< 2 Samweli 24 >

1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
And the strong veniaunce of the Lord addide to be wrooth ayens Israel, and he stiride in hem Dauid, seiynge to Joab, Go thou, and noumbre thou Israel and Juda.
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
And the kyng seide to Joab, the prince of his oost, Go thou bi alle lynagis of Israel fro Dan `til to Bersabee, and noumbre thou the puple, that Y wite the noumbre therof.
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
And Joab seide to the kyng, Thi Lord God encresse to this puple, `hou greet it is now, and eft multiplie he an hundrid fold in the siyt of my lord the kyng; but what wole my lord the kyng to hym silf in sich a thing?
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
Sotheli the word of the kyng ouer cam the wordis of Joab, and of the princes of the oost; and Joab yede out, and the princes of the knyytis, fro the face of the kyng, that thei schulden noumbre the puple of Israel.
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
And whanne thei hadden passid Jordan, thei camen in to Aroer, to the riyt side of the citee which is in the valei of Gad;
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
and thei passiden bi Jazer in to Galaad, and in to the lowere lond of Odsi, and camen in to the wodi places of Dan; and thei cumpassiden bisidis Sidon,
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
and passiden nyy the wallis of Tire, and nyy al the lond of Euei, and of Chananei; and thei camen to the south of Juda, in Bersabee.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
And whanne al the lond was cumpassid, thei camen aftir nyne monethis and twenti daies in to Jerusalem.
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
Therfor Joab yaf the noumbre of discriuyng of the puple to the kyng. And of Israel weren foundun nyne hundryd thousynd of stronge men, that drewen out swerd; and of Juda fyue hundrid thousynde of fiyteris.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
Forsothe the herte of Dauid smoot hym, `that is, his concience repreuyde hym, aftir that the puple was noumbrid; and Dauid seide to the Lord, Y synnede greetli in this dede; but, Lord, Y preye that thou turne awei the wickidnesse of thi seruaunt, for Y dide ful folili.
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
Therfor Dauid roos eerli, and the word of the Lord was maad to Gad, the prophete and seere, and seide, Go thou,
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
and speke to Dauid, The Lord seith these thingis, The chesyng of thre thingis is youun to thee; chese thou oon, which thou wolt of these, that Y do to thee.
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
And whanne Gad hadde come to Dauid, he telde to Dauid, and seide, Ether hungur schal come to thee in thi lond seuene yeer; ethir thre monethis thou schalt fle thin aduersaries, and thei schulen pursue thee; ether certis thre daies pestilence schal be in thi lond; now therfor delyuere thou, `ether auyse thou, and se, what word Y schal answere to hym that sente me.
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
Forsothe Dauid seide to Gad, Y am constreyned on ech side greetli; but it is betere that Y falle in to the hondis of the Lord, for his emercies ben manye, than in the hondis of men.
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
And the Lord sente pestilence in to Israel fro the morewtid `til to the tyme ordeyned; and seuenti thousynde of men weren deed of the puple fro Dan `til to Bersabee.
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
And whanne the aungel of the Lord hadde holde forth his hond ouer Jerusalem, that he schulde distrie it, the Lord hadde mercy on the turmentyng; and seide to the aungel smytynge the puple, It sufficith now; withholde thin hond. Forsothe the aungel of the Lord was bisidis the corn floor of Areuna Jebusey.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
And Dauid seide to the Lord, whanne he hadde seyn the aungel sleynge the puple, Y am he that `haue synned, and Y dide wickidli; what han these do, that ben scheep? Y biseche, thin hond be turned ayens me, and ayens the hows of my fadir.
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
Forsothe Gad, the prophete, cam to Dauid in that dai, and seide to hym, Stie thou, and ordeyne an auter to the Lord in the corn floor of Areuna Jebusei.
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
And Dauid stiede, vpe the word of Gad, which the Lord hadde comaundid to hym.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
And Areuna bihelde, and perseyuede, that the kyng and hise seruauntis passiden to hym;
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
and he yede out, and worschipide the kyng bi low cheer to the erthe; and seide, What `cause is, that my lord the kyng cometh to his seruaunt? To whom Dauid seide, That Y bie of thee the corn floor, and bilde an auter to the Lord, and the sleynge ceesse, which is cruel in the puple.
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
And Areuna seide to Dauid, My lord the kyng take, and offre, as it plesith hym; thou hast oxis in to brent sacrifice, and a wayn and yockis of oxis in to vss of wode.
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Areuna yaf alle thingis to the king. And Areuna seide to the king, Thi Lord God reseyue thi vow.
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
To whom the king answeride, and seide, Not as thou wolt, but Y schal bie of thee for prijs, and Y schal not offre to `my Lord God brent sacrifices youun freli. Therfor Dauid bouyte the corn floor, and `he bouyte oxis for fifti siclis of siluer.
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
And Dauid bildide there an auter to the Lord, and offride brent sacrifices and pesible sacrifices; and the Lord dide merci to the lond, and the veniaunce was refreyned fro Israel.

< 2 Samweli 24 >