< 2 Samweli 3 >

1 Vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi vilidumu kwa muda mrefu. Daudi akaendelea kuwa imara zaidi na zaidi, wakati nyumba ya Sauli iliendelea kudhoofika zaidi na zaidi.
و جنگ در میان خاندان شاول و خاندان داود به طول انجامید و داود روز به روزقوت می‌گرفت و خاندان شاول روز به روزضعیف می‌شدند.۱
2 Wana walizaliwa kwa Daudi huko Hebroni: Mzaliwa wake wa kwanza alikuwa Amnoni mwana wa Ahinoamu wa Yezreeli;
و برای داود در حبرون پسران زاییده شدند، و نخست زاده‌اش، عمون، از اخینوعم یزرعیلیه بود.۲
3 mzaliwa wake wa pili alikuwa Danieli mwana wa Abigaili, mjane wa Nabali wa Karmeli; wa tatu, Absalomu mwana wa Maaka, binti Talmai mfalme wa Geshuri;
و دومش، کیلاب، از ابیجایل، زن نابال کرملی، و سوم، ابشالوم، پسر معکه، دختر تلمای پادشاه جشور.۳
4 wa nne, Adoniya mwana wa Hagithi; wa tano, Shefatia mwana wa Abitali;
و چهارم ادونیا، پسر حجیت، وپنجم شفطیا پسر ابیطال،۴
5 wa sita, Ithreamu mwana wa Egla, mkewe Daudi. Hawa ndio waliozaliwa kwa Daudi huko Hebroni.
و ششم، یترعام ازعجله، زن داود. اینان برای داود در حبرون زاییده شدند.۵
6 Wakati wa vita kati ya nyumba ya Sauli na nyumba ya Daudi, Abneri alikuwa anajiimarisha katika nafasi yake kwenye nyumba ya Sauli.
و هنگامی که جنگ در میان خاندان شاول وخاندان داود می‌بود، ابنیر، خاندان شاول راتقویت می‌نمود.۶
7 Basi Sauli alikuwa amekuwa na suria, jina lake Rispa binti wa Aiya. Naye Ish-Boshethi akamwambia Abneri, “Kwa nini umekutana kimwili na suria wa baba yangu?”
و شاول را کنیزی مسمی به رصفه دختر ایه بود، و ایشبوشت به ابنیر گفت: «چرا به کنیز پدرم درآمدی؟»۷
8 Abneri akakasirika sana kwa sababu ya kile Ish-Boshethi alichosema, naye akamjibu, “Je, mimi ni kichwa cha mbwa, kwa upande wa Yuda? Siku hii ya leo mimi ni mtiifu kwa nyumba ya baba yako Sauli, kwa jamaa yake na rafiki zake. Sijakukabidhi kwa Daudi, lakini bado unanilaumu kwa kosa la kuhusika na huyu mwanamke!
و خشم ابنیر به‌سبب سخن ایشبوشت بسیار افروخته شده، گفت: «آیا من سر سگ برای یهودا هستم و حال آنکه امروز به خاندان پدرت، شاول، و برادرانش واصحابش احسان نموده‌ام و تو را به‌دست داودتسلیم نکرده‌ام که به‌سبب این زن امروز گناه بر من اسناد می‌دهی؟۸
9 Mungu na amshughulikie Abneri, tena kwa ukali, ikiwa sitafanya kwa ajili ya Daudi kile Bwana alichomwahidi kwa kiapo,
خدا مثل این و زیاده از این به ابنیر بکند اگر من به طوری که خداوند برای داودقسم خورده است، برایش چنین عمل ننمایم.۹
10 na kuuhamisha ufalme kutoka kwenye nyumba ya Sauli na kuimarisha kiti cha ufalme cha Daudi juu ya Israeli na Yuda kuanzia Dani mpaka Beer-Sheba.”
تا سلطنت را از خاندان شاول نقل نموده، کرسی داود را بر اسرائیل و یهودا از دان تا بئرشبع پایدار گردانم.»۱۰
11 Ish-Boshethi hakuthubutu kusema neno jingine kwa Abneri, kwa sababu alimwogopa Abneri.
و او دیگر نتوانست در جواب ابنیر سخنی گوید زیرا که از او می‌ترسید.۱۱
12 Ndipo Abneri akatuma wajumbe kwa niaba yake kwa Daudi, kumwambia, “Nchi hii ni ya nani? Fanya mapatano na mimi, nami nitakusaidia kuiweka Israeli yote juu yako.”
