yako Sauli, kwa jamaa yake na rafiki zake. Sijakukabidhi kwa Daudi, lakini bado unanilaumu kwa kosa la kuhusika na huyu mwanamke!
I Avenir se razgnjevi na rijeèi Isvostejeve i reèe: jesam li ja pasja glava, koji sada èinim na Judi milost domu Saula oca tvojega i braæi njegovoj i prijateljima njegovijem, i nijesam te pustio u ruke Davidove, te danas tražiš na meni zlo radi te žene?
9 Mungu na amshughulikie Abneri, tena kwa ukali, ikiwa sitafanya kwa ajili ya Daudi kile Bwana alichomwahidi kwa kiapo,
Tako neka uèini Bog Aveniru, i tako neka doda, ako ne uèinim Davidu kako mu se Gospod zakleo,
10 na kuuhamisha ufalme kutoka kwenye nyumba ya Sauli na kuimarisha kiti cha ufalme cha Daudi juu ya Israeli na Yuda kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba.”
Da se prenese ovo carstvo od doma Saulova, i da se utvrdi prijesto Davidov nad Izrailjem i nad Judom, od Dana do Virsaveje.
11 Ish-Boshethi hakuthubutu kusema neno jingine kwa Abneri, kwa sababu alimwogopa Abneri.
I on ne može više ništa odgovoriti Aveniru, jer ga se bojaše.
12 Ndipo Abneri akatuma wajumbe kwa niaba yake kwa Daudi, kumwambia, “Nchi hii ni ya nani? Fanya mapatano na mimi, nami nitakusaidia kuiweka Israeli yote juu yako.”
I Avenir posla poslanike k Davidu od sebe i poruèi: èija je zemlja? I poruèi mu: uèini vjeru sa mnom, i evo ruka æe moja biti s tobom, da obratim k tebi svega Izrailja.
13 Daudi akasema, “Vyema, nitafanya mapatano nawe. Lakini nahitaji jambo moja kwako: Usije mbele yangu mpaka umemleta Mikali binti Sauli wakati utakapokuja kuniona.”
A on odgovori: dobro; ja æu uèiniti vjeru s tobom; ali jedno ištem od tebe, i to: da ne vidiš lica mojega ako mi prvo ne dovedeš Mihalu kæer Saulovu, kad doðeš da vidiš lice moje.
14 Kisha Daudi akapeleka wajumbe kwa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, kudai, “Nipe Mikali mke wangu, ambaye nilimposa mwenyewe kwa mahari ya magovi 100 ya Wafilisti.”
I posla David poslanike k Isvosteju sinu Saulovu, i poruèi mu: daj mi ženu moju Mihalu, koju isprosih za sto okrajaka Filistejskih.
15 Kwa hiyo Ish-Boshethi akatoa amri kwamba Mikali achukuliwe kutoka kwa Paltieli mumewe, mwana wa Laishi.
I Isvostej posla te je uze od muža, od Faltila, sina Laisova.
16 Hata hivyo, mumewe alikwenda pamoja naye, akilia nyuma ya mkewe njia yote hadi Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia Paltieli, “Rudi nyumbani!” Kwa hiyo akarudi.
A muž njezin poðe s njom, i jednako plakaše za njom do Vaurima. Tada mu reèe Avenir: idi, vrati se natrag. I on se vrati.
17 Abneri akafanya shauri pamoja na wazee wa Israeli, akasema, “Muda mrefu mmetaka kumfanya Daudi mfalme wenu.
Potom Avenir govori starješinama Izrailjskim, i reèe im: preðe tražiste Davida da bude car nad vama.
18 Sasa fanyeni hivyo! Kwa maana Bwana alimwahidi Daudi akisema, ‘Kwa kupitia Daudi mtumishi wangu nitawaokoa watu wangu Israeli kutoka mikononi mwa Wafilisti na kutoka mikononi mwa adui zako wote.’”
Eto sada uèinite; jer je Gospod rekao za Davida govoreæi: preko Davida sluge svojega izbaviæu narod svoj Izrailja iz ruku Filistejskih i iz ruku svijeh neprijatelja njihovijeh.
