< 2 Samweli 24 >
1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
La colère du Seigneur s'enflamma encore contre Israël; et il poussa David contre le peuple, en lui disant: Va, et fais le dénombrement d'Israël et de Juda.
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
Et le roi dit à Joab, général de ses troupes, qui était avec lui: Parcours toutes les tribus d'Israël et de Juda, depuis Dan jusqu'à Bersabée; fais le recensement du peuple, et j'en saurai le nombre.
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
Joab répondit au roi: Puisse le Seigneur Dieu ajouter à ce peuple, et le rendre cent fois aussi nombreux qu'il l'est; puisse le roi mon maître le voir de ses yeux; mais pourquoi le roi mon maître a-t-il formé ce dessein?
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
Mais la volonté du roi prévalut sur Joab et les autres chefs de l'armée. Joab partit donc avec les chefs des forces qui entouraient David, pour faire le recensement du peuple d'Israël.
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
Et ils traversèrent le Jourdain, et ils campèrent dans les champs d'Aroer, à droite de la ville, au milieu de la gorge de Gad et d'Eliézer.
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
Ils allèrent ensuite en Galaad et dans la terre de Thabason, la même qu'Adasaï; ils passèrent par Danidan, par Udan, et ils firent le tour de Sidon.
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
Puis, ils allèrent à Mapsar de Tyr, et dans toutes les villes de l'Evéen et du Chananéen; et ils retournèrent au sud de Juda en Bersabée.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
Et ils parcoururent toute la terre; enfin, ils rentrèrent à Jérusalem au bout de neuf mois et vingt jours.
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
Et Joab remit au roi le dénombrement du peuple qu'il avait recensé. Il y avait en Israël huit cent mille hommes dans la force de l'âge, portant l'épée, et en Juda cinq cent mille combattants.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Et le cœur de David le tourmenta, après qu'il eut compté le peuple, et il dit au Seigneur: J'ai gravement péché en ce que je viens de faire, ô Seigneur; remettez à votre serviteur son iniquité, car j'ai commis une insigne folie.
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
Et David se leva de grand matin, et la parole du Seigneur vint à Gad le voyant, le prophète, et le Seigneur lui dit:
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
Va, et parle à David, disant: Voici ce que dit le Seigneur: Je t'apporte trois choses: choisis pour toi l'une d'elles, et tu l'auras.
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
Et Gad entra chez le roi, lui parla, et lui dit: Choisis pour toi ce que tu veux qui arrive; il y aura ou trois années de famine en ta terre, ou trois mois, pendant lesquels tu fuiras devant tes ennemis qui te poursuivront, ou trois jours de mortalité dans ton royaume. Réfléchis, et vois ce que je dois répondre à Celui qui m'envoie.
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
Et David dit à Gad: De toutes parts le choix m'est cruel; mais j'aime mieux me livrer aux mains du Seigneur, parce qu'il a eu souvent compassion de moi; je ne tomberai point dans les mains des hommes.
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
David choisit donc la mortalité; or, on était au temps de la moisson; et le Seigneur envoya la mort en Israël depuis le point du jour jusqu'à midi; la peste commença à frapper le peuple, et, de Dan à Bersabée, soixante-dix mille hommes périrent.
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
Et l'ange de Dieu étendit la main sur Jérusalem pour la détruire; mais le Seigneur eut compassion de ses maux, et il dit à l'ange exterminateur qui détruisait le peuple: C'est assez, arrête ta main. Or, l'ange du Seigneur était auprès de l'aire d'Orna le Jébuséen.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
David, quand il vit l'ange du Seigneur frapper le peuple, parla au Seigneur, et lui dit: Me voici, c'est moi qui ai péché; mais ces brebis qu'ont-elles fait? Que votre main soit contre moi et contre la maison de mon père.
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
Et ce jour-là, Gad vint à David, et il lui dit: Lève-toi, et dresse un autel au Seigneur dans l'aire d'Orna le Jébuséen.
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
Et David se leva, comme le lui prescrivait Gad, et comme à Gad l'avait prescrit le Seigneur.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
Orna était penché à sa fenêtre, et voyant le roi qui venait à lui avec ses serviteurs, il sortit, se prosterna devant le roi la face contre terre,
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
Et dit: Pourquoi le roi mon maître est-il venu chez son serviteur? David répondit: C'est pour t'acheter ton aire, et y bâtir un autel au Seigneur, afin que cette peste cesse d'atteindre le peuple.
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
Et Orna dit à David: Que le roi mon maître prenne et consacre ce que bon lui semble; voici mes bœufs pour l'holocauste; les jougs et le chariot serviront à les brûler.
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Ainsi, Orna donna tout au roi, et il lui dit: Que le Seigneur ton Dieu te bénisse.
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
Mais le roi repartit: Je n'accepte point, je t'achèterai ce que tu m'offres, moyennant un bon prix; je ne présenterai point au Seigneur un holocauste qui ne me coûte rien. Et David acheta l'aire avec les bœufs cinquante sicles d'argent.
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
Aussitôt, David bâtit l'autel au Seigneur; puis, il y offrit des holocaustes et des hosties pacifiques. Salomon embellit plus tard l'autel, qui était d'abord fort petit. Pour le moment, le Seigneur exauça les vœux de la terre, et la peste cessa en Israël.