پس ابنیر در آن حین قاصدان نزد داودفرستاده، گفت: «این زمین مال کیست؟ و گفت تو بامن عهد ببند و اینک دست من با تو خواهد بود تاتمامی اسرائیل را به سوی تو برگردانم.»۱۲
13 Daudi akasema, “Vyema, nitafanya mapatano nawe. Lakini nahitaji jambo moja kwako: Usije mbele yangu mpaka umemleta Mikali binti Sauli wakati utakapokuja kuniona.”
اوگفت: «خوب، من با تو عهد خواهم بست ولیکن یک چیز از تو می‌طلبم و آن این است که روی مرانخواهی دید، جز اینکه اول چون برای دیدن روی من بیایی میکال، دختر شاول را بیاوری.»۱۳
14 Kisha Daudi akapeleka wajumbe kwa Ish-Boshethi mwana wa Sauli, kudai, “Nipe Mikali mke wangu, ambaye nilimposa mwenyewe kwa mahari ya magovi 100 ya Wafilisti.”
پس داود رسولان نزد ایشبوشت بن شاول فرستاده، گفت: «زن من، میکال را که برای خود به صد قلفه فلسطینیان نامزد ساختم، نزد من بفرست.»۱۴
15 Kwa hiyo Ish-Boshethi akatoa amri kwamba Mikali achukuliwe kutoka kwa Paltieli mumewe, mwana wa Laishi.
پس ایشبوشت فرستاده، او را از نزد شوهرش فلطئیل بن لایش گرفت.۱۵
16 Hata hivyo, mumewe alikwenda pamoja naye, akilia nyuma ya mkewe njia yote hadi Bahurimu. Ndipo Abneri akamwambia Paltieli, “Rudi nyumbani!” Kwa hiyo akarudi.
و شوهرش همراهش رفت و در عقبش تا حوریم گریه می‌کرد. پس ابنیر وی را گفت: «برگشته، برو.» و اوبرگشت.۱۶
17 Abneri akafanya shauri pamoja na wazee wa Israeli, akasema, “Muda mrefu mmetaka kumfanya Daudi mfalme wenu.
و ابنیر با مشایخ اسرائیل تکلم نموده، گفت: «قبل از این داود را می‌طلبیدید تا بر شماپادشاهی کند.۱۷
18 Sasa fanyeni hivyo! Kwa maana Bwana alimwahidi Daudi akisema, ‘Kwa kupitia Daudi mtumishi wangu nitawaokoa watu wangu Israeli kutoka mikononi mwa Wafilisti na kutoka mikononi mwa adui zako wote.’”
پس الان این را به انجام برسانیدزیرا خداوند درباره داود گفته است که به وسیله بنده خود، داود، قوم خویش، اسرائیل را از دست فلسطینیان و از دست جمیع دشمنان ایشان نجات خواهم داد.»۱۸
19 Pia Abneri mwenyewe akazungumza na kabila la Benyamini. Kisha akaenda mpaka Hebroni kumwambia Daudi kila kitu ambacho Israeli na nyumba yote ya Benyamini walichotaka kufanya.
و ابنیر به گوش بنیامینیان نیزسخن گفت. و ابنیر هم به حبرون رفت تا آنچه راکه در نظر اسرائیل و در نظر تمامی خاندان بنیامین پسند آمده بود، به گوش داود بگوید.۱۹
20 Wakati Abneri aliyekuwa na watu ishirini pamoja naye, alipokuja kwa Daudi huko Hebroni, Daudi akamwandalia karamu pamoja na watu wake.
پس ابنیر بیست نفر با خود برداشته، نزدداود به حبرون آمد و داود به جهت ابنیر ورفقایش ضیافتی برپا کرد.۲۰
21 Ndipo Abneri akamwambia Daudi, “Niache niende mara moja nikakusanye Israeli yote kwa ajili ya mfalme bwana wangu, ili waweze kufanya mapatano na wewe, ili kwamba uweze kutawala juu ya yote yale ambayo moyo wako unaonea shauku.” Basi Daudi akamuaga Abneri, naye akaenda kwa amani.
