< 2 Samweli 24 >

1 Hasira ya Bwana ikawaka tena dhidi ya Israeli, naye akamchochea Daudi dhidi yao, akisema, “Nenda ukawahesabu Israeli na Yuda.”
And the anger of YHWH adds to burn against Israel, and [an adversary] moves David about them, saying, “Go, number Israel and Judah.”
2 Kwa hiyo mfalme akamwambia Yoabu, pamoja na majemadari wa jeshi aliokuwa nao, “Nendeni kwa makabila yote ya Israeli kuanzia Dani hadi Beer-Sheba na mwandikishe watu wapiganaji, ili niweze kujua idadi yao.”
And the king says to Joab, head of the host that [is] with him, “Now go to and fro through all the tribes of Israel, from Dan even to Beer-Sheba, and inspect the people; then I have known the number of the people.”
3 Lakini Yoabu akamjibu mfalme, “Bwana Mungu wako na azidishe jeshi mara mia, nayo macho ya bwana wangu mfalme na yaone hili. Lakini kwa nini bwana wangu mfalme anataka kufanya kitu cha namna hii?”
And Joab says to the king, “Indeed, your God YHWH adds to the people, as they are, one hundred times, and the eyes of my lord the king are seeing; and my lord the king, why is he desirous of this thing?”
4 Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu pamoja na majemadari wa jeshi, kwa hiyo wakaondoka mbele ya mfalme kuandikisha wapiganaji wa Israeli.
And the word of the king is severe toward Joab, and against the heads of the force, and Joab goes out, and the heads of the force, [from] before the king to inspect the people, even Israel;
5 Baada ya kuvuka Yordani, walipiga kambi karibu na Aroeri, kusini ya mji ulioko kwenye bonde jembamba, ndipo wakipitia Gadi, wakaenda hadi Yazeri.
and they pass over the Jordan, and encamp in Aroer, on the right of the city that [is] in the midst of the Brook of Gad, and to Jazer,
6 Walikwenda hadi Gileadi na pia eneo la Tahtimu-Hodshi, wakaendelea hadi Dani-Yaani na kuzunguka kuelekea Sidoni.
and they come to Gilead, and to the land of Tahtim-Hodshi, and they come to Dan-Jaan, and around to Sidon,
7 Kisha wakaenda kuelekea ngome ya Tiro pamoja na miji yote ya Wahivi na ya Wakanaani. Mwishoni, walikwenda mpaka Beer-Sheba katika Negebu ya Yuda.
and they come to the fortress of Tyre, and all the cities of the Hivite, and of the Canaanite, and go out to the south of Judah, to Beer-Sheba.
8 Baada ya kupita katika nchi nzima, walirudi Yerusalemu baada ya miezi tisa na siku ishirini.
And they go to and fro through all the land, and come in to Jerusalem at the end of nine months and twenty days,
9 Yoabu akatoa hesabu ya wapiganaji kwa mfalme: Katika Israeli kulikuwako watu 800,000 wenye uwezo wa kupigana, na katika Yuda watu 500,000.
and Joab gives the account of the inspection of the people to the king, and Israel is eight hundred thousand men of valor, drawing sword, and the men of Judah five hundred thousand men.
10 Dhamiri ya Daudi ilishtuka baada ya kuwahesabu wapiganaji, naye akamwambia Bwana, “Nimefanya dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Ee Bwana, sasa ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
And the heart of David strikes him, after that he has numbered the people, and David says to YHWH, “I have greatly sinned in that which I have done, and now, O YHWH, please cause the iniquity of Your servant to pass away, for I have acted very foolishly.”
11 Kabla Daudi hajaamka kesho yake asubuhi, neno la Bwana lilikuwa limemjia Gadi nabii, aliyekuwa mwonaji wa Daudi, kusema:
And David rises in the morning, and the word of YHWH has been to Gad the prophet, seer of David, saying,
12 “Nenda ukamwambie Daudi, ‘Hivi ndivyo asemavyo Bwana: Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
“Go, and you have spoken to David, Thus said YHWH: I am lifting up three [choices] for you, choose one of them, and I do [it] to you.”
13 Basi Gadi akaenda kwa Daudi na kumwambia, “Je, ije njaa ya miaka mitatu katika nchi yako? Au miezi mitatu ya kukimbia adui zako wakikufuatia? Au siku tatu za tauni katika nchi yako? Basi sasa, fikiri juu ya hilo na uamue jinsi nitakavyomjibu huyo aliyenituma.”
