< 2 Samweli 24 >
1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
Tedy się znowu popędliwość Pańska zapaliła na Izraela, gdy pobudził szatan Dawida przeciwko nim mówiąc: Idź, policz Izraela i Judę.
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
I rzekł król do Joaba, hetmana wojska swego: Przbież zaraz wszystkie pokolenia Izraelskie od Dan aż do Beerseba, a policzcie lud, abym wiedział poczet ludu.
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
Lecz Joab rzekł do króla: Niech przymnoży Pan, Bóg twój, ludu, jako teraz jest tyle stokroć, aby na to oczy króla, pana mego patrzały; ale król, pan mój, przeczże się tego napiera?
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
Wszakże przemogło słowo królewskie Joaba i hetmany wojska. Przetoż wyszedł Joab, i hetmani wojska od oblicza królewskiego, aby policzyli lud Izraelski.
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
A przeprawiwszy się przez Jordan, położyli się obozem przy Aroer, po prawej stronie miasta, które jest w pośród potoku Gad i przy Jazer.
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
Potem przyszli do Galaad, i do ziemi dolnej Hadsy, a stamtąd przyszli do Dan Jaan i w okół Sydonu.
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
Potem przyszli ku twierdzy Tyrskiej, i do wszystkich miast Hewejskich i Chananejskich, skąd wyszli na południe Judy do Beerseba.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
A obszedłszy wszystkę ziemię, przyszli po dziewięciu miesiącach, i po dwudziestu dniach do Jeruzalemu.
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
I oddał Joab poczet obliczonego ludu królowi. A było w Izraelu ośm kroć sto tysięcy mężów rycerskich, godnych ku bojowi, a mężów Juda pięć kroć sto tysięcy mężów.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Potem uderzyło Dawida serce jego, gdy obliczył lud, i rzekł Dawid do Pana: Zgrzeszyłem bardzo, żem to uczynił: ale teraz o Panie! przenieś proszę nieprawość sługi twego, bomci bardzo głupio uczynił.
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
A gdy wstał Dawid rano, oto słowo Pańskie stało się do Gada proroka, Widzącego Dawidowego, mówiąc:
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
Idź, a powiedz Dawidowi: Tak mówi Pan: Trzyć rzeczy podawam, obierz sobie jednę z tych, abym ci uczynił.
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
A tak przyszedł Gad do Dawida, i oznajmił mu, a rzekł mu: Albo przyjdzie na cię głód przez siedm lat w ziemi twojej, albo przez trzy miesiące będziesz uciekał przed nieprzyjacioły twymi, a oni cię gonić będą, albo więc przez trzy dni będzie morowe powietrze w ziemi twojej; rozmyśl że się prędko, a obacz, co mam odpowiedzieć temu, który mię posłał.
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
I rzekł Dawid do Gada: Jestem bardzo ściśniony. Niech proszę raczej wpadniemy w rękę Pańską, gdyż wielkie są zlitowania jego; ale w rękę ludzką niech nie wpadam.
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
Tedy przepuścił Pan powietrze morowe na Izraela od poranku aż do czasu naznaczonego, i umarło z ludu od Dan aż do Beerseba siedmdziesiąt tysięcy mężów.
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
A gdy wyciągnął Anioł rękę swą na Jeruzalem, aby je wytracił, tedy się użalił Pan onego złego, i rzekł do Anioła, który tracił lud: Dosyć teraz; zawściągnij rękę twą. A Anioł Pański był podle bojewiska Arawny Jebuzejczyka.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
I rzekł Dawid do Pana, gdy ujrzał Anioła bijącego lud, mówiąc: Otom ja zgrzeszył, jam źle uczynił; ale te owce cóż uczyniły? niech się proszę obróci ręka twoja na mię i na dom ojca mego.
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
Tedy przyszedł Gad do Dawida onegoż dnia, i rzekł mu: Idź, a zbuduj ołtarz Panu na bojewisku Arawy Jebuzejczyka.
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
I szedł Dawid podług słowa Gadowego, jako był rozkazał Pan.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
Tedy spojrzawszy Arawna, ujrzał króla, i sługi jego, przychodzące do siebie: i wyszedł Arawna, a pokłonił się królowi twarzą swą ku ziemi.
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
I rzekł Arawna: Przeczże przyszedł król, pan mój, do sługi swego? I odpowiedział Dawid: Abym kupił u ciebie to bojewisko, i zbudował na niem ołtarz Panu, żeby zahamowana była ta plaga między ludem.
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
Tedy rzekł Arawna do Dawida: Niech weźmie, a ofiaruje król, pan mój, co mu się dobrego widzi: oto woły na całopalenie, i wozy, i jarzma wołów na drwa.
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Wszystko to dawał król Arawna królowi Dawidowi. I mówił Arawna do króla: Pan, Bóg twój, niech cię sobie upodoba.
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
Lecz król rzekł do Arawny: Nie tak, ale raczej kupię u ciebie i zapłacę; ani będę ofiarował Panu, Bogu memu, całopalenia darmo danego. A tak kupił Dawid ono bojewisko i woły za pięćdziesiąt syklów srebra.
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
Tamże zbudował Dawid ołtarz Panu, i sprawował całopalenia, i spokojne ofiary. I ubłagany był Pan ziemi, a zahamowana jest ona plaga od Izraela.