19 Pia Abneri mwenyewe akazungumza na kabila la Benyamini. Kisha akaenda mpaka Hebroni kumwambia Daudi kila kitu ambacho Israeli na nyumba yote ya Benyamini walichotaka kufanya.
Tako govori Avenir i sinovima Venijaminovijem. Potom otide Avenir i u Hevron da kaže Davidu sve što za dobro naðe Izrailj i sav dom Venijaminov.
20 Wakati Abneri aliyekuwa na watu ishirini pamoja naye, alipokuja kwa Daudi huko Hebroni, Daudi akamwandalia karamu pamoja na watu wake.
I kad doðe Avenir k Davidu u Hevron i s njim dvadeset ljudi, uèini David gozbu Aveniru i ljudima koji bijahu s njim.
21 Ndipo Abneri akamwambia Daudi, “Niache niende mara moja nikakusanye Israeli yote kwa ajili ya mfalme bwana wangu, ili waweze kufanya mapatano na wewe, ili kwamba uweze kutawala juu ya yote yale ambayo moyo wako unaonea shauku.” Basi Daudi akamuaga Abneri, naye akaenda kwa amani.
I reèe Avenir Davidu: da ustanem i idem da skupim k caru gospodaru svojemu sav narod Izrailjev da uèine vjeru s tobom, pa da caruješ kako ti duša želi. I David otpusti Avenira da ide s mirom.
22 Wakati huo huo, watu wa Daudi na Yoabu walirudi kutoka kwenye kushambulia, nao wakarudi na nyara nyingi mno. Lakini Abneri hakuwa tena pamoja na Daudi huko Hebroni, kwa sababu Daudi alikuwa amemruhusu aende zake, naye akaenda kwa amani.
A gle, sluge Davidove vraæahu se s Joavom iz boja, i tjerahu sa sobom velik plijen; a Avenir veæ ne bješe kod Davida u Hevronu, jer ga otpusti, te otide s mirom.
23 Yoabu na askari wote aliokuwa nao walipowasili, aliambiwa kwamba Abneri mwana wa Neri alikuwa amekuja kwa mfalme na kwamba mfalme alikuwa amemruhusu aende zake, na kwamba alikwisha ondoka kwa amani.
Joav dakle i sva vojska što bješe s njim doðoše onamo; i javiše Joavu govoreæi: Avenir sin Nirov dolazio je k caru, i on ga otpusti te otide s mirom.
24 Basi Yoabu alikwenda kwa mfalme na kumwambia, “Ni nini hiki ulichofanya? Tazama, Abneri alikuja kwako. Kwa nini ukamwacha aende? Sasa amekwenda!
I Joav otide k caru i reèe: šta uèini? Gle, Avenir je dolazio k tebi; zašto ga pusti te otide?
25 Wajua Abneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya na kuchunguza nyendo zako na kupata kila kitu unachokifanya.”
Poznaješ li Avenira sina Nirova? dolazio je da te prevari, da vidi kuda hodiš i da dozna sve šta radiš.
26 Ndipo Yoabu akamwacha Daudi na kutuma wajumbe wamfuate Abneri, nao wakamrudisha kutoka kisima cha Sira. Lakini Daudi hakufahamu jambo hili.
Potom otišav Joav od Davida posla ljude za Avenirom da ga vrate od studenca Sire, a David ne znadijaše za to.
27 Basi Abneri aliporudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando ndani ya lango, kama vile kuzungumza naye faraghani. Ili kulipiza kisasi damu ya nduguye Asaheli, Yoabu akamchoma mkuki tumboni palepale, naye akafa.
I kad se vrati Avenir u Hevron, odvede ga Joav na stranu pod vrata kao da govori s njim nasamo; ondje ga udari pod peto rebro, te umrije za krv Asaila brata njegova.
28 Baadaye, Daudi aliposikia kuhusu jambo hili, akasema, “Mimi na ufalme wangu kamwe hatuna hatia mbele za Bwana kuhusu damu ya Abneri mwana wa Neri.