And Gad comes to David, and declares [it] to him, and says to him, “Does seven years of famine come to you in your land? Or are you fleeing before your adversary [for] three months—and he is pursuing you? Or is there pestilence [for] three days in your land? Now, know and see what word I take back to Him sending me.”
14 Daudi akamjibu Gadi, “Nitataabika sana. Afadhali tuangukie mikononi mwa Bwana, kwa maana rehema zake ni kuu, lakini usiniache nianguke mikononi mwa wanadamu.”
And David says to Gad, “I have great distress; please let us fall into the hand of YHWH, for His mercies [are] many, but do not let me fall into the hand of man.”
15 Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli kuanzia asubuhi mpaka mwisho wa muda ulioamriwa, wakafa watu 70,000 kuanzia Dani hadi Beer-Sheba.
And YHWH gives a pestilence on Israel from the morning even to the time appointed, and there dies of the people, from Dan even to Beer-Sheba, seventy thousand men,
16 Malaika aliponyoosha mkono wake ili kuangamiza Yerusalemu, Bwana akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anawadhuru watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna, Myebusi.
and the messenger puts forth his hand to Jerusalem to destroy it, and YHWH sighs concerning the calamity, and says to the messenger who is destroying among the people, “Enough, now, cease your hand”; and the messenger of YHWH was near the threshing-floor of Araunah the Jebusite.
17 Ikawa Daudi alipomwona huyo malaika aliyekuwa akiwaua watu, akamwambia Bwana, “Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Mkono wako uwe juu yangu na nyumba yangu.”
And David speaks to YHWH when he sees the messenger who is striking among the people, and says, “Behold, I have sinned, indeed, I have done perversely; and these—the flock—what have they done? Please let Your hand be on me and on the house of my father.”
18 Siku hiyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia, “Panda ukamjengee Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria ya Arauna Myebusi.”
And Gad comes to David on that day and says to him, “Go up, raise an altar to YHWH in the threshing-floor of Araunah the Jebusite”;
19 Kwa hiyo Daudi akakwea kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kwa kinywa cha Gadi.
and David goes up, according to the word of Gad, as YHWH commanded.
20 Arauna alipotazama na kumwona mfalme na watu wake wakija kumwelekea, alitoka nje na kusujudu mbele ya mfalme kifudifudi, akiuinamisha uso wake ardhini.
And Araunah looks, and sees the king and his servants passing over to him, and Araunah goes out and bows himself to the king [with] his face to the earth.
21 Arauna akasema, “Mbona bwana wangu mfalme amekuja kwa mtumishi wake?” Daudi akajibu, “Kununua sakafu yako ya kupuria, ili niweze kumjengea Bwana madhabahu, ili tauni iliyo katika watu iondolewe.”
And Araunah says, “Why has my lord the king come to his servant?” And David says, “To buy the threshing-floor from you, to build an altar to YHWH, and the plague is restrained from the people.”
22 Arauna akamwambia Daudi, “Bwana wangu mfalme na achukue chochote kinachompendeza na akitoe sadaka. Hapa kuna maksai kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, pia kuna miti ya kupuria na nira za ngʼombe kwa ajili ya kuni.
And Araunah says to David, “Let my lord the king take [it] and cause that which is good in his eyes to ascend; see, [here are] the oxen for a burnt-offering, and the threshing instruments, and the instruments of the oxen, for wood”;
23 Ee mfalme, Arauna anatoa vyote hivi kwa mfalme.” Pia Arauna akamwambia mfalme, “Bwana Mungu wako na akukubali.”
Araunah has given the whole [as] a king to a king; and Araunah says to the king, “Your God YHWH accepts you.”
24 Lakini mfalme akamjibu Arauna, “La hasha, nasisitiza kuvilipia. Sitatoa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana Mungu wangu isiyonigharimu chochote.” Kwa hiyo Daudi akanunua ile sakafu ya kupuria nafaka na maksai, akazilipia shekeli hamsini za fedha.
And the king says to Araunah, “No, for I surely buy from you for a price, and I do not cause burnt-offerings to ascend to my God YHWH for nothing”; and David buys the threshing-floor and the oxen for fifty shekels of silver,
25 Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Kisha Bwana akajibu kwa ajili ya nchi, nayo tauni ikakoma katika Israeli.
and David builds an altar to YHWH there, and causes burnt-offerings and peace-offerings to ascend, and YHWH accepts the plea for the land, and the plague is restrained from Israel.

< 2 Samweli 24 >