و ابنیر به داود گفت: «من برخاسته، خواهم رفت و تمامی اسرائیل رانزد آقای خود، پادشاه، جمع خواهم آورد تا با توعهد ببندند و به هر‌آنچه دلت می‌خواهد سلطنت نمایی. پس داود ابنیر را مرخص نموده، او به سلامتی برفت.۲۱
22 Wakati huo huo, watu wa Daudi na Yoabu walirudi kutoka kwenye kushambulia, nao wakarudi na nyara nyingi mno. Lakini Abneri hakuwa tena pamoja na Daudi huko Hebroni, kwa sababu Daudi alikuwa amemruhusu aende zake, naye akaenda kwa amani.
و ناگاه بندگان داود و یوآب از غارتی بازآمده، غنیمت بسیار با خود آوردند. و ابنیر با داوددر حبرون نبود زیرا وی را رخصت داده، و او به سلامتی رفته بود.۲۲
23 Yoabu na askari wote aliokuwa nao walipowasili, aliambiwa kwamba Abneri mwana wa Neri alikuwa amekuja kwa mfalme na kwamba mfalme alikuwa amemruhusu aende zake, na kwamba alikwisha ondoka kwa amani.
و چون یوآب و تمامی لشکری که همراهش بودند، برگشتند، یوآب راخبر داده، گفتند که «ابنیر بن نیر نزد پادشاه آمد واو را رخصت داده و به سلامتی رفت.»۲۳
24 Basi Yoabu alikwenda kwa mfalme na kumwambia, “Ni nini hiki ulichofanya? Tazama, Abneri alikuja kwako. Kwa nini ukamwacha aende? Sasa amekwenda!
پس یوآب نزد پادشاه آمده، گفت: «چه کردی! اینک ابنیر نزد تو آمد. چرا او را رخصت دادی و رفت؟۲۴
25 Wajua Abneri mwana wa Neri alikuja kukudanganya na kuchunguza nyendo zako na kupata kila kitu unachokifanya.”
ابنیر بن نیر را می‌دانی که او آمد تا تو را فریب دهد و خروج و دخول تو را بداند و هر کاری را که می‌کنی دریافت کند.»۲۵
26 Ndipo Yoabu akamwacha Daudi na kutuma wajumbe wamfuate Abneri, nao wakamrudisha kutoka kisima cha Sira. Lakini Daudi hakufahamu jambo hili.
و یوآب از حضور داود بیرون رفته، قاصدان در عقب ابنیر فرستاد که او را از چشمه سیره بازآوردند اما داود ندانست.۲۶
27 Basi Abneri aliporudi Hebroni, Yoabu akamchukua kando ndani ya lango, kama vile kuzungumza naye faraghani. Ili kulipiza kisasi damu ya nduguye Asaheli, Yoabu akamchoma mkuki tumboni palepale, naye akafa.
و چون ابنیربه حبرون برگشت، یوآب او را در میان دروازه به کنار کشید تا با او به خفیه سخن گوید و به‌سبب خون برادرش عسائیل به شکم او زد که مرد.۲۷
28 Baadaye, Daudi aliposikia kuhusu jambo hili, akasema, “Mimi na ufalme wangu kamwe hatuna hatia mbele za Bwana kuhusu damu ya Abneri mwana wa Neri.
وبعد از آن چون داود این را شنید، گفت: «من وسلطنت من به حضور خداوند از خون ابنیر بن نیرتا به ابد بری هستیم.۲۸
29 Damu yake na iwe juu ya kichwa cha Yoabu na juu ya nyumba yote ya baba yake! Kamwe asikosekane yeyote katika nyumba ya Yoabu mwenye kidonda chenye usaha, au ukoma au mwenye kuegemea fimbo au aangukaye kwa upanga au kupungukiwa na chakula.”