A kad David poslije to èu, reèe: ja nijesam kriv ni carstvo moje pred Gospodom dovijeka za krv Avenira sina Nirova.
29 Damu yake na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya nyumba yote ya baba yake! Kamwe asikosekane yeyote katika nyumba ya Yoabu mwenye kidonda chenye usaha, au ukoma au mwenye kuegemea fimbo au aangukaye kwa upanga au kupungukiwa na chakula.”
Neka padne na glavu Joavovu i na sav dom oca njegova; i neka dom Joavov ne bude nikad bez èovjeka bolna od teèenja ili gubava ili koji ide o štapu ili koji padne od maèa ili koji nema hljeba.
30 (Yoabu na Abishai ndugu yake walimuua Abneri kwa sababu alikuwa amemuua Asaheli ndugu yao katika vita huko Gibeoni.)
Tako Joav i Avisaj brat njegov ubiše Avenira što on pogubi Asaila brata njihova kod Gavaona u boju.
31 Kisha Daudi akamwambia Yoabu na watu wote aliokuwa pamoja nao, “Rarueni nguo zenu na mvae nguo za gunia na mtembee mkiomboleza mbele ya Abneri.” Mfalme Daudi mwenyewe akatembea nyuma ya jeneza.
I reèe David Joavu i svemu narodu koji bijaše s njim: razderite haljine svoje i pripašite kostrijet, i plaèite za Avenirom. I car David iðaše za nosilima.
32 Wakamzika Abneri huko Hebroni, naye mfalme akalia kwa sauti kwenye kaburi la Abneri. Pia watu wote wakalia.
A kad pogreboše Avenira u Hevronu, car podiže glas svoj i plaka na grobu Avenirovu; plaka i sav narod.
33 Mfalme akaimba ombolezo hili kwa ajili ya Abneri: “Je, ilipasa Abneri afe kama afavyo mpumbavu?
I narièuæi za Avenirom reèe: umrije li Avenir kako umire bezumnik?
34 Mikono yako haikufungwa, miguu yako haikufungwa pingu. Ulianguka kama yeye aangukaye mbele ya watu waovu.” Nao watu wote wakamlilia tena.
Ruke tvoje ne biše vezane, niti noge tvoje u okov okovane; pao si kao što se pada od nevaljalijeh ljudi. Tada još veæma plaka za njim sav narod.
35 Kisha watu wote wakaja kumsihi Daudi ale chochote kulipokuwa kungali bado mchana; lakini Daudi akaapa, akisema, “Mungu na anishughulikie, tena kwa ukali, kama nikionja mkate au kitu kingine chochote kabla ya jua kutua!”
I doðe sav narod nudeæi Davida da jede što, dok još bijaše dan; ali se David zakle i reèe: Bog neka mi uèini tako, i tako neka doda, ako okusim hljeba ili što drugo dok ne zaðe sunce.
36 Watu wote wakaona hilo nao ikawapendeza; naam, kila kitu mfalme alichofanya kiliwapendeza.
I sav narod èu to, i bi im po volji; što god èinjaše car, bješe po volji svemu narodu.
37 Kwa hiyo siku ile watu wote na Israeli yote wakajua kwamba mfalme hakushiriki katika mauaji ya Abneri mwana wa Neri.
I pozna sav narod i sav Izrailj u onaj dan da nije bilo od cara što pogibe Avenir sin Nirov.
38 Kisha mfalme akawaambia watu wake, “Je, hamfahamu kwamba mkuu na mtu mashuhuri ameanguka katika Israeli leo?
I car reèe slugama svojim: ne znate li da je vojvoda i to veliki poginuo danas u Izrailju?
39 Nami leo ingawa ni mfalme mpakwa mafuta, mimi ni dhaifu, nao hawa wana wa Seruya wananizidi nguvu. Bwana na amlipize mtenda maovu sawasawa na matendo yake maovu!”
Ali ja sam sada još slab, ako i jesam pomazani car; a ovi ljudi, sinovi Serujini, vrlo su mi silni. Neka Gospod plati onome koji èini zlo prema zloæi njegovoj.

< 2 Samweli 3 >