پس بر سر یوآب و تمامی خاندان پدرش قرار گیرد و کسی‌که جریان وبرص داشته باشد و بر عصا تکیه کند و به شمشیربیفتد و محتاج نان باشد، از خاندان یوآب منقطع نشود.»۲۹
30 (Yoabu na Abishai ndugu yake walimuua Abneri kwa sababu alikuwa amemuua Asaheli ndugu yao katika vita huko Gibeoni.)
و یوآب و برادرش ابیشای، ابنیر راکشتند، به‌سبب این که برادر ایشان، عسائیل را درجبعون در جنگ کشته بود.۳۰
31 Kisha Daudi akamwambia Yoabu na watu wote aliokuwa pamoja nao, “Rarueni nguo zenu na mvae nguo za gunia na mtembee mkiomboleza mbele ya Abneri.” Mfalme Daudi mwenyewe akatembea nyuma ya jeneza.
و داود به یوآب و تمامی قومی که همراهش بودند، گفت: «جامه خود را بدرید وپلاس بپوشید و برای ابنیر نوحه کنید.» و داودپادشاه در عقب جنازه رفت.۳۱
32 Wakamzika Abneri huko Hebroni, naye mfalme akalia kwa sauti kwenye kaburi la Abneri. Pia watu wote wakalia.
و ابنیر را درحبرون دفن کردند و پادشاه آواز خود را بلندکرده، نزد قبر ابنیر گریست و تمامی قوم گریه کردند.۳۲
33 Mfalme akaimba ombolezo hili kwa ajili ya Abneri: “Je, ilipasa Abneri afe kama afavyo mpumbavu?
و پادشاه برای ابنیر مرثیه خوانده، گفت: «آیا باید ابنیر بمیرد به طوری که شخص احمق می‌میرد.۳۳
34 Mikono yako haikufungwa, miguu yako haikufungwa pingu. Ulianguka kama yeye aangukaye mbele ya watu waovu.” Nao watu wote wakamlilia tena.
دستهای تو بسته نشد وپایهایت در زنجیر گذاشته نشد. مثل کسی‌که پیش شریران افتاده باشد افتادی.» پس تمامی قوم بار دیگر برای او گریه کردند.۳۴
35 Kisha watu wote wakaja kumsihi Daudi ale chochote kulipokuwa kungali bado mchana; lakini Daudi akaapa, akisema, “Mungu na anishughulikie, tena kwa ukali, kama nikionja mkate au kitu kingine chochote kabla ya jua kutua!”
و تمامی قوم چون هنوز روز بود آمدند تا داود را نان بخوراننداما داود قسم خورده، گفت: «خدا به من مثل این بلکه زیاده از این بکند اگر نان یا چیز دیگر پیش ازغروب آفتاب بچشم.»۳۵
36 Watu wote wakaona hilo nao ikawapendeza; naam, kila kitu mfalme alichofanya kiliwapendeza.
و تمامی قوم ملتفت شدند و به نظر ایشان پسند آمد. چنانکه هر‌چه پادشاه می‌کرد، در نظر تمامی قوم پسند می‌آمد.۳۶
37 Kwa hiyo siku ile watu wote na Israeli yote wakajua kwamba mfalme hakushiriki katika mauaji ya Abneri mwana wa Neri.
و جمیع قوم و تمامی اسرائیل در آن روزدانستند که کشتن ابنیر بن نیر از پادشاه نبود.۳۷
38 Kisha mfalme akawaambia watu wake, “Je, hamfahamu kwamba mkuu na mtu mashuhuri ameanguka katika Israeli leo?
وپادشاه به خادمان خود گفت: «آیا نمی دانید که سروری و مرد بزرگی امروز در اسرائیل افتاد؟۳۸
39 Nami leo ingawa ni mfalme mpakwa mafuta, mimi ni dhaifu, nao hawa wana wa Seruya wananizidi nguvu. Bwana na amlipize mtenda maovu sawasawa na matendo yake maovu!”
و من امروز با آنکه به پادشاهی مسح شده‌ام ضعیف هستم و این مردان، یعنی پسران صرویه ازمن تواناترند. خداوند عامل شرارت را بر‌حسب شرارتش جزا دهد.»۳۹

< 2 Samweli 3 >